Zaburi 142
Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Watesi
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi.
1142:1 1Fal 8:52; Za 3:4; 30:8Namlilia Bwana kwa sauti,
nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
2142:2 Za 64:1; 50:15Namimina malalamiko yangu mbele zake,
mbele zake naeleza shida zangu.
3142:3 Za 6:2; 77:3; 84:2; 88:4; 143:4, 7; Yer 4:18; Mao 1:22Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu,
wewe ndiwe unajua njia zangu.
Katika njia ninayopita
watu wameniwekea mtego.
4142:4 Yer 25:35; 30:17Tazama kuume kwangu na uone,
hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.
Sina kimbilio,
hakuna anayejali maisha yangu.
5142:5 Za 16:5; 27:13; 46:1; Kum 32:9; Ay 28:13; Mao 3:24Ee Bwana, nakulilia wewe,
nasema, “Wewe ni kimbilio langu,
fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6142:6 Za 17:1; 79:8; 25:20; Yer 31:11Sikiliza kilio changu,
kwa sababu mimi ni mhitaji sana;
niokoe na wale wanaonifuatilia,
kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7142:7 Za 66:11; 7:17; 9:2; 2Nya 6:41Nifungue kutoka kifungo changu,
ili niweze kulisifu jina lako.
Ndipo wenye haki watanizunguka,
kwa sababu ya wema wako kwangu.