Yoshua 8 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 8:1-35

Mji Wa Ai Waangamizwa

18:1 Mwa 26:24; Kum 31:6; Hes 14:9; Kum 1:21; Yos 10:7; 7:2; 9:3; 10:1; 12:9; 6:2Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake. 28:2 Mwa 49:27; Kum 20:14; Amu 9:43; 20:29; Yos 6:21Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”

3Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku 48:4 Amu 20:29; 2Nya 13:13akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho. 58:5 Amu 20:35Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia. 6Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia, 78:7 Amu 7:7; 1Sam 23:4ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu. 88:8 Amu 20:29-38; 2Sam 13:28; Yos 1:16Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”

98:9 2Nya 13:13Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.

108:10 Mwa 22:3; Yos 7:6; 6:12; Za 101:8; 119:60; Mhu 9:10; Yer 21:12Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai. 11Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji. 128:12 Mwa 12:8; 28:19Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji. 13Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.

148:14 Kum 1:1; Amu 20:34; Mt 24:39; 1The 5:1-3; 2Pet 2:3Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji. 158:15 Amu 20:36; Yos 15:61; 18:12Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani. 168:16 Amu 20:31; Kut 14:3-4; Za 9:16Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji. 17Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.

188:18 Ay 41:26; Za 35:3; Kut 4:2; 17:9-12; 14:16; Kum 7:23-24; 9:3; Yos 1:5; Yer 49:3Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai. 198:19 Amu 20:33Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.

208:20 Amu 20:40Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao. 21Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia. 228:22 Kum 7:2; Yos 10:1; Law 27:29; Ay 20:5; Lk 17:26-30Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka. 238:23 1Sam 15:8Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.

24Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini. 258:25 Kum 20:16-18Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai. 268:26 Hes 21:2; 17:12Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai. 278:27 Hes 31:22, 26; Mt 20:15Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.

288:28 Hes 31:10; Yos 7:2; Yer 49:3; Kum 13:16; Yos 10:1; Mwa 35:20; 2Fal 19:25; Isa 17:1; 25:2; Yer 9:11Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo. 298:29 Kum 21:23; Yn 19:31; 2Sam 18:17; Yos 10:26, 27; Za 107:40; 110:5; Yos 7:26; 10:27Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.

Agano Linafanywa Upya Katika Mlima Ebali

308:30 Kum 11:29; Kut 20:24; Mwa 8:20; 12:7-8Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali, 318:31 Kut 20:24-25; Kum 27:6-7kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.8:31 Sadaka za ushirika. 328:32 Kum 27:8Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika. 338:33 Law 16:29; Kum 31:12; 11:29; Yn 4:20; 1Nya 15:11-13; Law 24:22; Hes 15:16Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.

348:34 Kum 28:61; 31:11; Neh 8:3; Kum 29:20-21Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria. 358:35 Kut 12:38; Kum 31:12; Yos 1:8Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.

New International Reader’s Version

Joshua 8:1-35

Israel Destroys Ai

1Then the Lord said to Joshua, “Do not be afraid. Do not lose hope. Go up and attack Ai. Take the whole army with you. I have handed the king of Ai over to you. I have given you his people, his city and his land. 2Remember what you did to Jericho and its king. You will do the same thing to Ai and its king. But this time you can keep for yourselves the livestock and everything else you take from them. Have some of your fighting men hide behind the city and take them by surprise.”

3So Joshua and the whole army moved out to attack Ai. He chose 30,000 of his best fighting men. He sent them out at night. 4He gave them orders. He said, “Listen carefully to what I’m saying. You must hide behind the city. Don’t go very far away from it. All of you must be ready to attack it. 5I and all those with me will march up to the city. The men of Ai will come out to fight against us, just as they did before. Then we’ll run away from them. 6They’ll chase us until we’ve drawn them away from the city. They’ll say, ‘They are running away from us, just as they did before.’ When we run away from them, 7come out of your hiding place. Capture the city. The Lord your God will hand it over to you. 8When you have taken it, set it on fire. Do what the Lord has commanded. Make sure you obey my orders.”

9Then Joshua sent them away. They went to the place where they had planned to hide. They hid in a place west of Ai. It was between Bethel and Ai. But Joshua spent that night with his troops.

