Yona 2 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yona 2:1-10

Maombi Ya Yona Katika Tumbo La Nyangumi

1Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake. 22:2 Za 18:6; 120:1; 86:13; Mao 3:55Akasema:

“Katika shida yangu nalimwita Bwana,

naye akanijibu.

Kutoka kina cha kaburi2:2 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. niliomba msaada,

nawe ukasikiliza kilio changu.

32:3 Za 88:6; 42:7; 2Sam 22:5Ulinitupa kwenye kilindi,

ndani kabisa ya moyo wa bahari,

mikondo ya maji ilinizunguka,

mawimbi yako yote na viwimbi

vilipita juu yangu.

42:4 Za 31:22; Yer 7:15; Isa 49:14; 1Fal 8:38, 48Nikasema, ‘Nimefukuziwa

mbali na uso wako,

hata hivyo nitatazama tena

kuelekea Hekalu lako takatifu.’

52:5 Za 69:1-2Maji yaliyonimeza yalinitisha,

kilindi kilinizunguka;

mwani2:5 Mwani hapa maana yake ni magugu yaotayo kwenye sakafu ya kilindi cha bahari. ulijisokota kichwani pangu.

62:6 Ay 28:9; 17:16; 33:18; Za 30:3Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima,

makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele.

Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni,

Ee Bwana Mungu wangu.

72:7 Za 11:4; 18:6; 77:11-12; 34:6; 130:2; Yer 2:13; 2Nya 30:27“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka,

nilikukumbuka wewe, Bwana,

nayo maombi yangu yalikufikia wewe,

katika Hekalu lako takatifu.

82:8 1Sam 12:21; Yer 10:8; 2Fal 17:15; Za 31:6; Kum 32:21“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa

hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.

92:9 Hos 14:2; Ebr 13:15; Hes 30:2; Kut 15:2; Za 50:14; 116:14; 66:13-15; 3:8; 42:4Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,

nitakutolea dhabihu.

Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza.

Wokovu watoka kwa Bwana.”

102:10 Yn 1:17; Mt 8:9Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

Ketab El Hayat

يونان 2:1-10

صلاة يونان

1ثُمَّ صَلَّى يُونَانُ إِلَى الرَّبِّ إِلَهِهِ مِنْ جَوْفِ الْحُوتِ، 2قَائِلاً: «اسْتَغَثْتُ بِالرَّبِّ فِي ضِيقِي فَاسْتَجَابَ لِي، وَمِنْ جَوْفِ الْهَاوِيَةِ ابْتَهَلْتُ فَسَمِعْتَ صَوْتِي. 3لأَنَّكَ طَرَحْتَنِي إِلَى اللُّجَجِ الْعَمِيقَةِ فِي قَلْبِ الْبِحَارِ، فَاكْتَنَفَنِي الْغَمْرُ وَأَحَاطَتْ بِي تَيَّارَاتُكَ وَأَمْوَاجُكَ 4فَقُلْتُ: قَدْ طُرِدْتُ مِنْ حَضْرَتِكَ، وَلَنْ أَعُودَ أَتَفَرَّسُ فِي هَيْكَلِكَ الْمُقَدَّسِ. 5قَدْ غَمَرَتْنِي الْمِيَاهُ وَأَحْدَقَتْ بِيَ اللُّجَجُ، وَالْتَفَّ عُشْبُ الْبَحْرِ حَوْلَ رَأْسِي. 6انْحَدَرْتُ إِلَى أُسُسِ الْجِبَالِ وَهَبَطْتُ إِلَى أَعْمَاقِ الأَرْضِ حَيْثُ أُغْلِقَتْ عَلَيَّ مَزَالِيجُهَا إِلَى الأَبَدِ. وَلَكِنَّكَ تُصْعِدُ حَيَاتِي مِنَ الْهَاوِيَةِ أَيُّهَا الرَّبُّ إِلَهِي. 7عِنْدَمَا وَهَنَتْ نَفْسِي فِي دَاخِلِي، تَذَكَّرْتُ إِلَهِي، فَحَلَّقَتْ صَلاتِي إِلَيْكَ، إِلَى هَيْكَلِكَ الْمُقَدَّسِ. 8إِنَّ الَّذِينَ يُبَجِّلُونَ الأَصْنَامَ الْبَاطِلَةَ يَتَخَلَّوْنَ عَنْ مَصْدَرِ نِعْمَتِهِمْ. 9أَمَّا أَنَا فَبِهُتَافِ الْحَمْدِ أَذْبَحُ لَكَ، وَمَا نَذَرْتُهُ أُوفِي بِهِ، لأَنَّ لِلرَّبِّ الْخَلاصَ».

10فَأَمَرَ الرَّبُّ الْحُوتَ فَقَذَفَ بِيُونَانَ إِلَى الشَّاطِئِ.