Yoshua 10 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 10:1-43

Jua Linasimama

110:1 Yos 12:10; 15:8, 63; 18:28; Amu 1:7; Yos 8:1; Kum 20:16; Yos 8:22; 9:3, 15Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao. 210:2 Kut 15:14-16; Kum 11:25; 28:10; Za 48:4-6; Mit 1:26, 27; Ebr 10:27, 31; Ufu 6:15-17Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita. 310:3 Mwa 13:18; Yos 12:11; 15:35; 21:29; Neh 11:29; Yos 12:11; 15:39; 2Fal 14:19; 2Nya 11:9; 25:27; 32:9; Neh 11:30; Isa 32:6; 37:8; Yer 34:7; Mik 1:13Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni. 410:4 Yos 9:15Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”

510:5 Hes 13:29; Kum 1:7; Yos 9:2Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.

610:6 Kum 11:30Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”

710:7 Yos 8:1Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita. 810:8 Kum 3:2; Yos 1:9; 2:24; Kum 7:24; 7:24; 11:25; Yos 11:6; 23:9; Amu 4:14Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”

9Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula. 1010:10 Kut 14:24; Kum 7:23; Yos 9:3; 16:3-5; 18:13-14; 21:22; 1Fal 9:17; 1Nya 6:68; 7:24; 2Nya 8:5; 25:13; Yos 15:35; 1Sam 17:1; 2Nya 11:9; Neh 11:30; Yer 34:7; Yos 12:16; 15:41Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda. 1110:11 Kut 9:18; Za 18:12; Isa 28:2; 17; 32:19; Eze 13:11; Amu 5:20Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.

1210:12 Amo 2:9; Yos 19:42; 21:24; Amu 1:35; 12:12; 1Sam 14:31; 1Nya 6:69; 8:13; 2Nya 11:10; 28:18Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema:

“Wewe jua, simama juu ya Gibeoni,

wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”

1310:13 Hab 3:11; 2Sam 1:18; Isa 38:8Hivyo jua likasimama,

nao mwezi ukatulia,

hadi taifa hilo lilipokwisha

kujilipizia kisasi kwa adui wake,

kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari.

Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima. 1410:14 Yos 10:42; Kut 14:14; Za 106:43; 136:24; Isa 63:10; Yer 21:5; Isa 38:8; Kum 1:30; 3:22; 20:4; 33:29; Amu 1:19, 22; 2Nya 20:29; Neh 4:20; Isa 31:4; Zek 12:3Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.

15Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.

Wafalme Watano Wa Waamori Wauawa

1610:16 Za 68:12Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda. 17Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda, 18akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda. 19Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”

2010:20 Kum 20:16; 2Nya 11:10; Yer 4:5; 5:17; 8:14; 35:11Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma. 21Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.

22Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.” 23Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni. 2410:24 Kum 7:24; Mal 4:3; 2Sam 22:40; Za 110:1; Isa 51:23Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.

2510:25 Kum 31:6; 1Sam 17:37; Za 63:9; 2Tim 4:17; Kum 3:21; 7:19Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.” 2610:26 Hes 25:14; Yos 8:29; 2Sam 21:6-9; Es 2:23; Za 149:7-9Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.

2710:27 Kum 21:23; Mwa 35:20; Yos 8:9, 29Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.

2810:28 Kum 20:16; Yos 6:21Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.

Israeli Yaangamiza Miji Ya Kusini

2910:29 Hes 33:20; Yos 15:42; 21:13; 2Fal 8:22; 19:8Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia. 30Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.

3110:31 2Fal 14:19; Mik 1:13Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia. 32Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna. 3310:33 Yos 12:12; 16:3, 10; 21:21; Amu 1:29; 2Sam 5:25; 1Fal 9:15; 1Nya 6:67Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.

34Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia. 3510:35 Hes 13:22; Amu 1:10; 2Sam 5:14Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.

3610:36 Mwa 13:18; Yos 14:13; 15:13; 20:7; 21:11; Amu 16:3Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia. 37Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.

3810:38 Yos 15:15; Amu 1:11Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri. 39Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.

4010:40 Mwa 12:9; Yos 12:8; 15:19-21; 18:25; 1Sam 30:27; Kum 1:7; 7:24; 20:16-17; Yos 15:21-63; 19:1-8; Kut 23:31-33Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru. 4110:41 Mwa 14:17; 10:19; Yos 11:16; 15:51; Hes 13:17; 32:8; Kum 2:23Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni. 4210:42 Yos 10:14; Za 44:2; 80:8Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.

4310:43 Yos 5:9; 1Sam 11:14; 13:12Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.