10Early the next morning Joshua brought together his army. He and the leaders of Israel marched in front of them to Ai. 11The whole army that was with him marched up to the city. They stopped in front of it. They set up camp north of Ai. There was a valley between them and the city. 12Joshua had chosen about 5,000 soldiers. He had ordered them to hide in a place west of Ai. It was between Bethel and Ai. 13The men took up their battle positions. All the men in the camp north of the city took up their positions. So did those who were supposed to hide west of the city. That night Joshua went into the valley.

14The king of Ai saw what the troops with Joshua were doing. So the king and all his men hurried out of the city early in the morning. They marched out to meet Israel in battle. They went to a place that looked out over the Arabah Valley. The king didn’t know that some of Israel’s fighting men were hiding behind the city. 15Joshua and all his men let the men of Ai drive them back. The Israelites ran away toward the desert. 16All the men of Ai were called out to chase them. They chased Joshua. So they were drawn away from the city. 17Not even one man remained in Ai or Bethel. All of them went out to chase Israel. When they did, they left the city wide open.

18Then the Lord said to Joshua, “Hold out toward Ai the javelin that is in your hand. I will give the city to you.” So Joshua held out toward the city the javelin in his hand. 19As soon as he did, the men hiding behind the city got up quickly. They came out of their hiding places and rushed forward. They entered the city and captured it. They quickly set it on fire.

20The men of Ai looked back. They saw smoke rising up from the city into the sky. But they couldn’t escape in any direction. The Israelites had been running away toward the desert. But now they turned around to face those chasing them. 21Joshua and all his men saw that the men who had been hiding behind the city had captured it. They also saw that smoke was going up from it. So they turned around and attacked the men of Ai. 22The men who had set Ai on fire came out of the city. They also fought against the men of Ai. So the men of Ai were caught in the middle. The army of Israel was on both sides of them. Israel struck them down. They didn’t let anyone remain alive or get away. 23But they captured the king of Ai alive. They brought him to Joshua.

24Israel finished killing all the men of Ai. They destroyed them in the fields and in the desert where they had chased them. They struck down every one of them with their swords. Then all the Israelites returned to Ai. And they killed those who were left in it. 25The total number of men and women they killed that day was 12,000. The Israelites put to death all the people of Ai. 26Joshua continued to hold out his javelin toward Ai. He didn’t lower his hand until he and his men had totally destroyed everyone who lived there. 27But this time Israel kept for themselves the livestock and everything else they had taken from the city. The Lord had directed Joshua to let them do it.

28So Joshua burned down Ai. He tore it down so it could never be built again. It has been deserted to this very day. 29Joshua killed the king of Ai. He stuck a pole through the body. Then he set it up where people could see it. He left it there until evening. At sunset, Joshua ordered his men to remove the body from the pole. He told them to throw the body down at the entrance of the city gate. They put a large pile of rocks over the body. That pile is still there to this day.

Joshua Reads the Book of the Law to the People

30Joshua built an altar to honor the Lord, the God of Israel. He built it on Mount Ebal. 31Moses, the servant of the Lord, had commanded the Israelites to do that. Joshua built the altar according to what is written in the Book of the Law of Moses. Joshua built the altar out of stones that iron tools had never touched. Then the people offered on the altar burnt offerings to the Lord. They also sacrificed friendship offerings on it. 32Joshua copied the law of Moses on stones. He did it while all the Israelites were watching. 33They were standing on both sides of the ark of the covenant of the Lord. All the Israelites, including outsiders and citizens, were there. Israel’s elders, officials and judges were also there. All of them faced the priests, who were Levites. They were carrying the ark. Half of the people stood in front of Mount Gerizim. The other half stood in front of Mount Ebal. Moses, the servant of the Lord, had earlier told them to do it. Moses told them to do it when he had given directions to bless the Israelites.

34Then Joshua read all the words of the law out loud. He read the blessings and the curses. He read them just as they are written in the Book of the Law. 35Joshua read every word Moses had commanded. He read them to the whole community of Israel. That included the women and children. It also included the outsiders living among them.