Yohana 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 4:1-54

Yesu Azungumza Na Mwanamke Msamaria

14:1 Yn 3:22-26Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana, 24:2 1Kor 1:17ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake. 34:3 Yn 3:22Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.

44:4 Lk 9:52Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria. 54:5 Mwa 48:22; Yos 24:32Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu. 6Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.

74:7 Mwa 24:17; 1Fal 17:10Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.” 84:8 Yn 4:5, 30(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)

94:9 Mt 10:5; Lk 9:52-53Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)

104:10 Isa 55:1; Ufu 21:6Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”

11Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi? 124:12 Yn 4:6; 8:53Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”

134:13 Yn 6:58Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena. 144:14 Yn 6:35; Isa 12:3; Yn 7:38; Mt 25:46Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.”

154:15 Yn 6:34Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”

16Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”

17Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.”

Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume. 18Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”

194:19 Mt 21:11Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii. 204:20 Kum 11:29; Yos 8:33; Lk 9:53; 4:21; 4:20; Yn 5:28; 16:2; 1Tim 2:8Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”

214:21 Yn 5:28; 16:2; Mal 1:11; 1Tim 2:8Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu. 224:22 2Fal 17:28-41; Isa 2:3; Rum 9:4-5Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi. 234:23 Yn 5:25; 16:32; Flp 3:3Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. 244:24 Flp 3:3Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”

254:25 Mt 1:16; Yn 1:41Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”

264:26 Yn 8:24; 9:35-37Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”

274:27 Yn 4:8Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”

28Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu, 294:29 Mt 12:23; Yn 7:26, 31“Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”4:29 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 30Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.

314:31 Mt 23:7Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”

324:32 Ay 23:12; Mt 4:4Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”

33Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?” 344:34 Mt 26:39; Yn 17:4; 19:30Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake. 354:35 Mt 9:37; Lk 10:2Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa! 364:36 Rum 1:13; Mt 25:46Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. 374:37 Ay 31:8; Mik 6:15Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa. 38Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”

Wasamaria Wengi Waamini

394:39 Yn 4:29Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.” 40Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili. 41Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.

424:42 Lk 2:11; 1Yn 4:14Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”

Yesu Amponya Mwana Wa Afisa

43Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya. 444:44 Mt 13:57; Lk 4:24(Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.) 454:45 Yn 2:23Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.

464:46 Yn 21:1-11Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu. 474:47 Yn 4:3, 54; Lk 7:2Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.

484:48 Dan 4:2-3; Ebr 2:4Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”

49Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”

50Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.”

Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake. 51Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima. 52Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”

534:53 Mdo 11:14Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.

544:54 Yn 4:8; 2:11Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.

King James Version

John 4:1-54

1When therefore the Lord knew how the Pharisees had heard that Jesus made and baptized more disciples than John, 2(Though Jesus himself baptized not, but his disciples,) 3He left Judæa, and departed again into Galilee. 4And he must needs go through Samaria. 5Then cometh he to a city of Samaria, which is called Sychar, near to the parcel of ground that Jacob gave to his son Joseph. 6Now Jacob’s well was there. Jesus therefore, being wearied with his journey, sat thus on the well: and it was about the sixth hour. 7There cometh a woman of Samaria to draw water: Jesus saith unto her, Give me to drink. 8(For his disciples were gone away unto the city to buy meat.) 9Then saith the woman of Samaria unto him, How is it that thou, being a Jew, askest drink of me, which am a woman of Samaria? for the Jews have no dealings with the Samaritans. 10Jesus answered and said unto her, If thou knewest the gift of God, and who it is that saith to thee, Give me to drink; thou wouldest have asked of him, and he would have given thee living water. 11The woman saith unto him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: from whence then hast thou that living water? 12Art thou greater than our father Jacob, which gave us the well, and drank thereof himself, and his children, and his cattle? 13Jesus answered and said unto her, Whosoever drinketh of this water shall thirst again: 14But whosoever drinketh of the water that I shall give him shall never thirst; but the water that I shall give him shall be in him a well of water springing up into everlasting life. 15The woman saith unto him, Sir, give me this water, that I thirst not, neither come hither to draw. 16Jesus saith unto her, Go, call thy husband, and come hither. 17The woman answered and said, I have no husband. Jesus said unto her, Thou hast well said, I have no husband: 18For thou hast had five husbands; and he whom thou now hast is not thy husband: in that saidst thou truly. 19The woman saith unto him, Sir, I perceive that thou art a prophet. 20Our fathers worshipped in this mountain; and ye say, that in Jerusalem is the place where men ought to worship. 21Jesus saith unto her, Woman, believe me, the hour cometh, when ye shall neither in this mountain, nor yet at Jerusalem, worship the Father. 22Ye worship ye know not what: we know what we worship: for salvation is of the Jews. 23But the hour cometh, and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and in truth: for the Father seeketh such to worship him. 24God is a Spirit: and they that worship him must worship him in spirit and in truth. 25The woman saith unto him, I know that Messias cometh, which is called Christ: when he is come, he will tell us all things. 26Jesus saith unto her, I that speak unto thee am he.

