Zaburi 32
Furaha Ya Msamaha
Zaburi ya Daudi. Funzo.
132:1 Za 85:2; 103:3; Rum 4:6Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,
ambaye dhambi zake zimefunikwa.
232:2 Rum 4:7-8; 5:13; Yn 1:47; Ufu 14:5; 2Kor 1:12; Law 17:4Heri mtu yule ambaye Bwana
hamhesabii dhambi,
na ambaye rohoni mwake
hamna udanganyifu.
332:3 Ay 31:34; 31:10; 3:24; Za 6:6Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa
kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
432:4 1Sam 5:6; Ay 9:34; Za 38:2; 39:10; 22:15Usiku na mchana
mkono wako ulinilemea,
nguvu zangu zilinyonywa
kama vile katika joto la kiangazi.
532:5 Ay 31:33; Mit 28:13; Lk 15:18; Za 103:12; Law 26:40; Yn 1:9Kisha nilikujulisha dhambi yangu
wala sikuficha uovu wangu.
Nilisema, “Nitaungama
makosa yangu kwa Bwana.”
Ndipo uliponisamehe
hatia ya dhambi yangu.
632:6 Za 69:13; Yn 7:34; Isa 55:6; Za 69:1; 43:2; Kut 15:10; 1Tim 1:16Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe
wakati unapopatikana,
hakika maji makuu yatakapofurika
hayatamfikia yeye.
732:7 Za 9:9; Amu 9:35; 5:1; Mit 18:10; Isa 4:6; Mt 23:37; Kol 3:3Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha,
utaniepusha na taabu
na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
832:8 Za 25:8; 34:11; 33:18; Isa 48:17Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;
nitakushauri na kukuangalia.
932:9 Ay 30:11; 39:10; Yak 3:3Usiwe kama farasi au nyumbu
wasio na akili,
ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu
la sivyo hawatakukaribia.
1032:10 Rum 2:9; Za 4:5; Mit 16:20; Yer 17:7; Mit 13:21; 16:20Mtu mwovu ana taabu nyingi,
bali upendo usio na kikomo wa Bwana
unamzunguka mtu anayemtumaini.
1132:11 Za 64:10Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki!
Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Psalm 32
Of David. A maskil.Title: Probably a literary or musical term
1Blessed is the one
whose transgressions are forgiven,
whose sins are covered.
2Blessed is the one
whose sin the Lord does not count against them
and in whose spirit is no deceit.
3When I kept silent,
my bones wasted away
through my groaning all day long.
4For day and night
your hand was heavy on me;
my strength was sapped
as in the heat of summer.32:4 The Hebrew has Selah (a word of uncertain meaning) here and at the end of verses 5 and 7.
5Then I acknowledged my sin to you
and did not cover up my iniquity.
I said, “I will confess
my transgressions to the Lord.”
And you forgave
the guilt of my sin.
6Therefore let all the faithful pray to you
while you may be found;
surely the rising of the mighty waters
will not reach them.
7You are my hiding place;
you will protect me from trouble
and surround me with songs of deliverance.
8I will instruct you and teach you in the way you should go;
I will counsel you with my loving eye on you.
9Do not be like the horse or the mule,
which have no understanding
but must be controlled by bit and bridle
or they will not come to you.
10Many are the woes of the wicked,
but the Lord’s unfailing love
surrounds the one who trusts in him.
11Rejoice in the Lord and be glad, you righteous;
sing, all you who are upright in heart!