Yoshua 14 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 14:1-15

Mgawanyo Wa Nchi Magharibi Mwa Yordani

114:1 Yos 11:23; Za 16:6; 136:21; Kut 6:23; Yos 21:1; Hes 26:53; 34:17-18; Yos 19:51Basi haya ndiyo maeneo Waisraeli waliyopokea kama urithi katika nchi ya Kanaani, ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliwagawia. 214:2 Law 16:8; Hes 34:13; Za 16:5; Mit 16:33; 18:18Urithi wao uligawanywa kwa kura kwa yale makabila tisa na nusu, kama Bwana alivyoamuru Mose. 314:3 Hes 32:33; 34:14; 35:2; Yos 13:14Mose alikuwa amewapa yale makabila mawili na nusu urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi miongoni mwa hao wengine, 414:4 Mwa 41:54; Amu 1:29; Hes 35:2-3; Yos 21:2kwa kuwa wana wa Yosefu walikuwa makabila mawili; Manase na Efraimu. Walawi hawakupata mgawo wa ardhi, bali walipewa miji tu kwa ajili ya kuishi, pamoja na maeneo ya malisho kwa ajili ya makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe wao. 514:5 Hes 34:13; 35:2; Yos 21:2; Eze 45:1-8; 48:8, 22Kwa hiyo Waisraeli wakagawana ile nchi, kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.

Kalebu Anapewa Mji Wa Hebroni

614:6 Kum 11:30; Hes 13:6; 14:30; Kum 33:1; Hes 14:38; Yos 15:17; Kum 1:19Kisha watu wa Yuda wakamwendea Yoshua huko Gilgali, naye Kalebu mwana wa Yefune yule Mkenizi, akamwambia, “Unajua jambo ambalo Bwana alimwambia Mose mtu wa Mungu huko Kadesh-Barnea kukuhusu wewe na mimi. 714:7 Yos 15:6; Hes 13:17; 13:30; 14:6-9Nilikuwa na umri wa miaka arobaini, wakati Mose mtumishi wa Bwana, aliponituma kutoka Kadesh-Barnea kuipeleleza hiyo nchi. Nami nikamletea taarifa kama kulingana na nilivyosadiki moyoni. 814:8 Hes 13:31; 14:24; 32:12; Kum 1:36; Ufu 14:4Lakini ndugu zangu tuliopanda nao waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa hofu. Bali mimi, nilimfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote. 914:9 Kum 11:24; Hes 14:24; Yos 1:3; Hes 13:22Hivyo katika siku ile, Mose akaniapia, ‘Nchi ambayo umeikanyaga kwa miguu yako itakuwa urithi wako na wa watoto wako milele, kwa sababu umemfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.’

1014:10 Hes 11:28; 14:30; Yos 5:6; 13:1; Hes 14:30; Kum 31:2; Za 90:10“Sasa basi, kama vile Bwana alivyoahidi, ameniweka hai kwa miaka arobaini na mitano tangu wakati alipomwambia Mose jambo hili, wakati Waisraeli wakiwa wanazunguka jangwani. Hivyo mimi hapa leo, nina umri wa miaka themanini na mitano! 1114:11 Kum 34:7; Mwa 15:15Bado ninazo nguvu kama siku ile Mose aliponituma. Bado ninazo nguvu za kwenda vitani sasa kama vile nilivyokuwa wakati ule. 1214:12 Hes 14:24-28; 13:33; 1Sam 14:6; 2Nya 14:11, 12; Za 18:32; 44:3; Rum 8:31; Flp 4:13; Yos 15:14; Amu 1:10Basi nipe nchi hii ya vilima, ambayo Bwana aliniahidi siku ile. Wewe mwenyewe ulisikia wakati ule kwamba Waanaki walikuwako huko na miji yao ilikuwa mikubwa na yenye maboma, lakini, kwa msaada wa Bwana, nitawafukuza watoke huko kama vile alivyonena.”

1314:13 Yos 22:6-7; 1Sam 30:14; Mwa 23:19; Yos 10:36; Amu 1:26; 1Nya 6:56Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune, na akampa Hebroni kama urithi wake. 1414:14 Hes 14:24Hivyo Hebroni imekuwa mali ya Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi tangu wakati ule, kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wote. 1514:15 Mwa 23:2; Yos 15:13; 11:23; Amu 3:11; 1Fal 4:24; 5:4; 1Nya 22:9(Hebroni uliitwa Kiriath-Arba hapo mwanzo, kutokana na huyo Arba ambaye alikuwa mtu mkuu kupita wote miongoni mwa Waanaki.)

Kisha nchi ikawa na amani bila vita.

New International Version – UK

Joshua 14:1-15

Division of the land west of the Jordan

1Now these are the areas the Israelites received as an inheritance in the land of Canaan, which Eleazar the priest, Joshua son of Nun and the heads of the tribal clans of Israel allotted to them. 2Their inheritances were assigned by lot to the nine-and-a-half tribes, as the Lord had commanded through Moses. 3Moses had granted the two-and-a-half tribes their inheritance east of the Jordan but had not granted the Levites an inheritance among the rest, 4for Joseph’s descendants had become two tribes – Manasseh and Ephraim. The Levites received no share of the land but only towns to live in, with pasture-lands for their flocks and herds. 5So the Israelites divided the land, just as the Lord had commanded Moses.

Land allotted to Caleb

6Now the people of Judah approached Joshua at Gilgal, and Caleb son of Jephunneh the Kenizzite said to him, ‘You know what the Lord said to Moses the man of God at Kadesh Barnea about you and me. 7I was forty years old when Moses the servant of the Lord sent me from Kadesh Barnea to explore the land. And I brought him back a report according to my convictions, 8but my fellow Israelites who went up with me made the hearts of the people sink. I, however, followed the Lord my God wholeheartedly. 9So on that day Moses swore to me, “The land on which your feet have walked will be your inheritance and that of your children for ever, because you have followed the Lord my God wholeheartedly.”14:9 Deut. 1:36

10‘Now then, just as the Lord promised, he has kept me alive for forty-five years since the time he said this to Moses, while Israel moved about in the wilderness. So here I am today, eighty-five years old! 11I am still as strong today as the day Moses sent me out; I’m just as vigorous to go out to battle now as I was then. 12Now give me this hill country that the Lord promised me that day. You yourself heard then that the Anakites were there and their cities were large and fortified, but, the Lord helping me, I will drive them out just as he said.’

13Then Joshua blessed Caleb son of Jephunneh and gave him Hebron as his inheritance. 14So Hebron has belonged to Caleb son of Jephunneh the Kenizzite ever since, because he followed the Lord, the God of Israel, wholeheartedly. 15(Hebron used to be called Kiriath Arba after Arba, who was the greatest man among the Anakites.)

Then the land had rest from war.