Yohana 4 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 4:1-54

Yesu Azungumza Na Mwanamke Msamaria

14:1 Yn 3:22-26Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana, 24:2 1Kor 1:17ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake. 34:3 Yn 3:22Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.

44:4 Lk 9:52Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria. 54:5 Mwa 48:22; Yos 24:32Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu. 6Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.

74:7 Mwa 24:17; 1Fal 17:10Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.” 84:8 Yn 4:5, 30(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)

94:9 Mt 10:5; Lk 9:52-53Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)

104:10 Isa 55:1; Ufu 21:6Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”

11Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi? 124:12 Yn 4:6; 8:53Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”

134:13 Yn 6:58Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena. 144:14 Yn 6:35; Isa 12:3; Yn 7:38; Mt 25:46Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.”

154:15 Yn 6:34Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”

16Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”

17Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.”

Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume. 18Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”

194:19 Mt 21:11Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii. 204:20 Kum 11:29; Yos 8:33; Lk 9:53; 4:21; 4:20; Yn 5:28; 16:2; 1Tim 2:8Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”

214:21 Yn 5:28; 16:2; Mal 1:11; 1Tim 2:8Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu. 224:22 2Fal 17:28-41; Isa 2:3; Rum 9:4-5Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi. 234:23 Yn 5:25; 16:32; Flp 3:3Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. 244:24 Flp 3:3Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”

254:25 Mt 1:16; Yn 1:41Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”

264:26 Yn 8:24; 9:35-37Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”

274:27 Yn 4:8Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”

28Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu, 294:29 Mt 12:23; Yn 7:26, 31“Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”4:29 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 30Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.

314:31 Mt 23:7Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”

324:32 Ay 23:12; Mt 4:4Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”

33Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?” 344:34 Mt 26:39; Yn 17:4; 19:30Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake. 354:35 Mt 9:37; Lk 10:2Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa! 364:36 Rum 1:13; Mt 25:46Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. 374:37 Ay 31:8; Mik 6:15Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa. 38Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”

Wasamaria Wengi Waamini

394:39 Yn 4:29Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.” 40Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili. 41Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.

424:42 Lk 2:11; 1Yn 4:14Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”

Yesu Amponya Mwana Wa Afisa

43Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya. 444:44 Mt 13:57; Lk 4:24(Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.) 454:45 Yn 2:23Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.

464:46 Yn 21:1-11Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu. 474:47 Yn 4:3, 54; Lk 7:2Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.

484:48 Dan 4:2-3; Ebr 2:4Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”

49Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”

50Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.”

Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake. 51Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima. 52Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”

534:53 Mdo 11:14Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.

544:54 Yn 4:8; 2:11Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.

Knijga O Kristu

Ivan 4:1-54

Isus i Samarijanka

1Kad je Gospodin saznao da su farizeji čuli kako on, Isus, krsti više učenika nego Ivan, 2iako ih nije on osobno krstio, nego učenici, 3ode iz Judeje i vrati se u pokrajinu Galileju.

4Na putu je morao proći kroz Samariju. 5Došao je do samarijskoga sela Sihara, blizu zemljišta koje je Jakov dao svojemu sinu Josipu. 6Tu se nalazio Jakovljev zdenac. Umoran od dugotrajnog hodanja, Isus je tako sjedio pokraj zdenca. Bilo je to oko podneva. 7Ubrzo zatim dođe po vodu neka Samarijanka i Isus ju zamoli: “Daj mi da se napijem!” 8Bio je sam jer su njegovi učenici otišli u grad kupiti hrane.

9“Ti si Židov, a ja Samarijanka. Kako to da od mene tražiš vode?” upita žena. Židovi se, naime, nisu družili sa Samarijancima.

10Isus odgovori: “Kad bi ti samo znala kakav ti dar nudi Bog i tko sam ja koji te tražim piti, tražila bi od mene žive vode i ja bih ti je dao.”

11“Gospodine, pa ti nemaš ni kabla ni užeta”, reče mu ona, “a zdenac je vrlo dubok. Odakle živa voda? 12Osim toga, zar si veći od našeg praoca Jakova, koji nam je dao ovaj zdenac? Kako možeš nuditi bolju vodu od ove koju su pili on i njegovi sinovi i kojom su napajali stoku?”

