Zaburi 104 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 104:1-35

Zaburi 104

Kumsifu Muumba

1104:1 Za 103:22; Ay 40:10Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.

Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana,

umejivika utukufu na enzi.

2104:2 Yer 43:12; 51:15; 1Tim 6:16; Ay 9:8; 37:18; Isa 44:24; 49:18, 22; 42:5; 40:22; Zek 12:1; Za 18:12; 19:4Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi,

amezitandaza mbingu kama hema

3104:3 Amo 9:6; Za 18:10; 24:2; Kum 33:26; Isa 19:1; Nah 1:3; 2Fal 12:11na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji.

Huyafanya mawingu kuwa gari lake,

na hupanda kwenye mbawa za upepo.

4104:4 Za 148:8; Mwa 3:24; 2Fal 2:11; Ebr 1:7Huzifanya pepo kuwa wajumbe104:4 Au: malaika. wake,

miali ya moto watumishi wake.

5104:5 Kut 31:17; Ay 26:7; Za 24:1, 2; 121:2; 102:25; 1Sam 2:8Ameiweka dunia kwenye misingi yake,

haiwezi kamwe kuondoshwa.

6104:6 Mwa 7:19; 1:2; 2Pet 3:6Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi,

maji yalisimama juu ya milima.

7104:7 Za 18:15; 29:3; Kut 9:23Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia,

kwa sauti ya radi yako yakatoroka,

8104:8 Za 33:7; Ay 38:10yakapanda milima, yakateremka mabondeni,

hadi mahali pale ulipoyakusudia.

9104:9 Yer 5:22; Za 16:6; 33:7; Ay 26:10; Mwa 1:9; 9:11Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka,

kamwe hayataifunika dunia tena.

10104:10 Za 107:33; Isa 41:16Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni,

hutiririka kati ya milima.

11104:11 Za 104:13; Mwa 16:12; Isa 32:14; Yer 14:6Huwapa maji wanyama wote wa kondeni,

punda-mwitu huzima kiu yao.

12104:12 Za 104:17; Mt 8:20; 13:32Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji,

huimba katikati ya matawi.

13104:13 Za 135:7; 147:8; Yer 10:13Huinyeshea milima kutoka orofa zake,

dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.

14104:14 Ay 38:27; 28:5; Mwa 1:30; Za 147:8; 136:25Huyafanya majani ya mifugo yaote,

na mimea kwa watu kulima,

wajipatie chakula kutoka ardhini:

15104:15 Mwa 14:18; Amu 9:13; Za 23:5; 92:10; Lk 7:46; Kum 8:3; Mit 31:6, 7; Yer 12:12; Mk 14:23; Mhu 10:19; Yn 2:9, 10divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu,

mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake,

na mkate wa kutia mwili nguvu.

16104:16 Mwa 1:11; Za 29:5; 72:16; Hes 24:6Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri,

mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.

17104:17 Za 104:12Humo ndege hufanya viota vyao,

korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.

18104:18 Mit 30:26; Kum 14:5Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu,

majabali ni kimbilio la pelele.

19104:19 Mwa 1:14; Za 19:6; Ay 38:12Mwezi hugawanya majira,

na jua hutambua wakati wake wa kutua.

20104:20 Isa 45:7; Amo 5:8; Za 74:16; 50:10Unaleta giza, kunakuwa usiku,

wanyama wote wa mwituni huzurura.

21104:21 Amo 3:4; Za 145:15; Mt 6:26; Yoe 1:20Simba hunguruma kwa mawindo yao,

na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.

22104:22 Za 37:8Jua huchomoza, nao huondoka,

hurudi na kulala katika mapango yao.

23104:23 Mwa 3:19; Amu 19:16Kisha mwanadamu huenda kazini mwake,

katika kazi yake mpaka jioni.

24104:24 Mwa 1:31; 1:20-22; Za 40:5; 24:1; 50:10, 11Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi!

Kwa hekima ulizifanya zote,

dunia imejaa viumbe vyako.

25104:25 Za 69:34; Eze 47:10Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele,

imejaa viumbe visivyo na idadi,

vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.

26104:26 Za 107:23; Eze 27:9; Yon 1:3; Ay 41:1; 40:20; Mwa 1:21Huko meli huenda na kurudi,

pia Lewiathani,104:26 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. uliyemuumba acheze ndani yake.

