Yohana 6 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 6:1-71

Yesu Alisha Wanaume 5,000

(Mathayo 14:13-21; Marko 6:30-44; Luka 9:10-17)

16:1 Mt 14:15; Mk 6:35; Lk 9:10, 12Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia. 26:2 Yn 2:11-13Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa. 36:3 Yn 6:15Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. 46:4 Yn 11:55Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.

56:5 Yn 1:43Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?” 6Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.

76:7 Hes 11:21, 22Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili,6:7 Dinari 200 ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku 200; mshahara wa kibarua ulikuwa dinari moja kwa siku. hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”

86:8 Yn 1:40Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia, 96:9 2Fal 4:43“Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”

10Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000. 116:11 Mt 14:19Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.

12Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.” 13Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.

146:14 Yn 2:11; Kum 18:15-18; Mt 21:11Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!” 156:15 Yn 18:36; Mt 14:23; Mk 6:46Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.

Yesu Atembea Juu Ya Maji

(Mathayo 14:22-33; Marko 6:45-52)

166:16 Mt 14:22-33; Mk 6:45-52Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini. 17Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao. 18Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma. 196:19 Ay 9:8Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne,6:19 Maili tatu au nne ni kama kilomita 5 au 6. walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana. 206:20 Mt 14:27Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.” 21Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.

Watu Wanamtafuta Yesu

226:22 Yn 6:2; 15:21Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao. 236:23 Yn 6:1, 11Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu. 24Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.

Yesu Ni Mkate Wa Uzima

256:25 Mt 23:7Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”

266:26 Yn 2:11Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba. 276:27 Mt 25:46; Yn 4:14; Mt 8:20; 2Tim 2:19; Ufu 7:3Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.”

28Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”

296:29 1Yn 3:23; 3:17Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”

306:30 Yn 2:11; Mt 12:38Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani? 316:31 Hes 11:7-9; Neh 9:15; Za 105:40Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’ ”

326:32 Yn 6:49Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni. 336:33 Yn 3:13, 31Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”

346:34 Yn 4:15Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”

356:35 Yn 4:14; 6:48; 7:37Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe. 366:36 Yn 6:26, 29Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini. 376:37 Yn 17:2-6, 9, 24Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe. 386:38 Yn 3:17; 4:34Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma. 396:39 Isa 27:3; Yn 18:9Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho. 406:40 Mt 25:26Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.”

41Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.” 426:42 Lk 4:22; Yn 7:27, 28Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”

43Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi. 44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho. 456:45 Isa 54:13; 1Kor 2:13Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu. 466:46 Yn 1:18; 7:29Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba. 476:47 Mt 25:46Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. 486:48 Yn 6:35, 51Mimi ni mkate wa uzima. 496:49 Yn 6:3, 58Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa. 506:50 Yn 6:33Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa. 516:51 Ebr 10:10Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”

526:52 Yn 9:16; 10:19Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”

536:53 Mt 26:26; 8:20; 26:28Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. 546:54 Yn 6:39Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. 55Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 566:56 1Yn 2:24; 3:24Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. 576:57 Yn 3:17Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu. 586:58 Yn 3:36; 5:24Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” 59Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.

Wafuasi Wengi Wamwacha Yesu

606:60 Yn 6:66; 6:52Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”

616:61 Mt 13:57Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi? 626:62 Mk 16:19; Yn 17:5Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza? 636:63 2Kor 3:6Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima. 646:64 Yn 2:24-25Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti. 656:65 Mt 13:11Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”

666:66 Yn 6:60Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.

676:67 Mt 10:2Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”

686:68 Mt 16:16Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. 696:69 Mk 1:24; Lk 9:20Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”

706:70 Yn 15:16-19; 13:27; 17:12Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.” 716:71 Mt 26:14; 10:4(Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)

O Livro

João 6:1-71

Jesus alimenta 5000 homens

(Mt 14.13-21; Mc 6.30-44; Lc 9.10-17)

1Depois disso, Jesus atravessou o mar da Galileia, também conhecido como mar de Tiberíades. 2Uma multidão enorme seguia-o, pois via os sinais que fazia curando os doentes. 3Assim, Jesus subiu ao monte e sentou-se com os discípulos à sua volta. 4Estava próxima a Páscoa, a festa anual judaica. 5Em breve viu que um grande grupo de pessoas subia também a colina à sua procura. Voltando-se para Filipe, perguntou: “Filipe, onde poderemos comprar pão para alimentarmos esta gente toda?” 6Estava a experimentá-lo, pois já sabia o que ia fazer.

