Zaburi 102 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 102:1-28

Zaburi 102

Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu

Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana.

1102:1 Za 4:1; Kut 2:23Ee Bwana, usikie maombi yangu,

kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.

2102:2 Za 22:24; 31:2; 88:2; 2Fal 19:16Usinifiche uso wako

ninapokuwa katika shida.

Unitegee sikio lako,

ninapoita, unijibu kwa upesi.

3Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,

mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.

4102:4 Za 37:2; 90:5-6; 1Sam 1:7; Ezr 10:6; Ay 33:26Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,

ninasahau kula chakula changu.

5102:5 Za 6:6Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,

nimebakia ngozi na mifupa.

6102:6 Isa 34:11; Sef 2:14; Kum 14:15-17; Ay 30:29Nimekuwa kama bundi wa jangwani,

kama bundi kwenye magofu.

7102:7 Za 77:4; 38:11Nilalapo sipati usingizi,

nimekuwa kama ndege mpweke

kwenye paa la nyumba.

8102:8 Za 31:11; 42:10; Mdo 23:12Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki,

wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.

9102:9 Isa 44:20; Za 6:6; 42:3; 80:5Ninakula majivu kama chakula changu

na nimechanganya kinywaji changu na machozi

10102:10 Za 7:11; 38:3; 30:7kwa sababu ya ghadhabu yako kuu,

kwa maana umeniinua na kunitupa kando.

11102:11 1Nya 29:15; Ay 14:2; 8:12; Za 39:6; Yak 1:10Siku zangu ni kama kivuli cha jioni,

ninanyauka kama jani.

12102:12 Kut 15:18; 3:15; Isa 55:13; 63:12; 40:2; Za 135:13Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele,

sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.

13102:13 Za 119:126; 44:26; 77:7; Kum 32:36; 1Fal 3:26; Isa 54:8; 60:10; 40:2; Zek 10:6; Kut 13:10; Dan 8:19; Mdo 1:7Utainuka na kuihurumia Sayuni,

kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema;

wakati uliokubalika umewadia.

14102:14 Dan 9:2Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako,

vumbi lake lenyewe hulionea huruma.

15102:15 1Fal 8:43; Isa 2:2; Za 67:7; 76:12; 138:4; 148:11Mataifa wataogopa jina la Bwana,

wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.

16102:16 Za 51:18; 8:1; Isa 60:1, 2Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni

na kutokea katika utukufu wake.

17102:17 Neh 2:8; 1Fal 8:29; Za 4:1; 6:9Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,

wala hatadharau hoja yao.

18102:18 Rum 4:24; 15:4; Za 22:31; 1Kor 10:1; Isa 43:21Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho,

ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:

19102:19 Kum 26:15; Za 14:2; 53:2Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu,

kutoka mbinguni alitazama dunia,

20102:20 Za 68:6; Lk 4:19kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa

na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”

21102:21 Za 22:22; 9:14Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni

na sifa zake katika Yerusalemu,

22102:22 Hos 1:11; Za 22:27; Isa 49:22, 23; Zek 8:20-23wakati mataifa na falme zitakapokusanyika

ili kumwabudu Bwana.

23102:23 Za 39:5Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu,

akafupisha siku zangu.

24102:24 Mwa 21:33; Ay 36:26; Za 90:2; Hab 1:12; Ufu 1:4, 8Ndipo niliposema:

“Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu;

miaka yako inaendelea vizazi vyote.

25102:25 Mwa 1:1; Ebr 1:10; 2Nya 2:12; Za 8:3; Kut 20:11; Ay 38:4-7Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia,

nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.

26102:26 Rum 8:20; Isa 51:6; 13:10, 13; 66:21; 34:4; Mt 24:35; Yoe 2:10; Eze 32:8; 2Pet 3:7-10; Ufu 20:11Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu,

zote zitachakaa kama vazi.

Utazibadilisha kama nguo

nazo zitaondoshwa.

