Zaburi 145 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 145:1-21

Zaburi 145145:1 Zaburi hii imetungwa kila mstari (ikiwa ni pamoja na 13b) ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.

Wimbo Wa Kusifu Ukuu Na Wema Wa Mungu

Wimbo wa Sifa. Wa Daudi.

1145:1 Za 30:1; 34:1; 2:6; 5:2; 54:6Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme,

nitalisifu jina lako milele na milele.

2145:2 Za 71:6; 34:1; Isa 25:1; 26:8Kila siku nitakusifu

na kulitukuza jina lako milele na milele.

3145:3 2Sam 22:4; Ay 5:9; Za 95:3; 96:4Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana,

ukuu wake haupimiki.

4145:4 Za 22:30; 71:16; Kum 11:19Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine,

watasimulia matendo yako makuu.

5145:5 Za 96:6; 148:13; 75:1Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako,

nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.

6145:6 Kum 32:3; Za 75:1; 78:4; 66:3; 106:2Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha,

nami nitatangaza matendo yako makuu.

7145:7 Kut 18:9; Za 5:11; 27:13; 138:5; 101:1Wataadhimisha wema wako mwingi,

na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.

8145:8 Za 57:10; 86:15; 103:8; Kut 34:6; Hes 14:18; Yn 1:17; Mao 3:22Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.

9145:9 1Nya 16:34; Mt 19:17; Nah 1:7; Mk 10:18; Mdo 14:17; Za 103:13, 14; 136:1; 100:5Bwana ni mwema kwa wote,

ana huruma kwa vyote alivyovifanya.

10145:10 Za 8:6; 103:22; 139:14; 148:14; 19:1; 149:9; 30:4; 115:17-18Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu,

watakatifu wako watakutukuza.

11Watasimulia utukufu wa ufalme wako

na kusema juu ya ukuu wako,

12145:12 Za 103:19; 105:1; 75:1; Isa 2:10, 19, 21ili watu wote wajue matendo yako makuu

na utukufu wa fahari ya ufalme wako.

13145:13 Kut 15:18; 1Tim 1:17; 2Pet 1:11; Ufu 11:15; Kum 7:9; 1Kor 1:9; Yos 23:14Ufalme wako ni ufalme wa milele,

mamlaka yako hudumu vizazi vyote.

Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote

na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.

14145:14 Za 37:17; 146:8; 38:6; 1Sam 2:8Bwana huwategemeza wote waangukao,

na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.

15145:15 Mwa 1:30; Ay 28:5; Mt 6:26; Za 37:25Macho yao wote yanakutazama wewe,

nawe huwapa chakula chao wakati wake.

16145:16 Za 90:14; 104; 28Waufumbua mkono wako,

watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.

17145:17 Kut 9:27; Ezr 9:15Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote,

na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.

18145:18 Flp 4:5; Za 46:1; 18:6; 80:18; 91:1; Isa 61:10; Ufu 3:20; Yak 4:8; 1Yn 2:24; Yud 23; Yn 4:23; 14:23; Hes 23:21Bwana yu karibu na wote wamwitao,

karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.

19145:19 1Yn 5:14; Za 20:4; 31:22; 40:1; 7:10; 34:18; 1Sam 10:19; Ay 22:28Huwatimizia wamchao matakwa yao,

husikia kilio chao na kuwaokoa.

20145:20 Za 94:23; 31:23; 91:14; 97:10; 1:6; 1Pet 1:5Bwana huwalinda wote wampendao,

bali waovu wote atawaangamiza.

21145:21 Za 71:8; 65:2; 150:6; 30:4; 99:3; Kut 3:15Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana.

Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu

milele na milele.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 145:1-21

第 145 篇

赞美之歌

大卫的赞美诗。

1我的上帝,我的王啊!

我要尊崇你,

我要永永远远称颂你的名。

2我要天天称颂你,

永永远远赞美你的名。

3耶和华是伟大的,

当受至高的颂赞,

祂的伟大无法测度。

4愿世世代代颂赞你的事迹,

传扬你大能的作为。

5我要默想你的荣耀、威严和奇妙作为。

6人们要述说你令人敬畏的大能作为,

我也要传扬你的伟大事迹。

7他们要诉说你的厚恩,

歌颂你的公义。

8耶和华有恩典和怜悯,

不轻易发怒,充满慈爱。

9耶和华善待万民,

怜悯祂所造的万物。

10耶和华啊,

你所创造的万物都要称谢你,

你忠心的子民也要称颂你。

11他们要述说你国度的荣耀,

讲论你的大能,

12好让世人知道你大能的作为和你国度的威严与荣耀。

13你的国度永远长存,

你的统治直到万代。

耶和华信守自己的一切应许,

以慈爱待祂所创造的万物。145:13 耶和华信守……万物”许多手抄本无此句。

14耶和华扶起跌倒的人,

扶持被重担所压的人。

15世人都仰赖你,

你按时赐给他们所需的食物。

16你慷慨满足一切生命的需要。

17耶和华的作为公义,

祂所行的充满慈爱。

18耶和华垂顾一切求告祂的人,

一切诚心求告祂的人。

19祂使敬畏祂的人心愿得偿,

垂听他们的呼求,拯救他们。

20耶和华保护所有爱祂的人,

毁灭一切恶人。

21我要开口赞美耶和华,

万物都要称颂祂的圣名,

直到永永远远。