7Filipe respondeu-lhe: “Nem com duzentas moedas de prata6.7 Literalmente, duzentos denários. se comprava pão suficiente para dar um pedaço a cada pessoa.” 8Um dos discípulos, André, irmão de Simão Pedro, acrescentou: 9“Está aqui um rapaz com cinco pães de cevada e alguns peixes! Mas de que serve para uma multidão tão numerosa?”

10“Digam a toda a gente que se sente”, ordenou Jesus. E todos se sentaram na colina relvada; só homens eram aproximadamente 5000. 11Jesus, pegando nos pães, deu graças a Deus e distribuiu-os entre o povo. Depois fez o mesmo com os peixes. E toda a gente comeu até estar satisfeita. 12“Agora juntem os sobejos”, disse Jesus aos discípulos, “para que nada se estrague.” 13E encheram-se doze cestos, só de sobras.

14Quando o povo se deu conta daquele grande sinal, exclamou: “Sem dúvida é este o Profeta cuja vinda temos esperado!” 15Jesus percebeu que estavam a ponto de o levar para fazer dele o seu rei. Por isso, subiu o monte, ainda mais para o alto, ficando sozinho.

Jesus anda sobre a água

(Mt 14.22-36; Mc 6.45-52)

16Ao cair da noite, os discípulos desceram à praia para o esperar. 17Como estava escuro e Jesus ainda não tinha voltado, meteram-se no barco e remaram para Cafarnaum, do outro lado do lago. 18Em breve, porém, se abateu um vendaval sobre eles, enquanto remavam, e o mar ficou bravo. 19Encontravam-se a cinco ou seis quilómetros de terra quando viram Jesus a caminhar sobre o mar e perto do barco, e ficaram cheios de medo. 20Mas ele disse-lhes: “Sou eu! Não tenham medo!” 21Fizeram-no entrar e logo o barco chegou ao destino desejado.

22Na manhã seguinte, de novo no outro lado, as multidões começaram a juntar-se na praia, pois sabiam que ele e os discípulos tinham atravessado juntos e que estes últimos tinham partido no barco, deixando-o em terra. 23Encontravam-se ali perto várias embarcações pequenas de Tiberíades, perto do local onde tinham comido o pão pelo qual o Senhor tinha dado graças. 24Quando o povo viu que nem Jesus nem os discípulos estavam ali, meteu-se nas embarcações e atravessou para Cafarnaum, a fim de o procurar.

Jesus, o pão da vida

25Quando chegaram e o encontraram, disseram: “Mestre, quando chegaste aqui?”

26Jesus retorquiu: “É realmente como vos digo: vieram ter comigo não porque viram sinais, mas porque vos alimentei e ficaram satisfeitos. 27Mas não se devem preocupar tanto com coisas que se acabam, tal como o alimento. Trabalhem antes pelo alimento que dura para a vida eterna, que o Filho do Homem vos há de dar, pois disso mesmo o Pai o encarregou.”

28Perguntaram-lhe então: “Que devemos fazer para obedecer à vontade de Deus?”

29“A vontade de Deus é que creiam naquele que ele enviou.”

30Eles responderam: “Que sinal fazes para que creiamos em ti? 31Os nossos pais comeram do maná, no deserto, como dizem as Escrituras: ‘deu-lhes pão do céu, para se alimentarem.’ ”6.31 Êx 16.4; Ne 9.15; Sl 78.24-25.

32Jesus disse: “É realmente como vos digo: não foi Moisés quem lho deu, mas meu Pai. Mas agora ele oferece-vos o verdadeiro pão do céu. 33O pão verdadeiro é aquele que foi enviado do céu por Deus e que dá a vida ao mundo.”

34“Senhor, dá-nos sempre desse pão!”

