Zaburi 22 – Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) NEN

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 22:1-31

Zaburi 22

Kilio Cha Uchungu Na Wimbo Wa Sifa

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi.

122:1 Za 9:10; 10:1; Mt 27:46; Ay 3:24; 6:15; Mk 15:34; Ebr 5:7Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa?

Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?

222:2 Ay 19:7; Za 42:3; 88:1Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu,

hata usiku, sinyamazi.

322:3 2Fal 19:22; Za 71:22; 148:14; Mk 1:24; Ufu 4:8; Kut 15:2; Isa 6:3Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;

wewe ni sifa ya Israeli.22:3 Tafsiri zingine zinasema: uketiye juu ya sifa za Israeli.

422:4 Za 78:53; 107:6Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao,

walikutumaini nawe ukawaokoa.

522:5 1Nya 5:20; Rum 9:33; Za 25:3; 31:17; 71:1; 2Nya 13:18; Isa 8:17; 25:9; 26:3; 30:18; 49:23Walikulilia wewe na ukawaokoa,

walikutegemea wewe nao hawakuaibika.

622:6 Ay 4:19; Mt 16:21; Mal 2:9; Isa 60:14; 49:7; 53:3; Za 119:141; 64:8; 109:25; 69:19; 2Sam 12:14Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu,

wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.

722:7 Mt 9:24; 27:41; Mk 15:20, 29, 31, 32; Lk 16:14; 23:36, 39; Mt 27:39, 44; Ay 17:2; Za 35:16; 69:12; 74:18Wote wanionao hunidhihaki,

hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

822:8 Za 91:14; 3:2; 2Sam 22:20; Mt 3:17; 27:43Husema, “Anamtegemea Bwana,

basi Bwana na amwokoe.

Amkomboe basi, kwa maana

anapendezwa naye.”

922:9 Ay 10:18; Hes 1:7; Za 71:6; 78:7Hata hivyo ulinitoa tumboni,

ukanifanya nikutegemee,

hata nilipokuwa ninanyonya

matiti ya mama yangu.

1022:10 Za 71:6; Isa 46:3; 49:1Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,

toka tumboni mwa mama yangu

umekuwa Mungu wangu.

1122:11 Za 10:1, 14; 2Fal 14:26; Isa 41:28Usiwe mbali nami,

kwa maana shida iko karibu

na hakuna wa kunisaidia.

1222:12 Za 69:30; 17:9; 27:6; 49:5; 109:3; 140:9; Kum 32:14; Isa 2:3; Eze 27:6; 39:18; Amo 4:1Mafahali wengi wamenizunguka,

mafahali wa Bashani wenye nguvu

wamenizingira.

1322:13 Eze 22:25; Sef 3:3; Mwa 49:9; 1Pet 5:8; Mao 3:6; Za 35:21Simba wangurumao wanaorarua mawindo

yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.

1422:14 Za 6:2Nimemiminwa kama maji,

mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake.

Moyo wangu umegeuka kuwa nta,

umeyeyuka ndani yangu.

1522:15 Isa 45:9; Yn 19:28; Za 137:6; 104:29; Mao 4:4; Ay 7:21; Eze 3:26Nguvu zangu zimekauka kama kigae,

ulimi wangu umegandamana

na kaakaa la kinywa changu,

kwa sababu umenilaza

katika mavumbi ya kifo.

1622:16 Flp 3:2; Isa 51:9; 53:5; Mit 17:22; Zek 12:10; Yn 20:25Mbwa wamenizunguka,

kundi la watu waovu limenizingira,

wametoboa mikono yangu na miguu yangu.

1722:17 Lk 23:35; Mik 7:8; Za 25:2; 30:1; 35:19; 38:16; Mao 2:17Naweza kuhesabu mifupa yangu yote,

watu wananikodolea macho na kunisimanga.

1822:18 Law 16:8; Yn 19:24; Mt 27:35; Mk 9:12; 15:24; Lk 23:34Wanagawana nguo zangu wao kwa wao,

na vazi langu wanalipigia kura.

1922:19 Za 18:1; 38:22; 70:5; 14:1; 40:13Lakini wewe, Ee Bwana,

usiwe mbali.

Ee Nguvu yangu,

uje haraka unisaidie.

2022:20 Ay 5:20; Za 141:1; 40:13Okoa maisha yangu na upanga,

uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.

2122:21 Ay 4:10, 12; Ebr 2:12; Hes 23:22; Za 22:13; 68:26; 40:9, 10; 35:18; 2Tim 4:17Niokoe kutoka kinywani mwa simba,

niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.

2222:22 Za 26:12; 35:18; 40:9, 10; 68:26; Ebr 2:12; Yn 20:17Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu,

katika kusanyiko nitakusifu wewe.

2322:23 Yer 3:17; Za 66:8; 33:2, 8; 103:1; 86:12; 106:1; 50:15; 113:1; 117:1; 135:19; Isa 24:15; 25:3; 49:23; 60:9; Kum 14:23Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni!

Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye!

Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!

2422:24 Ebr 5:7; Za 9:12; 102:17; 13:1; 27:9; 69:17; 102:2; 143:7; Ay 24:12; 36:5Kwa maana hakupuuza wala kudharau

mateso ya aliyeonewa;

hakumficha uso wake

bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.

2522:25 Za 26:12; 35:18; 40:9; 82:1; Hes 30:2Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa,

nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.

2622:26 Za 107:9; 40:16Maskini watakula na kushiba,

wale wamtafutao Bwana watamsifu:

mioyo yenu na iishi milele!

2722:27 Za 2:8; 86:9; 102:22; Dan 7:27; Mik 4:1Miisho yote ya dunia itakumbuka

na kumgeukia Bwana,

nazo jamaa zote za mataifa

watasujudu mbele zake,

2822:28 Za 47:7; Zek 14:9; Mt 6:13kwa maana ufalme ni wa Bwana

naye hutawala juu ya mataifa.

2922:29 Za 45:12; 89:48; 95:6; 96:9; 99:5; Isa 26:19; 27:13; 49:7; 66:23; Zek 14:16Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu.

Wote waendao mavumbini

watapiga magoti mbele yake,

wote ambao hawawezi

kudumisha uhai wao.

3022:30 Isa 53:10; 54:3; 61:9; 66:22; Za 102:18Wazao wa baadaye watamtumikia yeye;

vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.

3122:31 Za 5:8; 71:18; 78:6; 40:9; 102:18; Lk 18:31; 24:44Watatangaza haki yake kwa watu

ambao hawajazaliwa bado,

kwa maana yeye ametenda hili.