27102:27 Hes 23:19; Ebr 13:8; Mal 3:6; Yak 1:17; Za 9:7Lakini wewe, U yeye yule,

nayo miaka yako haikomi kamwe.

28102:28 Za 69:36; 25:13; 89:4Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako;

wazao wao wataimarishwa mbele zako.”

Hoffnung für Alle

Psalm 102:1-29

Herr, erbarme dich über Jerusalem!

1Gebet eines Menschen, der allen Mut verloren hat und dem Herrn sein Leid klagt.

2Höre mein Gebet, Herr,

und achte auf meinen Hilfeschrei!

3Ich bin in großer Not – verbirg dich nicht vor mir!

Höre mir zu und hilf mir schnell!

4Mein Leben verflüchtigt sich wie Rauch,

mein ganzer Körper glüht, von Fieber geschüttelt.

5Meine Kraft vertrocknet wie abgemähtes Gras,

selbst der Hunger ist mir vergangen.

6Ich bin nur noch Haut und Knochen,

mir bleibt nichts als endloses Stöhnen.

7Man hört mich klagen wie eine Eule in der Wüste,

wie ein Käuzchen in verlassenen Ruinen.

8Tiefe Verzweiflung raubt mir den Schlaf;

ich fühle mich wie ein einsamer Vogel auf dem Dach.

9Tag für Tag beschimpfen mich meine Feinde,

und wen sie verfluchen wollen,

dem wünschen sie mein Schicksal herbei.

10Ich esse Staub, als wäre es Brot,

und in meine Getränke mischen sich Tränen.

11Denn dein furchtbarer Zorn hat mich getroffen,

du hast mich hochgeworfen und zu Boden geschmettert!

12Mein Leben gleicht einem Schatten,

der am Abend in der Dunkelheit verschwindet.

Ich bin wie Gras, das bald verdorrt.

13Du aber, Herr, regierst für alle Zeiten;

von dir wird man erzählen, solange es Menschen gibt.

14Du wirst eingreifen und dich über Zion erbarmen.

Denn die Zeit ist gekommen, es zu begnadigen – die Stunde ist da!

15Dein Volk liebt die Mauern dieser Stadt

und trauert über ihre Trümmer.

16-17Aber der Herr wird sie wieder aufbauen,

er wird erscheinen in all seiner Pracht.

Dann werden die Völker ihn fürchten

und alle Könige vor seiner Macht zittern.

18Ja, der Herr wird das Gebet der Hilflosen hören,

er lässt ihr Flehen nicht außer Acht.

19Diese Worte soll man aufschreiben

für die Generationen, die nach uns kommen,

damit auch sie es lesen und den Herrn loben:

20Der Herr blickte von seinem Heiligtum herab,

er schaute vom Himmel auf die Erde.

21Er hörte das Stöhnen der Gefangenen

und rettete sie vor dem sicheren Tod.

22Darum wird man den Herrn auf dem Berg Zion rühmen;

in ganz Jerusalem wird man ihn loben,

23wenn alle Völker und Königreiche sich versammeln,

um sich in seinen Dienst zu stellen.

24Mitten im Leben102,24 Wörtlich: Auf dem Weg. hat Gott meine Kraft gebrochen,

ich weiß, meine Tage sind schon gezählt.

25Darum flehe ich ihn an:

Mein Gott, lass mich nicht jetzt schon sterben!

Du selbst überdauerst die Generationen.

26Vor langer Zeit hast du alles geschaffen,

Himmel und Erde sind das Werk deiner Hände.

27Sie werden vergehen, du aber bleibst.

Wie alte Kleider werden sie zerfallen,

wie ein abgetragenes Gewand legst du sie ab und wechselst sie aus.

28Du aber bleibst ein und derselbe,

deine Jahre haben kein Ende.

29Die Nachkommen deines Volkes werden in Sicherheit wohnen,

unter deinem Schutz werden sie geborgen sein.