Zaburi 21 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 21:1-13

Zaburi 21

Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

121:1 1Sam 2:10; 2Sam 22:51Ee Bwana, mfalme huzifurahia nguvu zako.

Tazama jinsi ilivyo kuu furaha yake

kwa ushindi unaompa!

221:2 Za 20:4; Yn 11:42Umempa haja ya moyo wake

na hukumzuilia maombi ya midomo yake.

321:3 2Sam 12:30; Ufu 14:14; Zek 6:11Ulimkaribisha kwa baraka tele

na kumvika taji ya dhahabu safi kichwani pake.

421:4 Za 10:16; 45:17; 48:14; 133:3; 2Sam 7:19Alikuomba maisha, nawe ukampa,

wingi wa siku milele na milele.

521:5 Za 18:50; 44:4; 8:5; 45:3; 93:1; 96:6; 104:1Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa,

umeweka juu yake fahari na utukufu.

621:6 Za 43:4; 126:3; 1Nya 17:27Hakika umempa baraka za milele,

umemfanya awe na furaha

kwa shangwe ya uwepo wako.

721:7 2Fal 18:5; Za 6:4; 15:5; 55:22; 91:7; Mwa 14:18Kwa kuwa mfalme anamtumaini Bwana;

kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa.

821:8 Isa 10:10Mkono wako utawashika adui zako wote,

mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.

921:9 Kum 32:22; Yer 15:14Wakati utakapojitokeza

utawafanya kama tanuru ya moto.

Katika ghadhabu yake Bwana atawameza,

moto wake utawateketeza.

1021:10 Kum 28:18Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,

uzao wao kutoka wanadamu.

1121:11 Za 2:1; 10:2; 26:10; 37:7; Ay 10:3Ingawa watapanga mabaya dhidi yako

na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,

1221:12 Kut 23:27kwa kuwa utawafanya wakimbie

utakapowalenga usoni pao

kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.

1321:13 Za 18:46; Ufu 15:3, 4Ee Bwana, utukuzwe katika nguvu zako,

tutaimba na kusifu nguvu zako.

Ketab El Hayat

مزمور 21:1-13

الْمَزْمُورُ الْحَادِي وَالْعِشْرُونَ

لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ مِنْ نَظْمِ دَاوُدَ

1رَبُّ بِقُوَّتِكَ يَفْرَحُ الْمَلِكُ، وَمَا أَعْظَمَ بَهْجَتَهُ بِخَلاصِكَ! 2لَقَدْ وَهَبْتَهُ بُغْيَةَ قَلْبِهِ وَلَمْ تَحْرِمْهُ مِنْ طِلْبَةِ شَفَتَيْهِ. 3بَادَرْتَهُ بِبَرَكَاتِ الْخَيْرِ، وَوَضَعْتَ عَلَى رَأْسِهِ تَاجاً مِنَ الذَّهَبِ النَّقِيِّ! 4طَلَبَ مِنْكَ الْحَيَاةَ فَوَهَبْتَهَا لَهُ، إِذْ أَطَلْتَ عُمْرَهُ إِلَى أَبَدِ الدُّهُورِ. 5عَظِيمٌ مَجْدُهُ بِفَضْلِ خَلاصِكَ، بِالْعِزَّةِ وَالْبَهَاءِ كَلَّلْتَهُ. 6لأَنَّكَ جَعَلْتَهُ أَكْثَرَ الْمُبَارَكِينَ إِلَى الأَبَدِ. تَغْمُرُهُ بِفَيْضِ الْفَرَحِ فِي حَضْرَتِكَ. 7لأَنَّ الْمَلِكَ يَتَوَكَّلُ عَلَى الرَّبِّ، وَبِنِعْمَةِ الْعَلِيِّ لَا يَتَزَعْزَعُ.

8يَدُكَ حَتْماً تَنَالُ جَمِيعَ أَعْدَائِكَ، وَيُمْنَاكَ حَقّاً تَظْفَرُ بِمُبْغِضِيكَ. 9حِينَ يَتَجَلَّى وَجْهُكَ تُحْرِقُهُمْ كَمَا بِمَوْقِدٍ مُشْتَعِلٍ. تَلْتَهِمُهُمْ فِي غَضَبِكَ فَتَأْكُلُهُمُ النَّارُ. 10تُبِيدُ ذُرِّيَّتَهُمْ مِنَ الأَرْضِ وَنَسْلَهُمْ مِنْ بَيْنِ بَنِي آدَمَ. 11لَقَدْ تَآمَرُوا لِلإِسَاءَةِ إِلَيْكَ، وَدَبَّرُوا مَكِيدَةً شِرِّيرَةً لَمْ يُفْلِحُوا فِيهَا. 12لأَنَّكَ تَجْعَلُهُمْ يُدْبِرُونَ لِلْهَرَبِ، عِنْدَمَا تَشُدُّ وَتَرَ الْقَوْسِ نَحْوَ وُجُوهِهِمْ. 13ارْتَفِعْ يَا رَبُّ بِقُوَّتِكَ، فَنَتَرَنَّمَ وَنَتَغَنَّى بِقُدْرَتِكَ.