Yoshua 9 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 9:1-27

Udanganyifu Wa Wagibeoni

19:1 Hes 13:17; 34:6; Kum 3:25; Mwa 13:7; Yos 3:10; 11:19; Kut 3:17Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu,9:1 Yaani Bahari ya Mediterania. hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi), 29:2 2Nya 20:1; Mit 11:11; Isa 8:9-12; Yoe 3:9-12; Mdo 4:26-289:2 1Nya 8:29; 14:16; 16:19; 21:29; 2Nya 1:2; Neh 3:7; Isa 28:21; Yer 28:1; 41:12; Mwa 12:8; Yos 8:1wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.

39:3 Yos 10:10; 11:19; 18:25; 21:17; 2Sam 2:21; 5:25; 20:8; 1Fal 3:4Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai, 4nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa. 5Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga. 69:6 Kum 11:30; Mwa 26:28; Yos 5:10Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”

79:7 Kut 23:32; 1Fal 5:12; Yos 11:19; Kum 7:2Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”

89:8 Kum 20:11; 2Fal 10:5Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.”

Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”

99:9 Kum 20:15; Hes 23:22; Yos 2:9; Ay 32:19; Mt 9:17; Lk 5:37-38; Amu 2:2Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri, 109:10 Hes 21:24-25; 21:33-35; Yos 2:10pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi. 11Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.” ’ 12Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu. 13Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”

149:14 Kut 16:28; Hes 27:21; 1Sam 22:10; 2Sam 5:19; Isa 30:1-2Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana. 159:15 Yos 10:1, 4; 11:19; 2Sam 21:2; 24:1; Amu 1:21; Za 106:34; Kut 23:32Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.

16Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao. 179:17 Yos 18:25; 2Sam 4:2; 23:37; Yos 15:9; 18:14-15; Amu 18:12; 1Sam 6:21; 7:2; Za 132:6; Yer 26:20Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu. 189:18 Amu 21:1, 7, 18; 1Sam 20:17; Za 15:4; Kut 15:24Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli.

Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi, 19lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa. 209:20 Mwa 24:8; Eze 17:13-18; Zek 5:3-4Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.” 219:21 Kum 29:11Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.

22Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi? 239:23 Mwa 9:25Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”

24Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili. 259:25 Mwa 16:6; Yer 26:14; Kut 23:32; Kum 20:15-17; Kut 15:14Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”

26Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa. 279:27 Kut 1:11; Kum 29:11; 12:5; 1Fal 8:29; 2Nya 7:12, 20; Za 78:68Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Josué 9:1-27

Astucia de los gabaonitas

1Había reyes que vivían en el lado occidental del Jordán, en la montaña, en la llanura y a lo largo de la costa del Mediterráneo, hasta el Líbano: hititas, amorreos, cananeos, ferezeos, heveos y jebuseos. Cuando estos monarcas se enteraron de lo sucedido, 2se aliaron bajo un solo mando para hacer frente a Josué y a los israelitas.

3Los gabaonitas, al darse cuenta de cómo Josué había tratado a las ciudades de Jericó y de Hai, 4maquinaron un plan. Enviaron unos mensajeros, cuyos asnos llevaban costales viejos y odres para el vino, rotos y remendados. 5Iban vestidos con ropa vieja y tenían sandalias gastadas y remendadas. El pan que llevaban para comer estaba duro y hecho migas. 6Fueron al campamento de Guilgal, donde estaba Josué, y les dijeron a él y a los israelitas:

―Venimos de un país muy lejano. Queremos hacer un trato con vosotros.

7Los israelitas replicaron:

―Tal vez sois de por aquí y, en ese caso, no podemos hacer ningún trato con vosotros.

8Ellos le dijeron a Josué:

―Nosotros estamos dispuestos a serviros.

Y Josué les preguntó:

―¿Quiénes sois vosotros y de dónde venís?

9Ellos respondieron:

―Nosotros somos tus siervos, y hemos venido de un país muy distante, hasta donde ha llegado la fama del Señor tu Dios. Nos hemos enterado de todo lo que él hizo en Egipto 10y de lo que les hizo a los dos reyes amorreos al este del Jordán: Sijón, rey de Hesbón, y Og, rey de Basán, el que residía en Astarot. 11Por eso los habitantes de nuestro país, junto con nuestros dirigentes, nos pidieron que nos preparáramos para el largo viaje y que os diéramos el siguiente mensaje: “Deseamos ser vuestros siervos; hagamos un trato”. 12Cuando salimos para acá, nuestro pan estaba fresco y caliente, pero ahora, ¡miradlo! Está duro y hecho migas. 13Estos odres estaban nuevecitos y repletos de vino, y ahora, tal como podéis ver, están todos rotos. Y nuestra ropa y sandalias están gastadas por el largo viaje.

14Los hombres de Israel participaron de las provisiones de los gabaonitas, pero no consultaron al Señor. 15Entonces Josué hizo con ellos un trato de ayuda mutua y se comprometió a perdonarles la vida. Y los jefes israelitas ratificaron el trato.

16Tres días después de haber concluido el trato con los gabaonitas, los israelitas se enteraron de que eran sus vecinos y vivían en las cercanías. 17Por eso se pusieron en marcha, y al tercer día llegaron a sus ciudades: Gabaón, Cafira, Berot y Quiriat Yearín. 18Pero los israelitas no los atacaron porque los jefes de la comunidad les habían jurado en nombre del Señor, Dios de Israel, perdonarles la vida. Y, aunque toda la comunidad se quejó contra sus jefes, 19estos contestaron:

―Hemos hecho un juramento en nombre del Señor, y no podemos hacerles ningún daño. 20Esto es lo que haremos con ellos: les perdonaremos la vida, para que no caiga sobre nosotros el castigo divino por quebrantar el juramento que hicimos.

21Luego añadieron:

―Se les permitirá vivir, pero a cambio de ser los leñadores y aguadores de la comunidad.

De ese modo, los jefes de la comunidad cumplieron su promesa.

22Entonces Josué llamó a los gabaonitas y les recriminó:

―¿Por qué nos engañasteis con el cuento de que erais de tierras lejanas, cuando en verdad sois nuestros vecinos? 23A partir de ahora, esta será vuestra maldición: seréis por siempre sirvientes del templo de mi Dios, responsables de cortar la leña y de acarrear el agua.

24Los gabaonitas contestaron:

―Nosotros, tus siervos, fuimos bien informados de que el Señor tu Dios ordenó a su siervo Moisés que os diera toda esta tierra y que destruyera a todos sus habitantes. Temimos tanto por nuestra vida que decidimos hacer lo que ya sabéis. 25Estamos en vuestras manos. Haced con nosotros lo que os parezca justo y bueno.

26Así salvó Josué a los gabaonitas de morir a manos del pueblo de Israel. 27Ese mismo día Josué los hizo leñadores y aguadores de la asamblea israelita, especialmente del altar del Señor que está en el lugar que él mismo eligió. Y así han permanecido hasta el día de hoy.