Yona 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yona 2:1-10

Maombi Ya Yona Katika Tumbo La Nyangumi

1Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake. 22:2 Za 18:6; 120:1; 86:13; Mao 3:55Akasema:

“Katika shida yangu nalimwita Bwana,

naye akanijibu.

Kutoka kina cha kaburi2:2 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. niliomba msaada,

nawe ukasikiliza kilio changu.

32:3 Za 88:6; 42:7; 2Sam 22:5Ulinitupa kwenye kilindi,

ndani kabisa ya moyo wa bahari,

mikondo ya maji ilinizunguka,

mawimbi yako yote na viwimbi

vilipita juu yangu.

42:4 Za 31:22; Yer 7:15; Isa 49:14; 1Fal 8:38, 48Nikasema, ‘Nimefukuziwa

mbali na uso wako,

hata hivyo nitatazama tena

kuelekea Hekalu lako takatifu.’

52:5 Za 69:1-2Maji yaliyonimeza yalinitisha,

kilindi kilinizunguka;

mwani2:5 Mwani hapa maana yake ni magugu yaotayo kwenye sakafu ya kilindi cha bahari. ulijisokota kichwani pangu.

62:6 Ay 28:9; 17:16; 33:18; Za 30:3Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima,

makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele.

Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni,

Ee Bwana Mungu wangu.

72:7 Za 11:4; 18:6; 77:11-12; 34:6; 130:2; Yer 2:13; 2Nya 30:27“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka,

nilikukumbuka wewe, Bwana,

nayo maombi yangu yalikufikia wewe,

katika Hekalu lako takatifu.

82:8 1Sam 12:21; Yer 10:8; 2Fal 17:15; Za 31:6; Kum 32:21“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa

hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.

92:9 Hos 14:2; Ebr 13:15; Hes 30:2; Kut 15:2; Za 50:14; 116:14; 66:13-15; 3:8; 42:4Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,

nitakutolea dhabihu.

Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza.

Wokovu watoka kwa Bwana.”

102:10 Yn 1:17; Mt 8:9Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約拿書 2:1-10

約拿的禱告

1約拿在魚腹中向他的上帝耶和華禱告說:

2「我遭遇患難的時候向你求告,

你就應允我。

我在陰間的深處呼求你,

你也垂聽我的聲音。

3你把我拋進深海,

茫茫大海把我吞沒,

你的巨浪洪濤淹沒我。

4我心想,你已經驅逐我離開你的面,

但我要再瞻仰你的聖殿。

5波濤環繞我,

深淵吞沒我,

海草纏繞著我的頭。

6我下沉到山的根基,

大地的門把我永遠關住;

然而,我的上帝耶和華啊,

你卻把我的性命從深坑中拯救出來。

7我的生命漸漸消逝的時候,

我就想起了耶和華。

我的禱告進入你的聖殿,

達到你面前。

8那些信奉虛無神明的人,

背棄了憐愛他們的主2·8 背棄了憐愛他們的主」或譯「背棄了他們對主的忠誠」。

9但我要用感謝的聲音向你獻祭,

我必還我許的願,

因為救恩來自耶和華。」

10於是,耶和華命令那條魚,

魚就把約拿吐到陸地上。