Zaburi 19 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 19:1-14

Zaburi 19

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

119:1 Isa 6:3; 40:22; Za 4:2; 97:6; 89:5; 50:6; 8:1, 6; 148:3; 103:22; Rum 1:19; Mwa 1:8Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,

anga zahubiri kazi ya mikono yake.

219:2 Za 74:16Siku baada ya siku zinatoa habari,

usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.

3Hakuna msemo wala lugha,

ambapo sauti zao hazisikiki.

419:4 Rum 10:18; Za 104:2; Ay 36:29; Amu 5:31Sauti yao imeenea duniani pote,

nayo maneno yao yameenea

hadi miisho ya ulimwengu.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,

519:5 1Sam 17:4; Mhu 11:7; Yoe 2:16; Ay 36:29linafanana na bwana arusi

akitoka chumbani mwake,

kama shujaa afurahiavyo

kukamilisha kushindana kwake.

619:6 Kum 30:4; Za 11:3; Mhu 1:5Huchomoza upande mmoja wa mbingu,

na kufanya mzunguko wake

hadi upande mwingine.

Hakuna kilichojificha joto lake.

719:7 Yak 1:25; Kum 4:6; Za 1:2; 23:3; 93:5; 119:130, 138, 142, 144; 11:7Sheria ya Bwana ni kamilifu,

ikihuisha nafsi.

Shuhuda za Bwana ni za kuaminika,

zikimpa mjinga hekima.

819:8 Za 33:4; 38:10; 119:14, 128; Ezr 9:7; Neh 9:13; Rum 7:12Maagizo ya Bwana ni kamili,

nayo hufurahisha moyo.

Amri za Bwana huangaza,

zatia nuru machoni.

919:9 Mhu 12:13; Isa 33:6; Za 34:11; 111:10; 119:138; Mit 1:7Kumcha Bwana ni utakatifu,

nako kwadumu milele.

Amri za Bwana ni za hakika,

nazo zina haki.

1019:10 Ay 22:24; Eze 3:3; Mit 8:10; 1Sam 14:27; Za 119:72, 103Ni za thamani kuliko dhahabu,

kuliko dhahabu iliyo safi sana,

ni tamu kuliko asali,

kuliko asali kutoka kwenye sega.

1119:11 Mit 6:22Kwa hizo mtumishi wako anaonywa,

katika kuzishika kuna thawabu kubwa.

1219:12 Za 51:2; 90:8; Mhu 12:14Ni nani awezaye kutambua makosa yake?

Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.

1319:13 Hes 15:30; Mwa 6:9; Za 18:32; 119:133Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi,

nazo zisinitawale.

Ndipo nitakapokuwa sina lawama,

wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.

1419:14 Za 104:34; 18:31; Kut 6:6; Isa 44:6; Ay 19:25Maneno ya kinywa changu

na mawazo ya moyo wangu,

yapate kibali mbele zako, Ee Bwana,

Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

Hoffnung für Alle

Psalm 19:1-15

Gottes gute Ordnungen in der Schöpfung und in seinem Gesetz

1Ein Lied von David.

2Der Himmel verkündet Gottes Hoheit und Macht,

das Firmament bezeugt seine großen Schöpfungstaten.

3Ein Tag erzählt dem nächsten davon,

und eine Nacht sagt es der anderen weiter.

4Dies alles geschieht ohne Worte,

ohne einen vernehmlichen Laut.

5Doch auf der ganzen Erde hört man diese Botschaft,

sie erreicht noch die fernsten Länder.

Der Sonne hat Gott am Himmel ein Zelt aufgeschlagen.

6Am Morgen kommt sie strahlend heraus

wie ein Bräutigam aus seiner Kammer.

Siegesgewiss wie ein Held beginnt sie ihren Lauf;

7am fernen Horizont geht sie auf

und wandert von einem Ende des Himmels zum andern.

Nichts bleibt vor ihrer Hitze verborgen.

8Das Gesetz des Herrn ist vollkommen,

es belebt und schenkt neue Kraft.

Auf seine Gebote kann man sich verlassen.

Sie machen auch den klug,

der bisher gedankenlos in den Tag hineinlebte.

9Die Weisungen des Herrn sind zuverlässig

und erfreuen das Herz.

Die Befehle des Herrn sind klar;

Einsicht gewinnt, wer auf sie achtet.

10Die Ehrfurcht vor dem Herrn ist gut, nie wird sie aufhören.

Die Gebote, die der Herr gegeben hat,

sind richtig, vollkommen und gerecht.

11Sie lassen sich nicht mit Gold aufwiegen,

sie sind süßer als der beste Honig.

12Herr, ich will dir dienen.

Wie gut, dass mich dein Gesetz vor falschen Wegen warnt!

Wer sich an deine Gebote hält, wird reich belohnt.

13Wer aber kann erkennen, ob er nicht doch vom rechten Weg abkommt?

Vergib mir die Verfehlungen, die mir selbst nicht bewusst sind!

14Bewahre mich vor mutwilligen Sünden19,14 Oder: vor gewissenlosen Menschen.

und lass nicht zu, dass sie Macht über mich gewinnen;

dann werde ich dir nie mehr die Treue brechen

und frei sein von schwerer Schuld.

15Herr, lass dir meine Worte und Gedanken gefallen!

Du bist mein schützender Fels, mein starker Erlöser!