Japanese Contemporary Bible

ヨシュア記 10:1-43

10

動かなくなった太陽と月

1エルサレムの王アドニ・ツェデクは、ヨシュアがエリコ同様アイを占領して破壊し、その王を殺害したことや、ギブオンの住民がイスラエルと和平交渉を行い、同盟を結んだことなどを聞いて、 2非常に恐れました。それは、ギブオンが実質的には王国の都のようであり、アイよりも大きく、そこの男たちはみな勇士だったからです。 3そこでアドニ・ツェデク王は、ヘブロンの王ホハム、ヤルムテの王ピルアム、ラキシュの王ヤフィア、エグロンの王デビルに使者を送り、 4こう伝えました。「さあ、ギブオンを滅ぼすために手を貸してくれ。彼らはヨシュアやイスラエル人どもと和を講じたからだ。」 5それで五人のエモリ人の王は、連合軍を編成してギブオンを攻撃しました。

6ギブオンの人々は急いで、ギルガルにいるヨシュアのもとへ伝令を走らせました。「しもべどもをお助けください。少しでも早く援軍を出してください。山地のエモリ人の王たちが連合して攻めて来ます。」 7そこでヨシュアはイスラエル軍を率いてギルガルを立ち、救援に向かいました。

8主はヨシュアに語りました。「恐れることはない。わたしは、彼らをあなたの手に渡した。一人としてあなたに立ち向かえる者はいない。」

9ヨシュアはギルガルから夜通し行軍して、敵軍を急襲しました。 10主が敵を混乱に陥れたので、イスラエル軍はギブオンで彼らに大打撃を与え、逃げる者をベテ・ホロンとアゼカとマケダまで追って打ち倒しました。 11敵がベテ・ホロンの丘を下って敗走する時、主はアゼカへ至る道に大粒の雹を降らせ続けて、彼らを滅ぼしました。事実、イスラエル軍が剣で殺した者よりも、雹に打たれて死んだ者のほうが多かったのです。

12イスラエル軍が敵を追いつめた時のことです。ヨシュアは民の前で大声で祈りました。「太陽よ、ギブオンの上にとどまれ。月よ、アヤロンの谷から動くな。」 13すると、太陽も月も、イスラエル軍が敵を全滅させるまで動かずにいました。この出来事は『ヤシャルの書』(イスラエルに古くから伝わる詩的文書)にくわしく記されています。太陽は丸一日、天にとどまっていました。 14こんなことは、あとにも先にもありませんでした。この日、主は一人の人の祈りを聞き入れ、イスラエルのために戦ったのです。 15そののち、ヨシュアとイスラエル軍は、ギルガルの陣営に引き揚げました。

16五人の王は戦いの最中に逃げ出し、マケダのほら穴に身を潜めていました。 17その王たちが見つかったという知らせを受けたヨシュアは、 18ほら穴の入口を大きな石でふさぎ、番兵を立てて、見張るよう命じました。 19続いて、ヨシュアは全軍に命じました。「敵のあとを追い、しんがりから切って捨てよ。みすみす生かして帰らせてはならない。主が敵を全滅させるために、力を貸してくださるからだ。」

20ヨシュアとイスラエル軍は、追撃の手を少しもゆるめず、五人の王の連合軍を全滅させました。ただ、ほんの一握りの者が生き残って、いのちからがら自分たちの町へ逃げ込みました。 21一方イスラエル軍は一人の兵士も失うことなく、マケダの陣営のヨシュアのもとに引き揚げたのです。このことがあってから、もはやイスラエルに刃向かう者はいなくなりました。

22-23さてヨシュアは、部下に命じて、ほら穴の入口から石を取り除き、エルサレム、ヘブロン、ヤルムテ、ラキシュ、エグロンの五人の王を連れて来させました。 24そして、イスラエル軍の指揮官たちに、王たちの首を踏みつけるよう命じ、 25言いました。「恐れたり、失望したりしてはならない。雄々しくあり、勇気を出しなさい。主は、すべての敵にこのようになさるからだ。」 26それから、ヨシュアは五人の王を次々に打ち、死体を五本の木にかけて、夕方までさらしました。 27日が沈むころ、死体を木から降ろさせ、彼らが隠れていたほら穴に投げ込むよう命じました。入口には石を山のように積み上げました。それは今も残っています。

28同じ日、ヨシュアはマケダの町を占領し、王と全住民を打ちました。 29次に、イスラエル軍はリブナへ向かい、 30そこでも、主がその町と王をイスラエルの手に渡したので、エリコと同様、最後の一人に至るまで剣で打ちました。

31さらにイスラエル軍は、リブナからラキシュを目指し、攻撃をかけました。 32二日目に、主がその町をイスラエルの手に渡したので、ここでもリブナ同様、全住民が打たれました。 33ラキシュ攻撃のさなか、ゲゼルの王ホラムが、ラキシュへ援軍を率いてやって来ましたが、ヨシュアはホラムをも倒して、彼らを一人も残しておきませんでした。

34-35次いでイスラエル軍はラキシュからエグロンに進み、一日でエグロンを占領し、ラキシュと全く同じようにしました。 36そのあとエグロンからヘブロンに進み、 37その町と周囲の村々を片っぱしから占領し、全住民を打ちました。 38それからデビルに引き返し、 39そこと周囲の村々をまたたく間に占領しました。そしてリブナと全く同じように、主と全住民を打ったのです。

40こうして、ヨシュアが率いるイスラエル軍は、山地、ネゲブ、低地、および山の斜面の国々と王とを征服したのです。彼らはイスラエルの神、主が命じたとおり、その地に住む者を打ち滅ぼしました。 41カデシュ・バルネアからガザまで、またゴシェンからギブオンまで、その地の全住民を打ったのです。 42これらはすべて、一度の出撃で果たしたものでした。イスラエルの神、主が、イスラエルのために戦ったからです。 43こうしてヨシュアは、全イスラエルを率い、ギルガルの陣営に凱旋しました。