Mwanamke Aliyefumaniwa Akizini
18:1 Mt 21:1Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni. 28:2 Mt 26:55Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha. 3Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote. 4Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini. 58:5 Kum 22:22; Ay 31:11Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?” 68:6 Mt 22:15-18; 12:10Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki.
Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake. 78:7 Kum 17:7; Eze 16:40; Rum 2:1, 22Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.” 8Akainama tena na kuandika ardhini.
98:9 Rum 2:22Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake. 10Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
118:11 Yn 3:17; 5:14Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.”
Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
Yesu Nuru Ya Ulimwengu
128:12 Yn 6:35; 12:35; Mit 4:18; Mt 5:14Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
138:13 Yn 5:31Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
148:14 Yn 13:3; 16:28; 7:28; 9:29Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda. 158:15 Yn 7:24; 3:17Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote. 168:16 Yn 5:30Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma. 17Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti. 188:18 Yn 5:37Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
198:19 Yn 16:3; 14:7; 1Yn 2:23Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?”
Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.” 208:20 Mt 26:18, 55; Mk 12:41; Yn 7:30Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
Yesu Atabiri Kifo Chake Mwenyewe
218:21 Eze 3:18; Yn 7:34; 13:33Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
228:22 Yn 7:35Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
238:23 Yn 3:31; 17:14Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu. 248:24 Yn 4:26; 13:19Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
258:25 Yn 8:14Wakamuuliza, “Wewe ni nani?”
Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo. 268:26 Yn 7:28; 3:32; 15:15Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni. 288:28 Yn 3:14; 5:19Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha. 298:29 Yn 16:32; Isa 50:5; Yn 4:34Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’ ” 308:30 Yn 7:31Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
Wanafunzi Wa Kweli
318:31 Yn 15:7; 2Yn 9Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli. 328:32 Gal 5:1, 13; Yak 2:12Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
338:33 Mk 3:9; Lk 3:8Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
348:34 Rum 6:16; 2Pet 2:19Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. 358:35 Gal 4:30Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. 368:36 Rum 8:2; Gal 5:1Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli. 378:37 Yn 7:19; 8:40Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu. 388:38 Yn 5:19, 30; 14:10, 24Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
Yesu Na Abrahamu
398:39 Lk 3:8; Gal 3:7Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.”
Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu. 408:40 Yn 8:37; 8:26Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii. 418:41 Isa 63:16; 64:8; Mal 1:6Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.”
Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
428:42 1Yn 5:1; Yn 16:27; 7:28; 3:17Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma. 438:43 Yn 7:17Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho. 448:44 1Yn 3:8; 2Nya 18:21; Za 12:2Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo. 458:45 Yn 18:37Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini! 468:46 2Kor 5:21; 1Pet 2:22Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini? 478:47 Yn 18:37; 1Yn 4:6Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
Maelezo Ya Yesu Kuhusu Yeye Mwenyewe
488:48 Mt 10:5; Mk 3:22; Yn 7:20Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
49Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau. 508:50 Yn 7:20; 8:54; 10:20Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi. 518:51 Yn 11:26Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.”
528:52 Zek 1:5; Ebr 11:13Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ 538:53 Yn 4:12Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
548:54 Yn 16:14; 17:1-5Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi. 558:55 Yn 7:28-29; 15:10Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake. 568:56 Mwa 18:18; Mt 13:17; Ebr 11:13Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
57Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
588:58 Yn 1:2; 17:5, 24; Kut 3:14; 6:3Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’ ” 598:59 1Sam 30:6; Yn 11:8; 12:36Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.
1ישוע הלך להר הזיתים, 2אולם למחרת בבוקר חזר לבית־המקדש. עד מהרה התאספו סביבו אנשים רבים והוא החל ללמד אותם. 3בעודו מלמד הביאו אליו הסופרים והפרושים אישה שנתפסה במעשה ניאוף, והעמידו אותה לפני הקהל.
