Zaburi 143 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 143:1-12

Zaburi 143

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Adui

Zaburi ya Daudi.

1143:1 Za 141:1; 28:2; 130:2; 89:1-2Ee Bwana, sikia sala yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie;

katika uaminifu na haki yako

njoo unisaidie.

2143:2 Za 14:3; Rum 3:10; Ay 14:3; 4:17; Mhu 7:20; Gal 2:16Usimhukumu mtumishi wako,

kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.

3143:3 Za 107:10; 7:1, 2; Law 3:6Adui hunifuatilia,

hunipondaponda chini;

hunifanya niishi gizani

kama wale waliokufa zamani.

4143:4 Za 30:7Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu,

moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.

5143:5 Za 77:6; 77:5, 11; Mwa 24:63Nakumbuka siku za zamani;

natafakari juu ya kazi zako zote,

naangalia juu ya kazi

ambazo mikono yako imezifanya.

6143:6 Kut 9:29; Ay 11:13; Za 28:2Nanyoosha mikono yangu kwako,

nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.

7143:7 Za 69:17; 142:3; 22:24; 27:9; 30:7Ee Bwana, unijibu haraka,

roho yangu inazimia.

Usinifiche uso wako,

ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.

8143:8 Kut 33:13; Ay 34:32; Za 6:4; 90:14; 27:11; 32:8; 25:1-2; 86:4Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma,

kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako.

Nionyeshe njia nitakayoiendea,

kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.

9143:9 Za 140:1; 18:17; 31:15Ee Bwana, uniokoe na adui zangu,

kwa kuwa nimejificha kwako.

10143:10 Za 119:12; 31:14; 25:4-5; 26:11; Neh 9:20; Yn 14:26; Rum 5:5; Efe 4:30; Gal 5:22, 23Nifundishe kufanya mapenzi yako,

kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu,

Roho wako mwema na aniongoze

katika nchi tambarare.

11143:11 Za 25:11; 41:2; 31:1; 71:2Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu,

kwa haki yako nitoe katika taabu.

12143:12 Za 8:2; 54:5; 116:16Kwa upendo wako usiokoma,

nyamazisha adui zangu;

waangamize watesi wangu wote,

kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

Het Boek

Psalmen 143:1-12

1Een psalm van David.

Here, luister naar mijn bidden,

hoor toch hoe ik smeek.

U bent trouw en rechtvaardig,

antwoord mij dan ook.

2Oordeel uw dienaar niet,

want geen mens is in uw ogen rechtvaardig.

3Mijn vijand achtervolgt mij.

Hij wil mij doden en mij het dodenrijk injagen,

de duisternis in.

4Ik weet mij geen raad meer

en ben zo verschrikkelijk bang.

5Ik denk aan vroeger

en aan wat U toen allemaal deed.

Alles wat U hebt gedaan en gemaakt,

trekt aan mijn geestesoog voorbij.

6Ik strek mijn handen naar U uit.

Ik verlang naar U

zoals droog land naar water verlangt.

7Geef mij snel antwoord, Here,

want ik houd het niet meer uit.

Verberg U niet voor mij,

want dan kan ik beter sterven.

8Laat mij ʼs morgens vroeg al

uw goedheid en liefde ervaren.

Ik vertrouw U volkomen.

Laat mij weten welke weg ik moet inslaan.

Alles in mij richt zich op U.

9Here, bevrijd mij van mijn tegenstanders,

ik vlucht naar U.

10Leer mij te doen wat U van mij vraagt.

U bent mijn God, de goedheid Zelf.

Uw Geest leidt mij op een effen weg.

11Here, laat mij leven tot eer van uw naam.

U bent rechtvaardig.

Haal mij uit deze ellende en moeilijkheden.

12Betoon uw goedheid en liefde

en vernietig mijn tegenstanders.

Ik ben uw dienaar.

Slaat U ieder neer die mij naar het leven staat.