Yona 2 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yona 2:1-10

Maombi Ya Yona Katika Tumbo La Nyangumi

1Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake. 22:2 Za 18:6; 120:1; 86:13; Mao 3:55Akasema:

“Katika shida yangu nalimwita Bwana,

naye akanijibu.

Kutoka kina cha kaburi2:2 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. niliomba msaada,

nawe ukasikiliza kilio changu.

32:3 Za 88:6; 42:7; 2Sam 22:5Ulinitupa kwenye kilindi,

ndani kabisa ya moyo wa bahari,

mikondo ya maji ilinizunguka,

mawimbi yako yote na viwimbi

vilipita juu yangu.

42:4 Za 31:22; Yer 7:15; Isa 49:14; 1Fal 8:38, 48Nikasema, ‘Nimefukuziwa

mbali na uso wako,

hata hivyo nitatazama tena

kuelekea Hekalu lako takatifu.’

52:5 Za 69:1-2Maji yaliyonimeza yalinitisha,

kilindi kilinizunguka;

mwani2:5 Mwani hapa maana yake ni magugu yaotayo kwenye sakafu ya kilindi cha bahari. ulijisokota kichwani pangu.

62:6 Ay 28:9; 17:16; 33:18; Za 30:3Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima,

makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele.

Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni,

Ee Bwana Mungu wangu.

72:7 Za 11:4; 18:6; 77:11-12; 34:6; 130:2; Yer 2:13; 2Nya 30:27“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka,

nilikukumbuka wewe, Bwana,

nayo maombi yangu yalikufikia wewe,

katika Hekalu lako takatifu.

82:8 1Sam 12:21; Yer 10:8; 2Fal 17:15; Za 31:6; Kum 32:21“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa

hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.

92:9 Hos 14:2; Ebr 13:15; Hes 30:2; Kut 15:2; Za 50:14; 116:14; 66:13-15; 3:8; 42:4Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,

nitakutolea dhabihu.

Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza.

Wokovu watoka kwa Bwana.”

102:10 Yn 1:17; Mt 8:9Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

Korean Living Bible

요나 2:1-10

요나의 기도

1요나는 물고기 뱃속에서 자기 하나님 여호와께 이렇게 기도하였다.

2“내가 고통 중에

주께 부르짖었더니

주께서는 나에게 응답하셨으며

내가 2:2 또는 ‘스올의 뱃속에서’무덤과 같은 곳에서

주의 도움을 구하였더니

주께서 내 음성을 들으셨습니다.

3주께서 나를

바다 깊은 곳에 던지셨으므로

물이 나를 두르고

주의 큰 파도가 나를 덮쳤습니다.

4내가 주 앞에서 쫓겨났으나

나는 다시 주의 성전을

바라보겠다고 말하였습니다.

5물이 나를 덮쳐

내가 바다 깊은 곳에 빠졌을 때

바다풀이 내 머리를 휘감았습니다.

6내가 해저의 산 밑바닥까지 내려가

2:6 또는 ‘땅이 그 빗장으로 나를 오래도록 막았사오나’죽음의 땅에 갇혀 있었으나

나의 하나님 여호와여,

주께서 내 생명을

죽음에서 구해 내셨습니다.

7“내 생명이 서서히 사라져 갈 때

내가 다시 한번 여호와를 생각하며

기도하였더니

성전에 계시는 주께서

내 기도를 들으셨습니다.

8무가치한 우상을 숭배하는 자들은

주의 자비를 저버린 자들입니다.

9그러나 나는 감사의 노래로

주께 제사를 드리며

내가 서약한 것을 지키겠습니다.

구원은

여호와께서 주시는 것입니다.”

10여호와께서 물고기에게 명령하시자 그 물고기가 요나를 해변에 토해 내었다.