Zaburi 140 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 140:1-13

Zaburi 140

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1140:1 Za 17:13; 25:20; 59:2; 71:4; 142:6; 143:9; 86:14Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu;

nilinde na watu wenye jeuri,

2140:2 Mit 6:14; 16:27; Isa 59:4; Hos 7:15; Za 36:4; 52:2; 68:30ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao,

na kuchochea vita siku zote.

3140:3 Za 57:4; 58:4; Rum 3:13; Yak 3:8Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka,

sumu ya nyoka iko midomoni mwao.

4140:4 Za 141:9; 36:11Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu;

nilinde na watu wenye jeuri

wanaopanga kunikwaza miguu yangu.

5140:5 Ay 34:30; Za 31:4; 38:12; 119:110; Ay 18:8; 18:9Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa,

wametandaza kamba za wavu wao,

wametega mitego kwenye njia yangu.

6140:6 Za 16:2; 28:2, 6Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.”

Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.

7Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,

unikingaye kichwa changu siku ya vita:

8140:8 Za 10:2-3; 66:7; Ay 5:12-13Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao,

usiache mipango yao ikafanikiwa,

wasije wakajisifu.

9140:9 Mit 18:7Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe

na shida zinazosababishwa na midomo yao.

10140:10 Za 11:6; 21:9; Mt 3:10; Lk 12:40; Ufu 20:15Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie!

Na watupwe motoni,

katika mashimo ya matope,

wasiinuke tena kamwe.

11140:11 Za 34:21Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi;

maafa na yawawinde watu wenye jeuri.

12140:12 1Fal 8:45; Za 35:10; 82:3; 109:31Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki,

na kuitegemeza njia ya mhitaji.

13140:13 Za 138:2; 11:7; 16:11Hakika wenye haki watalisifu jina lako,

na waadilifu wataishi mbele zako.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 140:1-13

第 140 篇

祈求上帝保护

大卫的诗,交给乐长。

1耶和华啊!

求你拯救我脱离恶人,

保护我脱离残暴之徒。

2他们心怀叵测,整天挑拨离间。

3他们的言语恶毒如蛇,

嘴唇有蛇的毒液。(细拉)

4耶和华啊,

求你使我免遭恶人的毒手,

保护我脱离残暴之徒。

他们图谋害我。

5傲慢人在我的路上暗设网罗,

布下圈套,挖了陷阱。(细拉)

6耶和华啊,

我说:“你是我的上帝。”

耶和华啊,求你垂听我的呼求。

7主耶和华,我大能的拯救者啊,

在战争的日子,你保护我。

8耶和华啊,

求你不要让恶人的愿望实现,

不要让他们的阴谋得逞,

免得他们狂妄自大。(细拉)

9愿那些围攻我的人自食恶果。

10愿火炭落在他们身上,

愿他们被丢进火里,

被抛进深坑,不得翻身。

11愿毁谤者在地上无法立足,

愿祸患毁灭残暴之徒。

12我知道耶和华必为贫穷人伸张正义,

为困苦者申冤。

13义人必赞美你的名,

正直人必活在你面前。