4”רבי, אישה זאת נתפסה במעשה ניאוף,“ אמרו, 5”ותורת משה מצווה עלינו לרגום באבנים נשים כאלה. מה דעתך?“
6הם רצו לנסות את ישוע, שכן חיפשו סיבה להכשיל ולהרשיע אותו. אולם ישוע התכופף וצייר באצבעו על הקרקע. 7כשהאיצו בו הסופרים והפרושים להשיב לשאלתם, הזדקף ישוע ואמר: ”מי שלא חטא מעולם ישליך בה את האבן הראשונה!“
8הוא התכופף שוב והמשיך לצייר באצבעו על הקרקע. 9כל השומעים נמלאו בושה, ובזה אחר זה עזבו את המקום, מזקן עד צעיר, וישוע נותר לבדו עם האישה.
10ישוע נשא את ראשו וראה שנותר לבדו עם האישה. ”היכן מאשימיך? האם הרשיע אותך מישהו?“ שאל אותה. 11”לא אדוני“, השיבה האישה.
”אם כן גם אני לא ארשיע אותך. לכי לשלום ואל תחטאי יותר.“ 12ישוע דיבר שוב אל העם: ”אני אור העולם. כל ההולך אחרי לא יתעה שוב בחשכה, אלא יקבל את אור החיים“.
13”אתה סתם מתפאר בעצמך ודבריך אינם מוכיחים דבר!“ קראו לעברו הפרושים. 14”אני אמנם מעיד על עצמי, אולם דברי נכונים, שכן אני יודע מאין באתי ולאן אני הולך. 15אתם שופטים אותי לפי קנה־המידה של העולם, ואילו אני איני שופט איש עתה. 16אם אני בכל זאת שופט, אני שופט בצדק, כי איני מחליט על דעת עצמי; אני מתייעץ עם אלוהים האב אשר שלח אותי. 17התורה אומרת כי על־פי שני עדים יקום דבר, לא כן? 18ובכן, אני עד אחד, ואבי אשר שלחני הוא העד השני.“
19”היכן אביך?“ שאלו אותו.
”אינכם יודעים מיהו אבי, מפני שאינכם יודעים מי אני. לו היכרתם אותי הייתם מכירים גם את אבי.“
20ישוע דיבר דברים אלה באגף האוצר בבית־המקדש, אולם איש לא אסר אותו, כי טרם הגיע המועד.
21”אני הולך מכאן“, המשיך ישוע. ”אתם תחפשו אותי ותמותו בחטאיכם. אינכם יכולים לבוא למקום שאליו אני הולך.“
22”האם הוא עומד להתאבד?“ תמהו היהודים. ”למה הוא מתכוון באמרו: ’אינכם יכולים לבוא למקום שאליו אני הולך‘?“
23ישוע הסביר להם: ”מקומי בשמים מעל, ואילו מקומכם בארץ למטה; אתם שייכים לעולם הזה, ואני איני מהעולם הזה. 24משום כך אמרתי לכם שתמותו בחטאיכם; אם לא תאמינו שאני הוא תמותו בחטאיכם.“
25”מי אתה?“ שאלו.
”אני הוא זה שאמרתי לכם כל הזמן“, השיב ישוע. 26”יש לי הרבה דברים לומר עליכם, לשפוט ולהרשיע אתכם, אך איני עושה זאת. אני מוסר לכם אך ורק מה שנאמר לי על־ידי שולחי, שהוא האמת.“ 27והם עדיין לא הבינו שהוא התכוון לאלוהים. 28ישוע המשיך: ”כאשר תרימו את בן־האדם (על הצלב), תדעו ותבינו שאני הוא המשיח ושאיני עושה דבר על דעת עצמי, אלא אני מספר לכם מה שלימד אותי אבי. 29שולחי תמיד איתי; הוא לא נטש אותי, כי אני עושה תמיד את הטוב בעיניו.“
30כשדיבר ישוע דברים אלה, יהודים רבים האמינו שהוא המשיח. 31על כן הוא אמר להם: ”אם תקיימו את דברי תהיו תלמידי באמת. 32אתם תדעו את האמת, והאמת תוציא אתכם לחופשי!“
33”זרע אברהם אנחנו,“ קראו היהודים לעומתו, ”ומעולם לא היינו עבדים לאיש. כיצד, אם כן, אתה אומר שנהיה בני־חורין?“
34”אני אומר לכם במלוא האמת,“ ענה ישוע, ”כל מי שחוטא הוא עבד לחטא, 35ולעבד אין כל זכויות, בעוד שלבן יש את כל הזכויות. 36לכן, אם הבן מוציא אתכם לחופשי, תהיו חופשיים באמת! 37אני יודע שזרע אברהם אתם, אולם יש ביניכם אחדים שרוצים להרוג אותי, מפני שאינם יכולים לסבול את דברי. 38אני מספר לכם את מה שראיתי אצל אבי, ואילו אתם עושים את מה שראיתם אצל אביכם.“
39”אברהם הוא אבינו!“ השיבו היהודים.
