Yoshua 4 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 4:1-24

Ukumbusho Wa Kuvuka Mto Yordani

14:1 Kum 27:2; Yos 2:17Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua, 24:2 Yos 3:17; Hes 13:1; 34:18; Yos 1:4-15; 1Fal 18:31“Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja, 3nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”

44:4 Yos 3:12Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila, 54:5 Yos 3:17naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli, 64:6 Yos 2:12; Kut 10:2; 12:26; 13:14; Kum 6:20; Za 78:3-6; Isa 38:16kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’ 74:7 Yos 3:13; Kut 28:12; 12:14waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”

84:8 Kut 28:21; Yos 3:17Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini. 94:9 Mwa 28:18; Yos 24:26; 1Sam 7:12; Mwa 35:20Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.

10Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka, 11na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama. 124:12 Mwa 29:32; 30:11; 41:51; Hes 32:27-29Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru. 134:13 Kut 13:18; Hes 32:17Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.

144:14 Yos 3:7; 1Sam 2:30; 2Nya 32:23; 1Nya 29:12Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.

15Basi Bwana akamwambia Yoshua, 164:16 Kut 25:22; Ufu 11:19; Yos 3:15“Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”

17Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”

184:18 Kut 14:27; Yos 3:15Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.

194:19 Kum 11:30; Yos 5:9; 15:17; 1Sam 11:14-15; Amo 4:4; 5:5; Mik 6:5Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko. 20Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani. 21Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’ 224:22 Kut 14:22; Yos 3:17Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’ 234:23 Kut 14:19-22; Neh 9:11; Za 77:16-19; Isa 43:16; 63:12Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka. 244:24 1Fal 8:60; 18:36; 2Fal 5:15; Za 67:2; 83:18; 106:8; Isa 37:20; 52:10; Kut 15:16; 1Nya 29:12; Za 44:3; 89:13; 98:1; 118:15-16; Kut 14:31Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”

Bibelen på hverdagsdansk

Josvabogen 4:1-24

1Efter at folket var kommet godt over på den anden side, sagde Herren til Josva:

2-3„Sig til de 12 mænd, der blev udpeget af Israels 12 stammer, at de hver skal tage en sten fra det sted i flodlejet, hvor præsterne står, og tage stenene med sig til det sted, hvor I slår lejr i aften.”

4Så kaldte Josva de 12 mænd sammen 5og sagde til dem: „Nu kan I gå over, men stands midt ude i flodlejet, hvor pagtens ark er. Der skal hver af jer samle en sten op og bære den på skulderen over på den anden side, så der er en sten for hver af Israels 12 stammer. 6De sten skal være et minde, og når jeres børn i fremtiden spørger: ‚Hvad betyder de mindesten?’ 7skal I svare: ‚De minder os om dengang, Jordanflodens vand standsede for at lade Herrens Ark og folket passere.’ De sten skal altid minde Israels folk om det under, som skete, da vi krydsede Jordanfloden.”

8Mændene gjorde, som Josva havde sagt. De samlede 12 sten op fra flodlejet, én sten for hver stamme, sådan som Herren havde befalet Josva, og tog dem med sig til det sted, hvor de slog lejr for natten. 9Josva anbragte desuden 12 sten midt i floden på det sted, hvor præsterne stod med pagtens ark, og de sten er der den dag i dag. 10De præster, som bar arken, blev altså stående ude i flodlejet, indtil alt, hvad Herren havde befalet Josva, var udført. På den måde førte Josva folket over floden, sådan som Moses havde givet instrukser om. Folket skyndte sig over floden, mens præsterne stod i midten, 11og da de alle var kommet over, fulgte præsterne efter med arken, mens folket stod og så til.

12Som Moses havde befalet, gik de våbenføre mænd fra Rubens, Gads og Manasses halve stamme også med over floden. 13De udgjorde 40.000 bevæbnede krigere, som var klar til at kæmpe for Herren på Jerikos sletter. 14Herren gjorde det sådan, at Josva den dag vandt stor respekt i folkets øjne. Fremover viste de ham samme ærefrygt, som de havde vist Moses. 15-18Efter at Josva på Herrens befaling havde sagt til de præster, der stod med pagtens ark, at de skulle komme op af flodlejet, steg de op på bredden, og i samme øjeblik de satte foden på landjorden, strømmede vandet tilbage, og floden gik over sine bredder som før.

19Det var den tiende dag i årets første måned,4,19 Den første måned i Israels religiøse kalender kaldtes også aviv og senere nisan, jf. 2.Mos. 12 og 13,4. Det svarer til marts-april. at folket krydsede Jordanfloden og slog lejr ved Gilgal øst for Jeriko. 20Det var også der, Josva anbragte de 12 mindesten, de havde taget med fra midten af floden. 21Så gentog han over for hele Israels folk, hvad han allerede tidligere havde sagt: „I fremtiden, når jeres børn spørger: ‚Hvad betyder de mindesten?’ 22skal I sige: ‚De er til minde om, at Israels folk gik tørskoet over Jordanfloden.’ 23Fortæl dem, hvordan Herren holdt vandet tilbage for øjnene af jer, indtil alle var kommet over, ligesom han gjorde med Det Røde Hav, dengang Israels folk skulle krydse det. 24For alle jordens folk skal det være et tegn på Herrens vældige magt, og det skal hjælpe jer til altid at have respekt og ærefrygt for Herren, jeres Gud.”