Yona 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yona 4:1-11

Hasira Ya Yona Kwa Ajili Ya Huruma Ya Bwana.

14:1 Mt 20:11; 20:15; Lk 15:28Lakini Yona alichukizwa sana akakasirika. 24:2 Yer 20:7-8; Kum 4:31; Za 103:8; Kut 34:6; 22:27; Hes 14:18; Yoe 2:13Akamwomba Bwana, “Ee Bwana, hili si lile nililolisema nilipokuwa ningali nyumbani? Hii ndiyo sababu niliharikisha kukimbilia Tarshishi. Nikifahamu kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na huruma, si mwepesi wa hasira na umejaa upendo, ni Mungu ambaye hughairi katika kupeleka maafa. 34:3 Hes 11:15; Ay 7:15; Yer 8:3; 1Fal 19:4Sasa, Ee Bwana, niondolee uhai wangu, kwa kuwa ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”

44:4 Mwa 4:6; Mt 20:11-15Lakini Bwana akamjibu, “Je unayo haki yoyote kukasirika?”

5Yona akatoka nje akaketi mahali upande wa mashariki wa mji. Hapo akajitengenezea kibanda, akaketi kwenye kivuli chake na kungojea ni nini kitakachotokea katika mji. 64:6 Yon 1:17Ndipo Bwana, Mungu akaweka tayari mzabibu na kuufanya uote, kumpa Yona kivuli kilichomfunika kichwa ili kuondoa taabu yake, naye Yona akafurahi sana kwa ajili ya ule mzabibu. 74:7 Yoe 1:12Lakini kesho yake asubuhi na mapema Mungu akaamuru buu, autafune mzabibu huo nao ukanyauka. 84:8 Za 121:6; 1Fal 19:4Wakati jua lilipochomoza, Mungu akautuma upepo wa hari wa mashariki, nalo jua likawaka juu ya kichwa cha Yona mpaka akazimia. Akatamani kufa, naye akasema, “Ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”

9Lakini Mungu alimwambia Yona, “Je, unayo haki kukasirika kuhusu mzabibu huo?”

Akasema, “Ndiyo, ninayo haki. Nimekasirika kiasi cha kufa.”

10Lakini Bwana akamwambia, “Wewe unakasirika kwa ajili ya mzabibu huu, nawe hukuusababisha kuota wala kuutunza. Uliota usiku mmoja, nao ukafa usiku mmoja. 114:11 Eze 33:11; Kum 1:39; Za 36:6; Yon 1:2; 3:2; 3:1Lakini Ninawi ina zaidi ya watu 120,000 ambao hawawezi kupambanua kulia au kushoto, pamoja na ngʼombe wengi. Je, hainipasi kufikiri juu ya mji ule mkubwa?”

King James Version

Jonah 4:1-11

1But it displeased Jonah exceedingly, and he was very angry. 2And he prayed unto the LORD, and said, I pray thee, O LORD, was not this my saying, when I was yet in my country? Therefore I fled before unto Tarshish: for I knew that thou art a gracious God, and merciful, slow to anger, and of great kindness, and repentest thee of the evil. 3Therefore now, O LORD, take, I beseech thee, my life from me; for it is better for me to die than to live.

4¶ Then said the LORD, Doest thou well to be angry?4.4 Doest…: or, Art thou greatly angry?

5So Jonah went out of the city, and sat on the east side of the city, and there made him a booth, and sat under it in the shadow, till he might see what would become of the city. 6And the LORD God prepared a gourd, and made it to come up over Jonah, that it might be a shadow over his head, to deliver him from his grief. So Jonah was exceeding glad of the gourd.4.6 gourd: or, palmcrist: Heb. Kikajon4.6 was…: Heb. rejoiced with great joy 7But God prepared a worm when the morning rose the next day, and it smote the gourd that it withered. 8And it came to pass, when the sun did arise, that God prepared a vehement east wind; and the sun beat upon the head of Jonah, that he fainted, and wished in himself to die, and said, It is better for me to die than to live.4.8 vehement: or, silent 9And God said to Jonah, Doest thou well to be angry for the gourd? And he said, I do well to be angry, even unto death.4.9 Doest…: or, Art thou greatly angry?4.9 I do well…: or, I am greatly angry 10Then said the LORD, Thou hast had pity on the gourd, for the which thou hast not laboured, neither madest it grow; which came up in a night, and perished in a night:4.10 had pity: or, spared4.10 came…: Heb. was the son of the night 11And should not I spare Nineveh, that great city, wherein are more than sixscore thousand persons that cannot discern between their right hand and their left hand; and also much cattle?