Zaburi 106 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 106:1-48

Zaburi 106

Wema Wa Bwana Kwa Watu Wake

1106:1 Ezr 3:11; Za 63:7; 22:23; 103:2; 119:68; 136:1-26; Yer 33:11; Mt 19:17Msifuni Bwana.

Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

2106:2 Za 40:5; 71:16Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana

au kutangaza kikamilifu sifa zake?

3106:3 Yer 22:15, 16; Mt 22:37; Za 15:2; 112:5; Hos 12:6Heri wale wanaodumisha haki,

ambao daima wanafanya yaliyo mema.

4106:4 Za 25:6-7; 77:7; Mwa 50:24Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako,

uwe msaada wangu unapowaokoa,

5106:5 Kum 30:15; Za 1:3; 105:6; 20:5; 27:5; 47:5; 118:15; Kut 34:9ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako,

niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako,

na kuungana na urithi wako katika kukusifu.

6106:6 1Fal 8:47; Neh 1:7; Dan 9:5; Rum 3:9; 2Nya 30:7; Law 26:40Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda,

tumekosa na tumetenda uovu.

7106:7 Amu 3:7; Za 78:42; Kut 14:11, 12Wakati baba zetu walipokuwa Misri,

hawakuzingatia maajabu yako,

wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako,

bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.

8106:8 Kut 9:16; 14:30-31; Za 80:3; 107:13; 23:3; 143:11; Isa 25:9; Yoe 2:32; Yos 7:9; Yer 14:7, 21Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake,

ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.

9106:9 Nah 1:4; Isa 50:3; 63:11-14; Kut 14:21; Za 18:15; 78:13Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka,

akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.

10106:10 Kut 14:30; Za 107:13; 78:42, 53; Isa 35:9; 62:12Aliwaokoa mikononi mwa adui;

kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.

11106:11 Kut 14:28Maji yaliwafunika adui zao,

hakunusurika hata mmoja.

12106:12 Kut 15:1-21; Za 105:43Ndipo walipoamini ahadi zake,

nao wakaimba sifa zake.

13106:13 Kut 15:24; 16:28; Hes 27:21Lakini mara walisahau aliyowatendea,

wala hawakungojea shauri lake.

14106:14 1Kor 10:9; Kut 17:2; Za 78:40; 68:7Jangwani walitawaliwa na tamaa zao,

walimjaribu Mungu nyikani.

15106:15 Isa 10:16; Hes 11:33; Kut 16:13; Za 78:29Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba,

lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.

16106:16 Hes 16:1-3Kambini walimwonea wivu Mose,

na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.

17106:17 Kum 11:6; 15:12; Hes 16:1Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani,

ikawazika Abiramu na kundi lake.

18106:18 Law 10:2Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao,

mwali wa moto uliwateketeza waovu.

19106:19 Kut 32:4; Mdo 7:41Huko Horebu walitengeneza ndama,

na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.

20106:20 Yer 2:11; Rum 1:23Waliubadilisha Utukufu wao

kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.

21106:21 Za 78:11; 75:1; Kum 10:21Walimsahau Mungu aliyewaokoa,

aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,

22106:22 Za 78:51; Kut 3:20; Kum 4:34miujiza katika nchi ya Hamu

na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.

23106:23 Kut 32:10-14; Hes 11:2; Eze 13:5; 20:13; Kum 9:19Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza:

kama Mose mteule wake,

asingesimama kati yao na Mungu

kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.

24106:24 Ebr 3:18; Yer 3:19; Hes 14:11, 30, 31; Kum 8:7Kisha waliidharau ile nchi nzuri,

hawakuiamini ahadi yake.

25106:25 Kut 15:24; Kum 1:27; 1Kor 10:10Walinungʼunika ndani ya mahema yao,

wala hawakumtii Bwana.

26106:26 Hes 14:23; Ebr 4:3; 3:17; Kum 2:14Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa

kwamba atawafanya waanguke jangwani,

27106:27 Law 26:33kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa,

na kuwatawanya katika nchi zote.

28106:28 Hes 23:28; 25:2, 3; Kum 4:3; Hos 9:10; Ufu 2:14Walijifunga nira na Baali wa Peori,

wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.

29106:29 Za 64:2; 141:4; Hes 16:46; 25:3, 8Waliichochea hasira ya Bwana,

wakamkasirisha kwa matendo yao maovu,

nayo tauni ikazuka katikati yao.

30106:30 Kut 6:25; Hes 25:8Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati,

nayo tauni ikazuiliwa.

31106:31 Mwa 15:6; Za 49:11; Hes 15:11-13Hili likahesabiwa kwake haki,

kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.

32106:32 Kum 1:37; Kut 17:7; Hes 20:2-13Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana,

janga likampata Mose kwa sababu yao;

33106:33 Kut 17:4-7; 23:21; Yak 3:2; Isa 63:10; Za 107:11; 51:11; Hes 20:8-12kwa maana walimwasi Roho wa Mungu,

na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.

34106:34 Amu 1:21, 27-36; 2:2; Yos 9:15; Kum 2:34; 7:2, 16; 20:10; Kut 23:24Hawakuyaangamiza yale mataifa

kama Bwana alivyowaagiza,

35106:35 Amu 3:5, 6; Ezr 9:1, 2bali walijichanganya na mataifa

na wakazikubali desturi zao.

36106:36 Kut 10:7; 23:33; Amu 2:12; 2Fal 17:8-11; 2Nya 33:2-7; Kum 7:10, 16Waliabudu sanamu zao,

zikawa mtego kwao.