35“Eu sou o pão da vida. Quem vem a mim não terá fome. Quem crê em mim nunca terá sede. 36O pior, como vos disse, é não acreditarem, mesmo depois de me terem visto. 37Mas alguns virão ter comigo, aqueles que o Pai me deu, e a esses jamais mandarei embora. 38Eu vim do céu para fazer a vontade de Deus, que me enviou, e não a minha. 39E a vontade de Deus é esta: que eu não perca nem um só daqueles que ele me deu, antes os faça viver de novo para a vida eterna, no último dia. 40Porque a vontade de meu Pai é que todo aquele que vê o Filho, e nele crê, tenha a vida eterna, para que lhe torne a dar vida no último dia.”

41Então os judeus começaram a murmurar contra ele por dizer que era o pão do céu. 42“O quê?”, interrogavam-se. “Ele não é outro senão Jesus, filho de José, cujo pai e a mãe conhecemos. Que é isto que diz agora, que veio do céu?”

43Mas Jesus respondeu: “Não murmurem por eu ter dito isto. 44Ninguém pode vir a mim se o Pai, que me enviou, o não atrair a mim, e no último dia os trarei a todos de novo para a vida. 45Como dizem as Escrituras, ‘Todos eles serão ensinados por Deus.’6.45 Is 54.13. Aqueles que escutam o Pai e que dele aprendem serão atraídos para mim. 46Aliás, ninguém realmente vê o Pai; só eu o vi.

47É realmente como vos digo: quem crê em mim tem a vida eterna! 48Eu sou o pão da vida! 49Os vossos antepassados, no deserto, comeram o maná e morreram. 50Mas aqui está o pão que veio do céu e que dá a vida a todo aquele que o come. 51Eu sou o pão da vida que veio do céu. Quem comer deste pão viverá para sempre. A minha carne é esse pão que darei para dar vida à humanidade.”

52Então os judeus começaram a discutir entre si acerca do que queriam dizer as suas palavras. “Como nos pode este homem dar a sua carne a comer?”

53E Jesus repetiu: “É realmente como vos digo: a não ser que comam a carne do Filho do Homem e bebam o seu sangue, não têm vida em vocês mesmos. 54Mas quem comer a minha carne e beber o meu sangue tem a vida eterna e eu o ressuscitarei no último dia. 55Porque a minha carne é o alimento verdadeiro e o meu sangue é a bebida verdadeira. 56Quem come a minha carne e bebe o meu sangue está em mim e eu nele. 57Assim como eu vivo pelo Pai, que me enviou e vive eternamente, do mesmo modo, aqueles que se alimentam de mim por mim viverão. 58Eu sou o pão vindo do céu; todo aquele que comer deste pão viverá para sempre e não morrerá. Não é o caso dos vossos antepassados que comeram o maná e morreram.”

59Estas coisas ele disse enquanto ensinava na sinagoga em Cafarnaum.

Muitos discípulos abandonam Jesus

60Muitos dos seus discípulos diziam: “Isto é muito difícil de compreender. Quem é que pode aceitar estas coisas?”

61Jesus sabia que os seus discípulos se queixavam e disse-lhes: “Estas coisas chocam-vos? 62Então o que pensarão quando me virem, a mim, o Filho do Homem, voltar de novo para o céu? 63Só o Espírito Santo dá a vida eterna. Pelo poder humano jamais se receberá este dom. As palavras que eu vos disse são espírito e vida. 64Alguns de vocês, porém, não creem em mim.” Pois Jesus sabia, desde o princípio, quem não cria e quem o ia trair. 65“Era isto que eu queria dizer quando revelei que ninguém pode vir a mim a não ser que o Pai o traga.”

66Nesta altura muitos dos seus discípulos afastaram-se e abandonaram-no. 67Jesus voltou-se para os doze e perguntou-lhes: “Também se querem ir embora?”

68Simão Pedro respondeu: “Mestre, para quem iremos nós? Só tu tens as palavras que dão a vida eterna! 69Nós acreditamos nelas e sabemos que és o Santo de Deus.”

70Então Jesus informou: “Escolhi-vos a todos, mas um é um diabo.” 71Falava-lhes de Judas, filho de Simão Iscariotes, um dos doze, que o iria trair.