אולם ישוע השיב: ”אילו הייתם בני אברהם, הייתם נוהגים כמוהו. 40אולם עתה מבקשים אתם להרוג אותי על שסיפרתי לכם את האמת אשר שמעתי מאלוהים. אברהם מעולם לא היה עושה דבר כזה! 41ואילו אתם עושים את מעשי אביכם האמתי.“
”אין אנו ממזרים! יש לנו אב אחד – האלוהים!“ טענו.
42אולם ישוע המשיך: ”אילו אלוהים היה באמת אביכם, אזי הייתם אוהבים אותי, שהרי באתי אליכם מאת האלוהים. לא באתי על דעת עצמי – אלוהים שלח אותי. 43האם אתם יודעים מדוע אינכם מבינים את דברי? מפני שאינכם מסוגלים להקשיב לי. 44השטן הוא אביכם, ואתם רוצים לעשות את חפצו! הוא היה רוצח ונשאר רוצח; הוא שונא את האמת, כי אין בו שמץ של אמת; כל דבריו הם שקר בכוונה תחילה, שהרי הוא מלך השקרים. 45אינכם מאמינים לי משום שאני אומר את האמת. 46האם יכול מישהו מכם להוכיח אותי על איזשהו עוון? ואם אני אומר את האמת, מדוע אינכם מאמינים לי? 47ילדי האלוהים מקשיבים בשמחה לקול אביהם, אולם אתם אינכם מקשיבים, כי אינכם ילדי האלוהים!“
48”בצדק קראנו לך שומרוני!“ קראו בחזרה בחימה. ”שד נכנס בך!“
49”לא נכנס בי שד“, ענה ישוע. ”אתם לועגים ובזים לי רק מפני שאני מכבד את אבי. 50איני מבקש כבוד לעצמי, אולם אלוהים אבי דורש זאת למעני, והוא ישפוט את מי שאינו מאמין בי. 51אני אומר לכם ברצינות ובכנות: מי שישמע בקולי לא ימות לעולם!“
52”עכשיו אנחנו בטוחים שנכנס בך שד“, אמרו לו. ”אפילו אברהם והנביאים מתו, ואילו אתה טוען שכל השומע בקולך לא ימות לעולם? 53האם אתה גדול וחזק מאברהם אבינו או מהנביאים? למי אתה חושב את עצמך?“
54”אם אני מכבד את עצמי, אין לכך כל ערך“, אמר ישוע. ”אולם אבי מכבד אותי – כן, האב אשר אתם קוראים לו אלוהיכם 55למרות אינכם מכירים אותו. אולם אני מכיר אותו, ואם אכחיש זאת אהיה לשקרן כמוכם. אני באמת מכיר אותו ושומע בקולו. 56אברהם אביכם שש לראות את יום בואי; הוא ראה אותו ושמח.“
57”איך יכולת לראות את אברהם?“ שאלו היהודים בחוסר אמון. ”לא מלאו לך עדיין חמישים שנה אפילו!“
58”אמן אומר אני לכם, עוד לפני שאברהם נולד, אני הוא!“ השיב ישוע.
59דבריו עוררו את חמתם, והם החלו להשליך עליו אבנים. אולם ישוע נעלם מעיניהם, עבר על פניהם ויצא מהמקדש.