Yohana 4 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 4:1-54

Yesu Azungumza Na Mwanamke Msamaria

14:1 Yn 3:22-26Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana, 24:2 1Kor 1:17ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake. 34:3 Yn 3:22Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.

44:4 Lk 9:52Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria. 54:5 Mwa 48:22; Yos 24:32Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu. 6Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.

74:7 Mwa 24:17; 1Fal 17:10Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.” 84:8 Yn 4:5, 30(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)

94:9 Mt 10:5; Lk 9:52-53Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)

104:10 Isa 55:1; Ufu 21:6Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”

11Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi? 124:12 Yn 4:6; 8:53Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”

134:13 Yn 6:58Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena. 144:14 Yn 6:35; Isa 12:3; Yn 7:38; Mt 25:46Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.”

154:15 Yn 6:34Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”

16Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”

17Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.”

Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume. 18Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”

194:19 Mt 21:11Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii. 204:20 Kum 11:29; Yos 8:33; Lk 9:53; 4:21; 4:20; Yn 5:28; 16:2; 1Tim 2:8Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”

214:21 Yn 5:28; 16:2; Mal 1:11; 1Tim 2:8Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu. 224:22 2Fal 17:28-41; Isa 2:3; Rum 9:4-5Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi. 234:23 Yn 5:25; 16:32; Flp 3:3Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. 244:24 Flp 3:3Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”

254:25 Mt 1:16; Yn 1:41Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”

264:26 Yn 8:24; 9:35-37Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”

274:27 Yn 4:8Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”

28Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu, 294:29 Mt 12:23; Yn 7:26, 31“Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”4:29 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 30Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.

314:31 Mt 23:7Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”

324:32 Ay 23:12; Mt 4:4Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”

33Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?” 344:34 Mt 26:39; Yn 17:4; 19:30Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake. 354:35 Mt 9:37; Lk 10:2Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa! 364:36 Rum 1:13; Mt 25:46Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. 374:37 Ay 31:8; Mik 6:15Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa. 38Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”

Wasamaria Wengi Waamini

394:39 Yn 4:29Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.” 40Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili. 41Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.

424:42 Lk 2:11; 1Yn 4:14Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”

Yesu Amponya Mwana Wa Afisa

43Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya. 444:44 Mt 13:57; Lk 4:24(Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.) 454:45 Yn 2:23Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.

464:46 Yn 21:1-11Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu. 474:47 Yn 4:3, 54; Lk 7:2Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.

484:48 Dan 4:2-3; Ebr 2:4Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”

49Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”

50Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.”

Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake. 51Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima. 52Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”

534:53 Mdo 11:14Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.

544:54 Yn 4:8; 2:11Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.

New International Version – UK

John 4:1-54

Jesus talks with a Samaritan woman

1Now Jesus learned that the Pharisees had heard that he was gaining and baptising more disciples than John – 2although in fact it was not Jesus who baptised, but his disciples. 3So he left Judea and went back once more to Galilee.

4Now he had to go through Samaria. 5So he came to a town in Samaria called Sychar, near the plot of ground Jacob had given to his son Joseph. 6Jacob’s well was there, and Jesus, tired as he was from the journey, sat down by the well. It was about noon.

7When a Samaritan woman came to draw water, Jesus said to her, ‘Will you give me a drink?’ 8(His disciples had gone into the town to buy food.)

9The Samaritan woman said to him, ‘You are a Jew and I am a Samaritan woman. How can you ask me for a drink?’ (For Jews do not associate with Samaritans.4:9 Or do not use dishes Samaritans have used)

10Jesus answered her, ‘If you knew the gift of God and who it is that asks you for a drink, you would have asked him and he would have given you living water.’

11‘Sir,’ the woman said, ‘you have nothing to draw with and the well is deep. Where can you get this living water? 12Are you greater than our father Jacob, who gave us the well and drank from it himself, as did also his sons and his livestock?’

13Jesus answered, ‘Everyone who drinks this water will be thirsty again, 14but whoever drinks the water I give them will never thirst. Indeed, the water I give them will become in them a spring of water welling up to eternal life.’

