Yoshua 17 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 17:1-18

Mgawo Wa Nusu Nyingine Ya Manase Upande Wa Magharibi

117:1 Hes 1:34; 1Nya 7:14; Mwa 41:51; 50:23; Yos 12:2, 5Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu. 217:2 Hes 26:30; Amu 6:11, 34; 8:2; 1Nya 7:14-19; Hes 27:1Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.

317:3 Hes 27:1; 26:33Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. 417:4 Hes 27:5-7; Yos 14:1Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana. 517:5 Yos 13:30-31Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani, 6kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.

717:7 Yos 19:24, 31; 21:6, 30; Amu 1:31; 5:17; 6:35; 7:23; Yos 16:6; Mwa 12:6; Yos 21:12; 24:25Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua. 817:8 Yos 12:17; 15:34(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.) 917:9 Yos 16:8Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari. 1017:10 Mwa 30:18; Eze 48:5Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.

1117:11 Amu 1:27; 1Sam 31:10; 2Sam 21:12; 1Fal 4:12; 1Nya 7:29; 2Fal 9:27; Yos 11:2; 1Sam 28:7; Za 83:10; Yos 12:21; 1Fal 9:15; Eze 48:4Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori,17:11 Ndiyo Nafoth-Dori. Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).

1217:12 Yos 15:63; Hes 26:29; 32:39, 41Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo. 1317:13 Amu 1:27-28; Kut 23:29-33; Amu 1:27, 28Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.

Kabila La Yosefu Lakataa

1417:14 Hes 26:28-37; Yos 16:4; Mwa 48:22; 48:19Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”

1517:15 2Sam 18:6; Yos 3:10; Mwa 14:5; Yos 15:8; 18:16; 2Sam 5:18; 23:13; 1Sam 17:5Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”

1617:16 Amu 1:19; 4:3, 13; Yos 15:56; 1Sam 29:1; Amu 6:33; 1Fal 4:12; 18:46Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”

1717:17 Eze 48:5Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu, 1817:18 1Sam 1:1; Kum 20:1; Yos 11:4-6; 13:6; Rum 8:31; Ebr 13:6bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约书亚记 17:1-18

1以下是约瑟的长子玛拿西支派分到的土地:玛拿西的长子、基列的父亲玛吉是个战士,因此分到了基列巴珊两地。 2玛拿西其他的子孙也按宗族分到了土地,他们属于亚比以谢希勒亚斯列示剑希弗示米大宗族。这些男子按宗族都是约瑟的儿子玛拿西的后代。 3玛拿西的玄孙、玛吉的曾孙、基列的孙子、希弗的儿子西罗非哈没有儿子,只有五个女儿,名叫玛拉挪阿曷拉密迦得撒4她们来见祭司以利亚撒的儿子约书亚和各首领,说:“耶和华曾经吩咐摩西在我们亲族中分给我们产业。”约书亚便照耶和华的吩咐,让她们在叔伯中也分到产业。 5除了约旦河东的基列巴珊两地以外,玛拿西人还分到十块土地, 6因为在玛拿西的后代中,女性也分到了产业。玛拿西其他的子孙分到基列地区。

7玛拿西支派分到的产业从亚设开始,到示剑东面的密米他,再向南到隐·他普亚人居住的地方。 8他普亚地属于玛拿西,但在玛拿西边界上的他普亚城属于以法莲的子孙。 9边界继续向南到加拿河,在河南侧玛拿西境内的城邑都归以法莲玛拿西的边界沿着加拿河北侧直到地中海。 10这样,南面归以法莲,北面归玛拿西,西部边界是地中海,北接亚设,东邻以萨迦11以萨迦亚设境内,玛拿西拥有伯·善以伯莲多珥隐·多珥他纳米吉多及其附近的乡村。 12可是,玛拿西人没能把这些城邑的迦南人赶走,因为他们执意不肯离开。 13以色列人国势强盛的时候,就让迦南人服劳役,但始终没有把他们完全赶走。

14约瑟的子孙对约书亚说:“耶和华赐福给我们,使我们人口众多,为什么你只让我们抽一支签,分一份产业呢?” 15约书亚对他们说:“如果你们人口众多,认为以法莲山区窄小,你们可以到比利洗人和利乏音人居住的地方开辟林区。” 16他们答道:“那些地方不够我们住,何况住在伯·善一带和耶斯列平原的迦南人都有铁战车。” 17约书亚约瑟的子孙以法莲人和玛拿西人说:“你们人口众多,势力强大,不应只得一签之地, 18山区也要分给你们,虽然全是森林,但可以开辟土地,使整个地区归你们。虽然迦南人强盛,有铁战车,但你们能够赶走他们。”