Yoshua 6 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 6:1-27

Yeriko Yatekwa Na Kuangamizwa

16:1 Yos 24:11Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.

26:2 Kum 7:24; Yos 8:1; Amu 11:21; 2Sam 5:19; Neh 9:24; Dan 5:18-19Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita. 3Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita. 46:4 Kut 19:13; Law 25:9; Hes 10:8; Amu 7:16Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo. 56:5 Kut 19:13; 1Sam 6:15; Ezr 3:11; 10:12; Za 42:4; 95:1; Isa 8:9; 42:13Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”

6Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.” 76:7 Kut 14:15; Hes 10:35; 1Sam 4:3; 7:1Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”

86:8 Yos 4:13Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata. 96:9 Hes 2:31; Isa 52:12, 13; Hes 10:25; Isa 42:11-13Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa. 106:10 1Sam 4:5; Ezr 3:11Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!” 11Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.

126:12 Kum 31:25Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana. 136:13 1Nya 15:26; Gal 6:9Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia. 14Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.

156:15 1Fal 18:44; 2Fal 4:35; 5:14Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba. 166:16 Amu 7:20; 2Nya 14:14Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu! 176:17 Law 27:28; Kum 20:17; Isa 13:5; 24:1; 34:2-5; Mal 4:6; Yos 2:14; Mwa 13:3; 1Sam 15:6; Mt 10:41; 25:40; Ebr 6:10; 11:31; Yak 2:25Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma. 186:18 Yos 7:1, 12, 25, 26; 1Nya 2:7; Kum 7:26; 13:17; Isa 52:11; Rum 12:9; 2Kor 6:17; Efe 5:11; 1The 5:2; 1Fal 18:17, 18Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu. 196:19 Hes 31:22Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”

206:20 Law 25:9; Amu 6:34; 7:22; 1Fal 1:41; Isa 18:3; Yer 4:21; 42:14; Amo 2:2; Ebr 11:30Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji. 216:21 Kum 20:16; 1Sam 15:3, 8; 1Fal 20:42; Yer 48:18; Ufu 18:21Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.

226:22 Mwa 42:9; Yos 2:4; Hes 21:32; Yos 2:14; Ebr 11:30-31Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.” 236:23 Yos 2:13Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.

246:24 Hes 31:10; Kum 13:16Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana. 256:25 Amu 1:25; Yos 2:1; 2:1, 6; Ebr 11:31Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.

266:26 1Sam 14:24; Hes 5:21; 1Fal 16:34Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko:

“Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume

ataiweka misingi yake;

kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho

atayaweka malango yake.”

276:27 Mwa 39:2; Hes 14:43; Yos 9:1; 1Nya 14:17; Amu 1:9; 2Sam 7:9; Rum 8:31; 1Sam 2:30Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.

New International Reader’s Version

Joshua 6:1-27

1The gates of Jericho were shut tight and guarded closely because of the Israelites. No one went out. No one came in.

2Then the Lord said to Joshua, “I have handed Jericho over to you. I have also handed over to you its king and its fighting men. 3March around the city once with all your fighting men. In fact, do it for six days. 4Have seven priests get trumpets made out of rams’ horns. They must carry them in front of the ark. On the seventh day, march around the city seven times. Tell the priests to blow the trumpets as you march. 5You will hear them blow a long blast on the trumpets. When you do, tell the whole army to give a loud shout. The wall of the city will fall down. Then the whole army will march up to the city. Everyone will go straight in.”

6So Joshua, the son of Nun, called for the priests. He said to them, “Go and get the ark of the covenant of the Lord. I want seven of you to carry trumpets in front of it.” 7He gave an order to the army. He said, “Move out! March around the city. Some of the fighting men must march in front of the ark of the Lord.”

8When Joshua had spoken to the men, the seven priests went forward. They were carrying the seven trumpets as they marched in front of the ark of the Lord. They were blowing the trumpets. The ark of the Lord’s covenant was carried behind the priests. 9Some of the fighting men marched ahead of the priests who were blowing the trumpets. The others followed behind the ark and guarded all the priests. That whole time the priests were blowing the trumpets. 10But Joshua had given an order to the army. He had said, “Don’t give a war cry. Don’t raise your voices. Don’t say a word until the day I tell you to shout. Then shout!” 11So he had the ark of the Lord carried around the city once. Then the army returned to camp. They spent the night there.

12Joshua got up early the next morning. The priests went and got the ark of the Lord. 13The seven priests carrying the seven trumpets started out. They marched in front of the ark of the Lord. They blew the trumpets. Some of the fighting men marched ahead of them. The others followed behind the ark and guarded all of them. The priests kept blowing the trumpets. 14On the second day they marched around the city once. Then the army returned to camp. They did all those things for six days.

15On the seventh day, they got up at sunrise. They marched around the city, just as they had done before. But on that day they went around it seven times. 16On the seventh time around, the priests blew a long blast on the trumpets. Then Joshua gave a command to the army. He said, “Shout! The Lord has given you the city! 17The city and everything in it must be set apart to the Lord to be destroyed. But the prostitute Rahab and all those with her in her house must be spared. That’s because she hid the spies we sent. 18But keep away from the things that have been set apart to the Lord. If you take any of them, you will be destroyed. And you will bring trouble on the camp of Israel. You will cause it to be destroyed. 19All the silver and gold is holy. It is set apart to the Lord. So are all the things made out of bronze and iron. All those things must be added to the treasures kept in the Lord’s house.”

20The priests blew the trumpets. As soon as the army heard the sound, they gave a loud shout. Then the wall fell down. Everyone charged straight in. So they took the city. 21They set it apart to the Lord to be destroyed. They destroyed every living thing in it with their swords. They killed men and women. They wiped out young people and old people. They destroyed cattle, sheep and donkeys.

22Then Joshua spoke to the two men who had gone in to check out the land. He said, “Go into the prostitute’s house. Bring her out. Also bring out everyone with her. That’s what you promised her you would do.” 23So the young men who had checked out the land went into Rahab’s house. They brought her out along with her parents and brothers and sisters. They brought out everyone else there with her. They put them in a place outside the camp of Israel.

24Then they burned the whole city and everything in it. But they added the silver and gold to the treasures kept in the Lord’s house. They also put there the things made out of bronze and iron. 25But Joshua spared the prostitute Rahab. He spared her family. He also spared everyone else in the house with her. He did it because she hid the spies he had sent to Jericho. Rahab lives among the Israelites to this day.

26At that time Joshua made a promise and called down a curse. He said, “May the person who tries to rebuild this city of Jericho be under the Lord’s curse.

“If that person lays its foundations,

it will cost the life of his oldest son.

If he sets up its gates,

it will cost the life of his youngest son.”

27So the Lord was with Joshua. And Joshua became famous everywhere in the land.