Zaburi 140 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 140:1-13

Zaburi 140

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1140:1 Za 17:13; 25:20; 59:2; 71:4; 142:6; 143:9; 86:14Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu;

nilinde na watu wenye jeuri,

2140:2 Mit 6:14; 16:27; Isa 59:4; Hos 7:15; Za 36:4; 52:2; 68:30ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao,

na kuchochea vita siku zote.

3140:3 Za 57:4; 58:4; Rum 3:13; Yak 3:8Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka,

sumu ya nyoka iko midomoni mwao.

4140:4 Za 141:9; 36:11Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu;

nilinde na watu wenye jeuri

wanaopanga kunikwaza miguu yangu.

5140:5 Ay 34:30; Za 31:4; 38:12; 119:110; Ay 18:8; 18:9Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa,

wametandaza kamba za wavu wao,

wametega mitego kwenye njia yangu.

6140:6 Za 16:2; 28:2, 6Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.”

Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.

7Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,

unikingaye kichwa changu siku ya vita:

8140:8 Za 10:2-3; 66:7; Ay 5:12-13Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao,

usiache mipango yao ikafanikiwa,

wasije wakajisifu.

9140:9 Mit 18:7Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe

na shida zinazosababishwa na midomo yao.

10140:10 Za 11:6; 21:9; Mt 3:10; Lk 12:40; Ufu 20:15Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie!

Na watupwe motoni,

katika mashimo ya matope,

wasiinuke tena kamwe.

11140:11 Za 34:21Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi;

maafa na yawawinde watu wenye jeuri.

12140:12 1Fal 8:45; Za 35:10; 82:3; 109:31Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki,

na kuitegemeza njia ya mhitaji.

13140:13 Za 138:2; 11:7; 16:11Hakika wenye haki watalisifu jina lako,

na waadilifu wataishi mbele zako.

King James Version

Psalms 140:1-13

To the chief Musician, A Psalm of David.

1Deliver me, O LORD, from the evil man: preserve me from the violent man;140.1 violent…: Heb. man of violences

2Which imagine mischiefs in their heart; continually are they gathered together for war.

3They have sharpened their tongues like a serpent; adders’ poison is under their lips. Selah.

4Keep me, O LORD, from the hands of the wicked; preserve me from the violent man; who have purposed to overthrow my goings.

5The proud have hid a snare for me, and cords; they have spread a net by the wayside; they have set gins for me. Selah.

6I said unto the LORD, Thou art my God: hear the voice of my supplications, O LORD.

7O GOD the Lord, the strength of my salvation, thou hast covered my head in the day of battle.

8Grant not, O LORD, the desires of the wicked: further not his wicked device; lest they exalt themselves. Selah.140.8 lest…: or, let them not be exalted

9As for the head of those that compass me about, let the mischief of their own lips cover them.

10Let burning coals fall upon them: let them be cast into the fire; into deep pits, that they rise not up again.

11Let not an evil speaker be established in the earth: evil shall hunt the violent man to overthrow him.140.11 an…: or, an evil speaker (Heb. a man of tongue), a wicked man of violence, be established in the earth: let him be hunted to his overthrow

12I know that the LORD will maintain the cause of the afflicted, and the right of the poor.

13Surely the righteous shall give thanks unto thy name: the upright shall dwell in thy presence.