Yoshua 3 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 3:1-17

Kuvuka Yordani

13:1 Yos 2:1; Mwa 13:10; Ay 40:23; Hes 25:1; 33:49Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka. 23:2 Mwa 40:13; Yos 2:16; Kum 1:16; Yos 1:11Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote, 33:3 Hes 10:33; 4:15; Kum 31:9; 1Fal 8:3; 1Sam 6:15wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata. 43:4 Hes 35:5; Kut 19:12; Kum 28:58; 1Nya 16:30; Za 2:11; 96:9; Ebr 12:28Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,0003:4 Dhiraa 2,000 ni sawa na mita 900. kati yenu na Sanduku.”

53:5 Kut 20:1; Law 11:44; Amu 6:13; 1Nya 16:9, 24; Za 26:7; 75:1; Kut 10:10; Hes 11:18; Yos 7:13; 1Sam 16:5; Yos 2:16Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”

63:6 Hes 4:15Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.

73:7 Yos 4:14; 1Nya 29:25; Yos 1:5Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose. 8Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’ ”

9Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu. 103:10 Kum 5:26; 1Sam 17:26, 36; 2Fal 19:4, 16; Za 18:46; 42:2; Isa 37:4, 17; Yer 10:10; 23:36; Dan 6:26; Hos 1:10; Mt 16:16; Kum 7:21; Mwa 26:24; Yos 17:15; 24:11; Amu 1:4; 3:5; Kut 3:8; 23:23; Kum 7:1; 9:1; 11:3; Amu 19:11; 1Nya 11:4Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi. 113:11 Kut 19:5; Kum 14:10; Ay 9:10; 28:24; 41:11; Za 50:12; 97:5; Zek 6:5; Kum 9:3Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia. 123:12 Yos 4:2-4Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila. 133:13 Yos 4:7; Kut 14:22; Isa 11:15; Za 78:13Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”

143:14 Za 132:8; Mdo 7:44-45; Kut 25:10; 26:30; Hes 10:3; 2Nya 6:41; Ebr 9:4Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia. 153:15 2Fal 3:6; Yos 4:18; 1Nya 12:15; Isa 8:7; Mwa 8:22; Yer 12:5; 49:19Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji, 163:16 Za 66:6; 74:15; 114:3; Ay 38:37; Za 33:7; 1Fal 4:12; 7:46; Mwa 14:3; 8:1; Kut 14:22; 2Fal 2:4maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.

173:17 Yos 4:3-9; Kut 14:22; Yos 2:10Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.

New International Version

Joshua 3:1-17

Crossing the Jordan

1Early in the morning Joshua and all the Israelites set out from Shittim and went to the Jordan, where they camped before crossing over. 2After three days the officers went throughout the camp, 3giving orders to the people: “When you see the ark of the covenant of the Lord your God, and the Levitical priests carrying it, you are to move out from your positions and follow it. 4Then you will know which way to go, since you have never been this way before. But keep a distance of about two thousand cubits3:4 That is, about 3,000 feet or about 900 meters between you and the ark; do not go near it.”

5Joshua told the people, “Consecrate yourselves, for tomorrow the Lord will do amazing things among you.”

6Joshua said to the priests, “Take up the ark of the covenant and pass on ahead of the people.” So they took it up and went ahead of them.

7And the Lord said to Joshua, “Today I will begin to exalt you in the eyes of all Israel, so they may know that I am with you as I was with Moses. 8Tell the priests who carry the ark of the covenant: ‘When you reach the edge of the Jordan’s waters, go and stand in the river.’ ”

9Joshua said to the Israelites, “Come here and listen to the words of the Lord your God. 10This is how you will know that the living God is among you and that he will certainly drive out before you the Canaanites, Hittites, Hivites, Perizzites, Girgashites, Amorites and Jebusites. 11See, the ark of the covenant of the Lord of all the earth will go into the Jordan ahead of you. 12Now then, choose twelve men from the tribes of Israel, one from each tribe. 13And as soon as the priests who carry the ark of the Lord—the Lord of all the earth—set foot in the Jordan, its waters flowing downstream will be cut off and stand up in a heap.”

14So when the people broke camp to cross the Jordan, the priests carrying the ark of the covenant went ahead of them. 15Now the Jordan is at flood stage all during harvest. Yet as soon as the priests who carried the ark reached the Jordan and their feet touched the water’s edge, 16the water from upstream stopped flowing. It piled up in a heap a great distance away, at a town called Adam in the vicinity of Zarethan, while the water flowing down to the Sea of the Arabah (that is, the Dead Sea) was completely cut off. So the people crossed over opposite Jericho. 17The priests who carried the ark of the covenant of the Lord stopped in the middle of the Jordan and stood on dry ground, while all Israel passed by until the whole nation had completed the crossing on dry ground.