Zaburi 124
Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1124:1 Za 129:1; Mwa 15:1; Hes 14:9; Yos 1:5Kama Bwana asingalikuwa upande wetu;
Israeli na aseme sasa:
2kama Bwana asingalikuwa upande wetu,
wakati watu walipotushambulia,
3124:3 Za 35:25; Mit 1:12; Yer 51:34wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,
wangalitumeza tungali hai,
4124:4 Za 88:17; 18:4mafuriko yangalitugharikisha,
maji mengi yangalitufunika,
5maji yaendayo kasi
yangalituchukua.
6Bwana asifiwe,
yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7124:7 Za 91:3; 25:15Tumeponyoka kama ndege
kutoka mtego wa mwindaji;
mtego umevunjika,
nasi tukaokoka.
8124:8 1Sam 17:45; Mwa 1:1; Za 115:15; 121:2; 134:3; Kut 18:4; Mit 18:10; Isa 50:10Msaada wetu ni katika jina la Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
A Song of degrees of David.
1If it had not been the LORD who was on our side, now may Israel say;
2If it had not been the LORD who was on our side, when men rose up against us:
3Then they had swallowed us up quick, when their wrath was kindled against us:
4Then the waters had overwhelmed us, the stream had gone over our soul:
5Then the proud waters had gone over our soul.
6Blessed be the LORD, who hath not given us as a prey to their teeth.
7Our soul is escaped as a bird out of the snare of the fowlers: the snare is broken, and we are escaped.
8Our help is in the name of the LORD, who made heaven and earth.