Zaburi 102
Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana.
1102:1 Za 4:1; Kut 2:23Ee Bwana, usikie maombi yangu,
kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2102:2 Za 22:24; 31:2; 88:2; 2Fal 19:16Usinifiche uso wako
ninapokuwa katika shida.
Unitegee sikio lako,
ninapoita, unijibu kwa upesi.
3Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,
mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4102:4 Za 37:2; 90:5-6; 1Sam 1:7; Ezr 10:6; Ay 33:26Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,
ninasahau kula chakula changu.
5102:5 Za 6:6Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,
nimebakia ngozi na mifupa.
6102:6 Isa 34:11; Sef 2:14; Kum 14:15-17; Ay 30:29Nimekuwa kama bundi wa jangwani,
kama bundi kwenye magofu.
7102:7 Za 77:4; 38:11Nilalapo sipati usingizi,
nimekuwa kama ndege mpweke
kwenye paa la nyumba.
8102:8 Za 31:11; 42:10; Mdo 23:12Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki,
wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
9102:9 Isa 44:20; Za 6:6; 42:3; 80:5Ninakula majivu kama chakula changu
na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10102:10 Za 7:11; 38:3; 30:7kwa sababu ya ghadhabu yako kuu,
kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
11102:11 1Nya 29:15; Ay 14:2; 8:12; Za 39:6; Yak 1:10Siku zangu ni kama kivuli cha jioni,
ninanyauka kama jani.
12102:12 Kut 15:18; 3:15; Isa 55:13; 63:12; 40:2; Za 135:13Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele,
sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13102:13 Za 119:126; 44:26; 77:7; Kum 32:36; 1Fal 3:26; Isa 54:8; 60:10; 40:2; Zek 10:6; Kut 13:10; Dan 8:19; Mdo 1:7Utainuka na kuihurumia Sayuni,
kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema;
wakati uliokubalika umewadia.
14102:14 Dan 9:2Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako,
vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15102:15 1Fal 8:43; Isa 2:2; Za 67:7; 76:12; 138:4; 148:11Mataifa wataogopa jina la Bwana,
wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16102:16 Za 51:18; 8:1; Isa 60:1, 2Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni
na kutokea katika utukufu wake.
17102:17 Neh 2:8; 1Fal 8:29; Za 4:1; 6:9Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,
wala hatadharau hoja yao.
18102:18 Rum 4:24; 15:4; Za 22:31; 1Kor 10:1; Isa 43:21Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho,
ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19102:19 Kum 26:15; Za 14:2; 53:2“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu,
kutoka mbinguni alitazama dunia,
20102:20 Za 68:6; Lk 4:19kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa
na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21102:21 Za 22:22; 9:14Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni
na sifa zake katika Yerusalemu,
22102:22 Hos 1:11; Za 22:27; Isa 49:22, 23; Zek 8:20-23wakati mataifa na falme zitakapokusanyika
ili kumwabudu Bwana.
23102:23 Za 39:5Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu,
akafupisha siku zangu.
24102:24 Mwa 21:33; Ay 36:26; Za 90:2; Hab 1:12; Ufu 1:4, 8Ndipo niliposema:
“Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu;
miaka yako inaendelea vizazi vyote.
25102:25 Mwa 1:1; Ebr 1:10; 2Nya 2:12; Za 8:3; Kut 20:11; Ay 38:4-7Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia,
nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26102:26 Rum 8:20; Isa 51:6; 13:10, 13; 66:21; 34:4; Mt 24:35; Yoe 2:10; Eze 32:8; 2Pet 3:7-10; Ufu 20:11Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu,
zote zitachakaa kama vazi.
Utazibadilisha kama nguo
nazo zitaondoshwa.
27102:27 Hes 23:19; Ebr 13:8; Mal 3:6; Yak 1:17; Za 9:7Lakini wewe, U yeye yule,
nayo miaka yako haikomi kamwe.
28102:28 Za 69:36; 25:13; 89:4Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako;
wazao wao wataimarishwa mbele zako.”
Salmo 102
Oração de um aflito que, quase desfalecido, derrama o seu lamento diante do Senhor.
1Ouve a minha oração, Senhor!
Chegue a ti o meu grito de socorro!
2Não escondas de mim o teu rosto
quando estou atribulado.
Inclina para mim os teus ouvidos;
quando eu clamar, responde-me depressa!
3Esvaem-se os meus dias como fumaça;
meus ossos queimam como brasas vivas.
4Como a relva ressequida está o meu coração;
esqueço até de comer!
5De tanto gemer
estou reduzido a pele e osso.
6Sou como a coruja do deserto102.6 Ou pelicano,
como uma coruja entre as ruínas.
7Não consigo dormir;
pareço um pássaro solitário no telhado.
8Os meus inimigos zombam de mim o tempo todo;
os que me insultam usam o meu nome para lançar maldições.
9Cinzas são a minha comida,
e com lágrimas misturo o que bebo,
10por causa da tua indignação e da tua ira,
pois me rejeitaste e me expulsaste para longe de ti.
11Meus dias são como sombras crescentes;
sou como a relva que vai murchando.
12Tu, porém, Senhor, no trono reinarás para sempre;
o teu nome será lembrado de geração em geração.
13Tu te levantarás e terás misericórdia de Sião,
pois é hora de lhe mostrares compaixão;
o tempo certo é chegado.
14Pois as suas pedras são amadas pelos teus servos,
as suas ruínas os enchem de compaixão.
15Então as nações temerão o nome do Senhor
e todos os reis da terra a sua glória.
16Porque o Senhor reconstruirá Sião
e se manifestará na glória que ele tem.
17Responderá à oração dos desamparados;
as suas súplicas não desprezará.
18Escreva-se isto para as futuras gerações,
e um povo que ainda será criado
louvará o Senhor, proclamando:
19“Do seu santuário nas alturas o Senhor olhou;
dos céus observou a terra,
20para ouvir os gemidos dos prisioneiros
e libertar os condenados à morte”.
21Assim o nome do Senhor será anunciado em Sião
e o seu louvor em Jerusalém,
22quando os povos e os reinos
se reunirem para adorar o Senhor.
23No meio da minha vida ele me abateu com sua força;
abreviou os meus dias.
24Então pedi:
“Ó meu Deus, não me leves no meio dos meus dias.
Os teus dias duram por todas as gerações!”
25No princípio firmaste os fundamentos da terra,
e os céus são obras das tuas mãos.
26Eles perecerão, mas tu permanecerás;
envelhecerão como vestimentas.
Como roupas tu os trocarás
e serão jogados fora.
27Mas tu permaneces o mesmo,
e os teus dias jamais terão fim.
28Os filhos dos teus servos terão uma habitação;
os seus descendentes serão estabelecidos na tua presença.