Zaburi 109 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 109:1-31

Zaburi 109

Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1109:1 Kut 15:2; Yer 17:14; Ay 34:29; Za 83:1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2109:2 Za 43:1; 52:4kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3109:3 Za 69:4; 35:7; 35:7, 10; Yn 15:25; 1Sam 19:4, 5Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4109:4 Za 69:13; 141:5Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5109:5 Mwa 44:4; Za 38:20Wananilipiza mabaya kwa mema,

chuki badala ya urafiki wangu.

6109:6 1Nya 21:1; Ay 1:6; Zek 3:1Agiza mtu mwovu ampinge,

mshtaki109:6 Mshtaki hapa maana yake ni Shetani. asimame mkono wake wa kuume.

7109:7 Za 1:5; Mit 28:9; Zek 3:1Anapohukumiwa, apatikane na hatia,

nayo maombi yake yamhukumu.

8109:8 Ay 15:32; Mdo 1:20Siku zake za kuishi na ziwe chache,

nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.

9109:9 Kut 22:24; Yer 18:21Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10109:10 Mwa 4:12Watoto wake na watangetange wakiomba,

na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.

11109:11 Hes 14:3; Isa 1:7; 6:11; 36:1; Mao 5:2; Neh 5:3; Ay 20:18; 18:9Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.

12109:12 Ay 5:4Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13109:13 Za 21:10; 9:5; 37:28; Hes 14:12; Mit 10:7; Ay 18:19Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14109:14 Kut 20:5Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele za Bwana,

dhambi ya mama yake

isifutwe kamwe.

15109:15 Za 90:8; Kut 17:14; Kum 32:26; Ay 18:17Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana,

ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.

16109:16 Ay 20:19; Za 35:10; 34:18Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17109:17 Mit 28:27; Mt 7:2Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18109:18 Za 10:7; Hes 5:22Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19109:19 Za 109:29; 73:6; Eze 7:27Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20109:20 Kut 32:34; Za 54:5; 94:23; 7:10; Isa 3:11; 2Tim 4:14Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.

21109:21 Kut 9:16; Za 3:7; 23:3; 69:16Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wa pendo lako.

22Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23109:23 Ay 14:2Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24109:24 Ebr 12:12; Ay 16:8; Za 35:13Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25109:25 Za 22:6; Ay 16:4; Mt 27:39; Mk 15:29; Isa 37:22Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.

26109:26 Za 12:1; 119:86Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27109:27 Ay 37:7Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.

28109:28 2Sam 16:12; Za 66:4; Isa 35:10; 51:11; 54:1; 65:14; Hes 22:12Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29109:29 Za 35:26Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.

30109:30 Za 35:18Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana,

katika umati mkubwa nitamsifu.

31109:31 Za 16:8; 108:6Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Забур 109:1-7

Песнь 109Песнь 109 Эта песнь является пророчеством об Исо Масехе (см. Мат. 22:41-46; Деян. 2:34-36; Евр. 5:5-10). Многие толкователи считают, что эта песнь изначально использовалась во время коронации исроильских царей.

Песнь Довуда.

1Вечный сказал моему Повелителю:

«Сядь по правую руку от Меня,

пока Я не повергну всех врагов Твоих

к ногам Твоим».

2Вечный распространит Твою власть за пределы Сиона.

Правь над врагами Твоими!

3В тот день Твой народ добровольно

пойдёт за Тобой на битву,

облачённый в святые одеяния.

Твоя сила будет обновляться

каждый день, как утренняя роса.

4Поклялся Вечный

и не откажется:

«Ты – священнослужитель навеки,

подобный Малик-Цедеку»109:4 См. Нач. 14:17-20..

5Владыка по правую руку от Тебя;

Он сразит царей в день Своего гнева.

6Будет судить народы, покроет поле боя их трупами,

сокрушит головы по всей земле.

7Он будет на пути пить из водного потока

и победоносно поднимет голову.