15The woman said to him, ‘Sir, give me this water so that I won’t get thirsty and have to keep coming here to draw water.’

16He told her, ‘Go, call your husband and come back.’

17‘I have no husband,’ she replied.

Jesus said to her, ‘You are right when you say you have no husband. 18The fact is, you have had five husbands, and the man you now have is not your husband. What you have just said is quite true.’

19‘Sir,’ the woman said, ‘I can see that you are a prophet. 20Our ancestors worshipped on this mountain, but you Jews claim that the place where we must worship is in Jerusalem.’

21‘Woman,’ Jesus replied, ‘believe me, a time is coming when you will worship the Father neither on this mountain nor in Jerusalem. 22You Samaritans worship what you do not know; we worship what we do know, for salvation is from the Jews. 23Yet a time is coming and has now come when the true worshippers will worship the Father in the Spirit and in truth, for they are the kind of worshippers the Father seeks. 24God is spirit, and his worshippers must worship in the Spirit and in truth.’

25The woman said, ‘I know that Messiah’ (called Christ) ‘is coming. When he comes, he will explain everything to us.’

26Then Jesus declared, ‘I, the one speaking to you – I am he.’

The disciples rejoin Jesus

27Just then his disciples returned and were surprised to find him talking with a woman. But no-one asked, ‘What do you want?’ or ‘Why are you talking with her?’

28Then, leaving her water jar, the woman went back to the town and said to the people, 29‘Come, see a man who told me everything I’ve ever done. Could this be the Messiah?’ 30They came out of the town and made their way towards him.

31Meanwhile his disciples urged him, ‘Rabbi, eat something.’

32But he said to them, ‘I have food to eat that you know nothing about.’

33Then his disciples said to each other, ‘Could someone have brought him food?’

34‘My food,’ said Jesus, ‘is to do the will of him who sent me and to finish his work. 35Don’t you have a saying, “It’s still four months until harvest”? I tell you, open your eyes and look at the fields! They are ripe for harvest. 36Even now the one who reaps draws a wage and harvests a crop for eternal life, so that the sower and the reaper may be glad together. 37Thus the saying “One sows and another reaps” is true. 38I sent you to reap what you have not worked for. Others have done the hard work, and you have reaped the benefits of their labour.’

Many Samaritans believe

39Many of the Samaritans from that town believed in him because of the woman’s testimony, ‘He told me everything I’ve ever done.’ 40So when the Samaritans came to him, they urged him to stay with them, and he stayed two days. 41And because of his words many more became believers.

42They said to the woman, ‘We no longer believe just because of what you said; now we have heard for ourselves, and we know that this man really is the Saviour of the world.’

Jesus heals an official’s son

43After the two days he left for Galilee. 44(Now Jesus himself had pointed out that a prophet has no honour in his own country.) 45When he arrived in Galilee, the Galileans welcomed him. They had seen all that he had done in Jerusalem at the Passover Festival, for they also had been there.

46Once more he visited Cana in Galilee, where he had turned the water into wine. And there was a certain royal official whose son lay ill at Capernaum. 47When this man heard that Jesus had arrived in Galilee from Judea, he went to him and begged him to come and heal his son, who was close to death.

48‘Unless you people see signs and wonders,’ Jesus told him, ‘you will never believe.’

49The royal official said, ‘Sir, come down before my child dies.’

50‘Go,’ Jesus replied, ‘your son will live.’

The man took Jesus at his word and departed. 51While he was still on the way, his servants met him with the news that his boy was living. 52When he enquired as to the time when his son got better, they said to him, ‘Yesterday, at one in the afternoon, the fever left him.’

53Then the father realised that this was the exact time at which Jesus had said to him, ‘Your son will live.’ So he and his whole household believed.

54This was the second sign Jesus performed after coming from Judea to Galilee.