Zaburi 136
Wimbo Wa Kumshukuru Mungu
1136:1 Za 105:1; 100:5; 145:9; 118:1-4; 106:1; Ezr 3:11; Hes 2:26; 1:7; 2Nya 5:13; Yer 33:11Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema.
Fadhili zake zadumu milele.
2136:2 Za 105:1; Kum 10:17; Kut 18:11Mshukuruni Mungu wa miungu.
Fadhili zake zadumu milele.
3136:3 Za 105:1; Kum 10:17; 1Tim 6:15Mshukuruni Bwana wa mabwana:
Fadhili zake zadumu milele.
4136:4 Kut 3:20; Ay 9:10Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu,
Fadhili zake zadumu milele.
5136:5 Mit 3:19; Yer 51:15; Mwa 1:1Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu,
Fadhili zake zadumu milele.
6136:6 Mwa 1:1; 1:6; Isa 42:5; Yer 10:12; 33:2Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji,
Fadhili zake zadumu milele.
7136:7 Mwa 1:14, 16; Za 74:16; Yak 1:17Ambaye aliumba mianga mikubwa,
Fadhili zake zadumu milele.
8136:8 Mwa 1:16Jua litawale mchana,
Fadhili zake zadumu milele.
9Mwezi na nyota vitawale usiku,
Fadhili zake zadumu milele.
10136:10 Kut 4:23; 12:12Kwake yeye aliyemuua mzaliwa wa kwanza wa Misri,
Fadhili zake zadumu milele.
11136:11 Kut 6:6; 13:3; Za 105:43Na kuwatoa Israeli katikati yao,
Fadhili zake zadumu milele.
12136:12 Kut 3:20; Kum 5:15; 9:29Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa,
Fadhili zake zadumu milele.
13136:13 Za 78:13Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu,
Fadhili zake zadumu milele.
14136:14 Kut 14:22; Za 106:9Na kuwapitisha Israeli katikati yake,
Fadhili zake zadumu milele.
15136:15 Kut 14:27Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu,
Fadhili zake zadumu milele.
16136:16 Kut 13:18; Za 78:52Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa,
Fadhili zake zadumu milele.
17136:17 Hes 21:23-25; Yos 24:8-11; Za 78:55; 135:9-12Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu,
Fadhili zake zadumu milele.
18136:18 Kum 29:7; Yos 12:7-24Naye aliwaua wafalme wenye nguvu,
Fadhili zake zadumu milele.
19136:19 Hes 21:21-25Sihoni mfalme wa Waamori,
Fadhili zake zadumu milele.
20136:20 Hes 21:33-35Ogu mfalme wa Bashani,
Fadhili zake zadumu milele.
21136:21 Kum 1:38; Yos 12:1; 14:1Akatoa nchi yao kuwa urithi,
Fadhili zake zadumu milele.
22136:22 Kum 29:8; Za 78:55; Isa 20:3; 41:8; 42:19; 43:10; 44:1, 21; 45:4; 49:5-7Urithi kwa Israeli mtumishi wake,
Fadhili zake zadumu milele.
23136:23 Za 78:29; 103:14; 115:12Aliyetukumbuka katika unyonge wetu,
Fadhili zake zadumu milele.
24136:24 Yos 10:14; Neh 9:28; Kum 6:19Alituweka huru toka adui zetu,
Fadhili zake zadumu milele.
25136:25 Mwa 1:30; Mit 6:26Ambaye humpa chakula kila kiumbe.
Fadhili zake zadumu milele.
26136:26 Za 105:1; 115:3; Ezr 3:11Mshukuruni Mungu wa mbinguni,
Fadhili zake zadumu milele.