27¶ And upon this came his disciples, and marvelled that he talked with the woman: yet no man said, What seekest thou? or, Why talkest thou with her? 28The woman then left her waterpot, and went her way into the city, and saith to the men, 29Come, see a man, which told me all things that ever I did: is not this the Christ? 30Then they went out of the city, and came unto him.

31¶ In the mean while his disciples prayed him, saying, Master, eat. 32But he said unto them, I have meat to eat that ye know not of. 33Therefore said the disciples one to another, Hath any man brought him ought to eat? 34Jesus saith unto them, My meat is to do the will of him that sent me, and to finish his work. 35Say not ye, There are yet four months, and then cometh harvest? behold, I say unto you, Lift up your eyes, and look on the fields; for they are white already to harvest. 36And he that reapeth receiveth wages, and gathereth fruit unto life eternal: that both he that soweth and he that reapeth may rejoice together. 37And herein is that saying true, One soweth, and another reapeth. 38I sent you to reap that whereon ye bestowed no labour: other men laboured, and ye are entered into their labours.

39¶ And many of the Samaritans of that city believed on him for the saying of the woman, which testified, He told me all that ever I did. 40So when the Samaritans were come unto him, they besought him that he would tarry with them: and he abode there two days. 41And many more believed because of his own word; 42And said unto the woman, Now we believe, not because of thy saying: for we have heard him ourselves, and know that this is indeed the Christ, the Saviour of the world.

43¶ Now after two days he departed thence, and went into Galilee. 44For Jesus himself testified, that a prophet hath no honour in his own country. 45Then when he was come into Galilee, the Galilæans received him, having seen all the things that he did at Jerusalem at the feast: for they also went unto the feast. 46So Jesus came again into Cana of Galilee, where he made the water wine. And there was a certain nobleman, whose son was sick at Capernaum. 47When he heard that Jesus was come out of Judæa into Galilee, he went unto him, and besought him that he would come down, and heal his son: for he was at the point of death. 48Then said Jesus unto him, Except ye see signs and wonders, ye will not believe. 49The nobleman saith unto him, Sir, come down ere my child die. 50Jesus saith unto him, Go thy way; thy son liveth. And the man believed the word that Jesus had spoken unto him, and he went his way. 51And as he was now going down, his servants met him, and told him, saying, Thy son liveth. 52Then enquired he of them the hour when he began to amend. And they said unto him, Yesterday at the seventh hour the fever left him. 53So the father knew that it was at the same hour, in the which Jesus said unto him, Thy son liveth: and himself believed, and his whole house. 54This is again the second miracle that Jesus did, when he was come out of Judæa into Galilee.