27104:27 Ay 36:31; Za 147:9; 145:15; Rum 11:36Hawa wote wanakutazamia wewe,

uwape chakula chao kwa wakati wake.

28104:28 Isa 58:11; Za 103:5; 145:16Wakati unapowapa,

wanakikusanya,

unapofumbua mkono wako,

wao wanashibishwa mema.

29104:29 Kum 31:17; Ay 7:21; Mhu 12:7Unapoficha uso wako,

wanapata hofu,

unapoondoa pumzi yao,

wanakufa na kurudi mavumbini.

30104:30 Mwa 1:2; Isa 32:15Unapopeleka Roho wako,

wanaumbwa,

nawe huufanya upya uso wa dunia.

31104:31 Kut 40:35; Rum 11:36; Mwa 1:4; Za 8:1Utukufu wa Bwana na udumu milele,

Bwana na azifurahie kazi zake:

32104:32 Kut 19:18; Hab 3:10; Za 97:4; 144:5yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka,

aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.

33104:33 Kut 15:1; Za 108:1Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote;

nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.

34104:34 Za 2:11; 9:2; 32:11Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye,

ninapofurahi katika Bwana.

35104:35 Ay 7:10; Za 28:6; 37:38; 105:45; 106:48Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia

na waovu wasiwepo tena.

Ee nafsi yangu, msifu Bwana.

Msifuni Bwana.104:35 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 104:1-35

第 104 篇

称颂创造主——上帝

1我的心啊,要称颂耶和华。

我的上帝耶和华啊,

你是多么伟大!

你以尊贵和威严为衣,

2你身披光华如披外袍,

你铺展穹苍如铺幔子。

3你在水中设立自己楼阁的栋梁。

你以云彩为车驾,乘风飞驰。

4风是你的使者,

火焰是你的仆役。

5你奠立大地的根基,

使它永不动摇。

6你以深水为衣覆盖大地,

淹没群山。

7你一声怒叱,众水便奔逃;

你一声雷鸣,众水就奔流,

8漫过山峦,流进山谷,

归到你指定的地方。

9你为众水划定不可逾越的界线,

以免大地再遭淹没。

10耶和华使泉水涌流在谷地,

奔腾在山间,

11让野地的动物有水喝,

野驴可以解渴。

12飞鸟也在溪旁栖息,

在树梢上歌唱。

13祂从天上的楼阁降雨在山间,

大地因祂的作为而丰美富饶。

14祂使绿草如茵,滋养牲畜,

让人种植作物,

享受大地的出产,

15有沁人心怀的醇酒、

滋润容颜的膏油、

增强活力的五谷。

16耶和华种植了黎巴嫩的香柏树,

使它们得到充沛的水源,

17鸟儿在树上筑巢,

鹳鸟在松树上栖息。

18高山是野山羊的住处,

峭壁是石獾的藏身之所。

19你命月亮定节令,

使太阳自知西沉。

20你造黑暗,定为夜晚,

作林中百兽出没的时间。

21壮狮吼叫着觅食,

寻找上帝所赐的食物。

22太阳升起,

百兽便退回自己的洞窟中休息,

23人们外出工作,直到黄昏。

24耶和华啊,你的创造多么繁多!

你用智慧造了这一切,

大地充满了你创造的万物。

25汪洋浩瀚,

充满了无数的大小水族,

26船只往来于海上,

你造的鲸鱼也在水中嬉戏。

27它们都倚靠你按时供应食物。

28它们从你那里得到供应,

你伸手赐下美食,

使它们饱足。

29你若对它们弃而不顾,

它们会惊慌失措。

你一收回它们的气息,

它们便死亡,归于尘土。

30你一吹气便创造了它们,

你使大地更新。

31愿耶和华的荣耀存到永远!

愿耶和华因自己的创造而欢欣!

32祂一看大地,大地就震动;

祂一摸群山,群山就冒烟。

33我要一生一世向耶和华歌唱,

我一息尚存就要赞美上帝。

34愿祂喜悦我的默想,

祂是我喜乐的泉源。

35愿罪人从地上消逝,

愿恶人荡然无存。

我的心啊,要称颂耶和华!

你们要赞美耶和华!