37106:37 Isa 57:5; Kut 10:7; 22:20; Law 18:21; Kum 32:17; 12:31; 7:16; 1Kor 10:20; Eze 16:20-21Wakawatoa wana wao

na binti zao dhabihu kwa mashetani.

38106:38 2Fal 3:27; Hes 35:33; Law 18:21; Kum 18:10Walimwaga damu isiyo na hatia,

damu za wana wao na binti zao,

ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani,

nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.

39106:39 Mwa 3:17; Law 18:24; Eze 20:18; Hes 15:39Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda;

kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.

40106:40 Law 26:28; Kut 34:9; 9:29Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake

na akauchukia sana urithi wake.

41106:41 Amu 2:14; Neh 9:27Akawakabidhi kwa mataifa

na adui zao wakawatawala.

42106:42 Amu 4:3Adui zao wakawaonea

na kuwatia chini ya mamlaka yao.

43106:43 Amu 7:1-25; 2:16-19; 6:1-7; Yos 10:14; Neh 9:28Mara nyingi aliwaokoa

lakini walikuwa wamezama kwenye uasi,

nao wakajiharibu katika dhambi zao.

44106:44 Amu 3:9; 10:10Lakini akaangalia mateso yao

wakati aliposikia kilio chao;

45106:45 Mwa 9:15; Lk 1:72; Za 105:8; 103:11; 17:7; Law 26:41; Mao 3:32; Kut 32:14kwa ajili yao akakumbuka agano lake,

na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.

46106:46 1Nya 16:8; Mt 19:17; 2Nya 5:13; 7:3Akawafanya wahurumiwe

na wote waliowashikilia mateka.

47106:47 Za 147:2; 105:1; 30:4; 99:3; 28:9; 107:3; Isa 11:12; 27:13; 56:8; 66:20; Yer 31:8; Lk 1:74; Eze 20:34; Mik 4:6; 2Kor 5:15Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe.

Tukusanye tena kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.

48106:48 Za 41:13; 72:19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Watu wote na waseme, “Amen!”

Msifuni Bwana.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 106:1-48

第 106 篇

上帝恩待祂的子民

(平行经文:历代志上16:34-36

1你们要赞美耶和华!

要称谢耶和华,

因为祂是美善的,

祂的慈爱永远长存!

2谁能述说耶和华的大能作为?

谁能道尽祂当受赞美之处?

3那些行事公正,

持守公义的人有福了。

4耶和华啊!

你恩待你子民的时候,

求你别忘了我;

你拯救他们的时候,

求你帮助我,

5使我看到你所拣选的人繁荣昌盛,

与他们同乐,

与你的子民一同夸耀。

6我们跟祖先一样也犯了罪,

行事邪恶。

7我们祖先在埃及漠视你行的神迹,

忘记你向他们屡施慈爱,

海边反叛你。

8但祂为了自己的名拯救了他们,

以彰显祂的大能。

9祂斥责海,海就干了,

祂带领他们走过深渊,

如履干地。

10祂救他们逃脱敌人的追赶,

从仇敌的手中救赎了他们。

11海水淹没了敌军,

没有一人生还。

12那时他们才相信祂的话,

歌唱赞美祂。

13然而,他们很快忘了祂的作为,

不愿等候祂的引导。

14他们在旷野大起贪念,

试探上帝。

15祂满足了他们的要求,

但在他们当中降下了瘟疫。

16他们还在营中嫉妒摩西和耶和华拣选为祭司的亚伦

17于是大地裂开,

吞没了大坍亚比兰和他们的家人。

18火在他们的党羽中烧起,

消灭了这些恶人。

19他们在何烈山铸造牛犊,祭拜偶像,

20他们把荣耀的上帝变成了吃草之牛的铸像。

21他们忘记了拯救他们的上帝,

祂曾在埃及行奇事,

22地行神迹,

海边行可畏的事。

23因此祂说要消灭他们。

若不是祂所拣选的摩西为他们求情,

祂早已在烈怒中毁灭了他们。

24他们藐视那佳美之地,

不相信祂的应许。

25他们在帐篷里发怨言,

不听从祂的命令。

26因此,祂举手起誓要使他们倒毙在旷野,

27使他们的后代分散到各族各方去。

28他们在毗珥祭拜巴力

吃献给假神的祭物。

29他们的所作所为触怒耶和华,

以致瘟疫降在他们中间,

30直到非尼哈起来惩罚罪人,

瘟疫才停止。

31这就是他的义行,世代永存。

32他们在米利巴泉边惹耶和华发怒,

连累了摩西

33因为他们惹摩西发怒,

以致他说了鲁莽的话。

34他们没有照耶和华的命令消灭外族人,

35反倒与他们混居,

仿效他们的习俗,

36拜他们的神像,陷入网罗。

37他们把自己的儿女当祭物献给鬼魔,

38他们把自己的儿女献给迦南的神像作祭物,

流他们儿女无辜的血,

玷污了那地方。

39他们的行为玷污了自己,

使自己沦为淫妇。

40耶和华因此向祂的子民发怒,

厌恶他们,

41使他们落在列邦的手中,

受敌人的辖制。

42他们的敌人压迫他们,

奴役他们。

43祂多次拯救他们,

他们却执意背叛,

陷入罪中不能自拔。

44但祂听见他们在苦难中呼求时,

仍然眷顾他们。

45祂没有忘记与他们立的约,

因祂伟大无比的爱而怜悯他们。

46祂使掳掠他们的人怜悯他们。

47我们的上帝耶和华啊,

求你拯救我们,

从各国招聚我们,

使我们可以称谢你的圣名,

欢然赞美你。

48以色列的上帝耶和华永永远远当受称颂。

愿万民都说:“阿们!”

你们要赞美耶和华!