Zaburi 116 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 116:1-19

Zaburi 116

Shukrani Kwa Kuokolewa Kutoka Mauti

1116:1 Za 18:1; 31:22; 40:1; 6:9; 28:2Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu;

amesikia kilio changu ili anihurumie.

2116:2 Za 5:1Kwa sababu amenitegea sikio lake,

nitamwita siku zote za maisha yangu.

3116:3 2Sam 22:6; Za 18:4-5Kamba za mauti zilinizunguka,

maumivu makuu ya kuzimu yalinipata,

nikalemewa na taabu na huzuni.

4116:4 Za 80:2, 18; 118:5Ndipo nikaliitia jina la Bwana:

“Ee Bwana, niokoe!”

5116:5 Kut 22:27; 9:27; Ezr 9:15; Za 11:7; 86:15; 2Nya 12:6; Neh 9:8; Yer 12:1; Mao 1:18; Ufu 16:5Bwana ni mwenye neema na haki,

Mungu wetu ni mwingi wa huruma.

6116:6 Za 79:8; 18:3; 22:5; 107:13Bwana huwalinda wanyenyekevu,

nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.

7116:7 Za 13:6; 106:1; 142:7; 46:10; 62:1; 131:2; Mt 11:29; Yer 6:16Ee nafsi yangu, tulia tena,

kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.

8116:8 Za 86:13Kwa kuwa wewe, Ee Bwana,

umeniokoa nafsi yangu na mauti,

macho yangu kutokana na machozi,

miguu yangu kutokana na kujikwaa,

9116:9 Mwa 5:22; Za 56:13; 89:15; 27:13; Ay 28:13; Isa 38:11; Yer 11:9ili niweze kutembea mbele za Bwana,

katika nchi ya walio hai.

10116:10 Za 9:18; 72:2; 107:17; 119:67, 71, 75; 2Kor 4:13Niliamini, kwa hiyo nilisema,

“Mimi nimeteseka sana.”

11116:11 Yer 9:3-5Katika taabu yangu nilisema,

“Wanadamu wote ni waongo.”

12116:12 Za 103:2; 106:1Nimrudishie Bwana nini

kwa wema wake wote alionitendea?

13116:13 Za 105:1Nitakiinua kikombe cha wokovu

na kulitangaza jina la Bwana.

14116:14 Hes 30:2; Za 66:13Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana

mbele za watu wake wote.

15116:15 Za 72:14; Hes 23:10; Ay 5:26; Lk 16:22; Ufu 14:13Kifo cha watakatifu kina thamani

machoni pa Bwana.

16116:16 Za 119:125; 143:12; 86:16; Ay 12:18Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako,

mimi ni mtumishi wako,

mwana wa mjakazi wako;116:16 Au: mwanao mwaminifu.

umeniweka huru

toka katika minyororo yangu.

17116:17 Law 7:12; Ezr 1:4Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru

na kuliita jina la Bwana.

18116:18 Za 116:14; Law 22:18Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana

mbele za watu wake wote,

19116:19 Za 102:21; 92:13; 135:2; 96:8; 100:4katika nyua za nyumba ya Bwana,

katikati yako, ee Yerusalemu.

Msifuni Bwana.

Ketab El Hayat

مزمور 116:1-19

الْمَزْمُورُ الْمِئَةُ وَالسَّادِسَ عَشَرَ

1إِنِّي أُحِبُّ الرَّبَّ لأَنَّهُ يَسْمَعُ ابْتِهَالِي وَيَسْتَجِيبُ إِلَى تَضَرُّعَاتِي. 2أَمَالَ أُذُنَهُ إِلَيَّ لِذَلِكَ أَدْعُوهُ مَادُمْتُ حَيًّا. 3طَوَّقَتْنِي حِبَالُ الْمَوْتِ. أَطْبَقَ عَلَيَّ رُعْبُ الْهَاوِيَةِ. قَاسَيْتُ ضِيقاً وَحُزْناً. 4فَدَعَوْتُ الرَّبَّ: آهِ يَا رَبُّ نَجِّ نَفْسِي! 5الرَّبُّ حَنُونٌ وَبَارٌّ. إِلَهُنَا رَحِيمٌ. 6الرَّبُّ حَافِظُ الْبُسَطَاءِ. تَذَلَّلْتُ فَخَلَّصَنِي. 7عُودِي يَا نَفْسِي إِلَى طُمَأْنِينَتِكِ، لأَنَّ الرَّبَّ قَدْ أَحْسَنَ إِلَيْكِ. 8لأَنَّكَ يَا رَبُّ أَنْقَذْتَ نَفْسِي مِنَ الْمَوْتِ، وَعَيْنِي مِنَ الدَّمْعِ، وَقَدَمَيَّ مِنَ التَّعَثُّرِ، 9لِذَلِكَ أَسْلُكُ بِطَاعَةٍ أَمَامَ الرَّبِّ فِي دِيَارِ الأَحْيَاءِ.

10آمَنْتُ لِذَلِكَ تَكَلَّمْتُ. أَنَا عَانَيْتُ كَثِيراً. 11وَقُلْتُ فِي حَيْرَتِي: «جَمِيعُ الْبَشَرِ كَاذِبُونَ». 12مَاذَا أَرُدُّ لِلرَّبِّ مُقَابِلَ كُلِّ مَا أَبْدَاهُ نَحْوي مِنْ حُسْنِ الصَّنِيعِ؟ 13سَأَتَنَاوَلُ كَأْسَ الْخَلاصِ، وَأَدْعُو بِاسْمِ الرَّبِّ. 14أُوْفِي نُذُورِي لِلرَّبِّ أَمَامَ كُلِّ شَعْبِهِ.

15عَزِيزٌ فِي عَيْنَي الرَّبِّ مَوْتُ قِدِّيسِيهِ. 16آهِ يَا رَبُّ أَنَا عَبْدُكَ. أَنَا عَبْدُكَ وَابْنُ أَمَتِكَ. أَنْتَ حَلَلْتَ قُيُودِي. 17لَكَ أُقَدِّمُ ذَبَائِحَ الشُّكْرِ، وَأَدْعُو بِاسْمِكَ. 18أُوْفِي نُذُورِي لِلرَّبِّ أَمَامَ كُلِّ شَعْبِهِ. 19فِي دِيَارِ بَيْتِ الرَّبِّ، فِي وَسَطِكِ يَا أُورُشَلِيمُ. هَلِّلُويَا.