Zaburi 102
Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana.
1102:1 Za 4:1; Kut 2:23Ee Bwana, usikie maombi yangu,
kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2102:2 Za 22:24; 31:2; 88:2; 2Fal 19:16Usinifiche uso wako
ninapokuwa katika shida.
Unitegee sikio lako,
ninapoita, unijibu kwa upesi.
3Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,
mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4102:4 Za 37:2; 90:5-6; 1Sam 1:7; Ezr 10:6; Ay 33:26Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,
ninasahau kula chakula changu.
5102:5 Za 6:6Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,
nimebakia ngozi na mifupa.
6102:6 Isa 34:11; Sef 2:14; Kum 14:15-17; Ay 30:29Nimekuwa kama bundi wa jangwani,
kama bundi kwenye magofu.
7102:7 Za 77:4; 38:11Nilalapo sipati usingizi,
nimekuwa kama ndege mpweke
kwenye paa la nyumba.
8102:8 Za 31:11; 42:10; Mdo 23:12Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki,
wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
9102:9 Isa 44:20; Za 6:6; 42:3; 80:5Ninakula majivu kama chakula changu
na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10102:10 Za 7:11; 38:3; 30:7kwa sababu ya ghadhabu yako kuu,
kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
11102:11 1Nya 29:15; Ay 14:2; 8:12; Za 39:6; Yak 1:10Siku zangu ni kama kivuli cha jioni,
ninanyauka kama jani.
12102:12 Kut 15:18; 3:15; Isa 55:13; 63:12; 40:2; Za 135:13Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele,
sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13102:13 Za 119:126; 44:26; 77:7; Kum 32:36; 1Fal 3:26; Isa 54:8; 60:10; 40:2; Zek 10:6; Kut 13:10; Dan 8:19; Mdo 1:7Utainuka na kuihurumia Sayuni,
kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema;
wakati uliokubalika umewadia.
14102:14 Dan 9:2Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako,
vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15102:15 1Fal 8:43; Isa 2:2; Za 67:7; 76:12; 138:4; 148:11Mataifa wataogopa jina la Bwana,
wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16102:16 Za 51:18; 8:1; Isa 60:1, 2Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni
na kutokea katika utukufu wake.
17102:17 Neh 2:8; 1Fal 8:29; Za 4:1; 6:9Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,
wala hatadharau hoja yao.
18102:18 Rum 4:24; 15:4; Za 22:31; 1Kor 10:1; Isa 43:21Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho,
ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19102:19 Kum 26:15; Za 14:2; 53:2“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu,
kutoka mbinguni alitazama dunia,
20102:20 Za 68:6; Lk 4:19kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa
na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21102:21 Za 22:22; 9:14Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni
na sifa zake katika Yerusalemu,
22102:22 Hos 1:11; Za 22:27; Isa 49:22, 23; Zek 8:20-23wakati mataifa na falme zitakapokusanyika
ili kumwabudu Bwana.
23102:23 Za 39:5Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu,
akafupisha siku zangu.
24102:24 Mwa 21:33; Ay 36:26; Za 90:2; Hab 1:12; Ufu 1:4, 8Ndipo niliposema:
“Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu;
miaka yako inaendelea vizazi vyote.
25102:25 Mwa 1:1; Ebr 1:10; 2Nya 2:12; Za 8:3; Kut 20:11; Ay 38:4-7Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia,
nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26102:26 Rum 8:20; Isa 51:6; 13:10, 13; 66:21; 34:4; Mt 24:35; Yoe 2:10; Eze 32:8; 2Pet 3:7-10; Ufu 20:11Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu,
zote zitachakaa kama vazi.
Utazibadilisha kama nguo
nazo zitaondoshwa.
27102:27 Hes 23:19; Ebr 13:8; Mal 3:6; Yak 1:17; Za 9:7Lakini wewe, U yeye yule,
nayo miaka yako haikomi kamwe.
28102:28 Za 69:36; 25:13; 89:4Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako;
wazao wao wataimarishwa mbele zako.”
Psalm 102In Hebrew texts 102:1-28 is numbered 102:2-29.
A prayer of an afflicted person who has grown weak and pours out a lament before the Lord.
1Hear my prayer, Lord;
let my cry for help come to you.
2Do not hide your face from me
when I am in distress.
Turn your ear to me;
when I call, answer me quickly.
3For my days vanish like smoke;
my bones burn like glowing embers.
4My heart is blighted and withered like grass;
I forget to eat my food.
5In my distress I groan aloud
and am reduced to skin and bones.
6I am like a desert owl,
like an owl among the ruins.
7I lie awake; I have become
like a bird alone on a roof.
8All day long my enemies taunt me;
those who rail against me use my name as a curse.
9For I eat ashes as my food
and mingle my drink with tears
10because of your great wrath,
for you have taken me up and thrown me aside.
11My days are like the evening shadow;
I wither away like grass.
12But you, Lord, sit enthroned forever;
your renown endures through all generations.
13You will arise and have compassion on Zion,
for it is time to show favor to her;
the appointed time has come.
14For her stones are dear to your servants;
her very dust moves them to pity.
15The nations will fear the name of the Lord,
all the kings of the earth will revere your glory.
16For the Lord will rebuild Zion
and appear in his glory.
17He will respond to the prayer of the destitute;
he will not despise their plea.
18Let this be written for a future generation,
that a people not yet created may praise the Lord:
19“The Lord looked down from his sanctuary on high,
from heaven he viewed the earth,
20to hear the groans of the prisoners
and release those condemned to death.”
21So the name of the Lord will be declared in Zion
and his praise in Jerusalem
22when the peoples and the kingdoms
assemble to worship the Lord.
23In the course of my life102:23 Or By his power he broke my strength;
he cut short my days.
24So I said:
“Do not take me away, my God, in the midst of my days;
your years go on through all generations.
25In the beginning you laid the foundations of the earth,
and the heavens are the work of your hands.
26They will perish, but you remain;
they will all wear out like a garment.
Like clothing you will change them
and they will be discarded.
27But you remain the same,
and your years will never end.
28The children of your servants will live in your presence;
their descendants will be established before you.”