13Isus odgovori: “Tko god pije tu vodu, opet će ožednjeti. 14A tko pije vodu koju ću mu ja dati, nikada više neće ožednjeti. Štoviše, ta će voda u njemu postati nepresušnim izvorom koji struji u vječni život.”

15“Gospodine, molim te”, reče žena, “daj mi te vode da više nikad ne ožednim i da ne moram više ovamo dolaziti po vodu!”

16“Idi i dovedi svojeg muža, pa se vrati ovamo!” reče joj Isus.

17“Ali ja nemam muža”, odgovori žena. “Dobro si kazala: nemaš muža!” reče Isus. 18“Jer si imala pet muževa, a nisi vjenčana ni s ovim s kojim sada živiš. Istinu si rekla.”

19“Gospodine,” reče žena, “vidim da si prorok. 20Zašto vi Židovi tvrdite da se Bogu treba klanjati jedino u Jeruzalemu, kad su mu se naši preci klanjali na ovoj gori?”

21Isus joj odgovori: “Vjeruj mi, ženo, dolazi vrijeme kad više neće biti potrebno štovati Oca ni na ovoj planini ni u Jeruzalemu. 22Vi Samarijanci ne znate onoga kojemu se klanjate, a mi Židovi ga znamo jer spasenje dolazi od Židova. 23Ali dolazi vrijeme—već je stiglo—kad će se pravi klanjatelji klanjati Ocu u duhu i istini. Bog želi takve klanjatelje. 24Bog je Duh i oni koji mu se klanjaju moraju mu se klanjati u duhu i istini.”

25“Znam da će jednoga dana doći Mesija, zvani Krist—Pomazanik”, reče žena. “Kada on dođe, sve će nam objasniti.”

26Tada joj Isus reče: “Ja, koji govorim s tobom, sam Mesija.”

27Nato stignu njegovi učenici. Začude se što razgovara sa ženom, ali ga nitko ne upita: “O čemu govoriš?”, ili: “Zašto razgovaraš s njom?” 28Žena tada ostavi svoju posudu kraj zdenca pa ode u grad i svima reče: 29“Dođite vidjeti čovjeka koji mi je rekao sve što sam dosad učinila! Da to nije Krist?” 30I ljudi su dolazili iz grada da ga vide.

31U međuvremenu su ga učenici nudili: “Rabbi, jedi!” 32“Neću,” odgovarao im je, “ja imam hrane za koju vi i ne znate.”

33“Zar mu je netko već donio jelo?” pitali su učenici jedan drugoga.

34Isus im tada objasni: “Moja je hrana činiti volju onoga koji me poslao i dovršiti njegovo djelo. 35Vi kažete da rad na žetvi neće početi dok ne mine ljeto, a to je tek za četiri mjeseca. No pogledajte oko sebe! Prostrana polja bjelasaju se svuda i već su spremna za žetvu. 36Žeteoci će biti dobro plaćeni, a plod njihove žetve su ljudi koji su dobili vječni život. Kakve li radosti i za sijače i za žeteoce! 37Istinita je izreka da jedan sije, a drugi žanje. 38Ja sam vas poslao da žanjete ondje gdje se niste trudili—drugi su naporno radili, a vi ste dobili plod njihova truda.”

Obraćenje Samarijanaca

39Mnogi Samarijanci iz toga grada povjerovali su u njega zbog ženina svjedočanstva: “Rekao mi je sve što sam dosad činila!” 40Kad su Samarijanci došli k njemu, zamolili su ga da ostane kod njih. I ostao je ondje dva dana. 41Tada ih je još mnogo više povjerovalo kad su ga čuli govoriti. 42A ženi su kazali: “Sada vjerujemo jer smo ga i sami čuli, a ne zbog onoga što si nam ti ispričala. On je zaista Spasitelj svijeta!”

Isus iscjeljuje činovnikova sina

43Dva dana nakon toga Isus ode odande u Galileju. 44Sam Isus bijaše rekao da prorok nema časti u vlastitom zavičaju. 45Ali Galilejci su ga lijepo primili jer su za svetkovanja Pashe bili u Jeruzalemu i vidjeli njegova čudesna djela.

46Putujući Galilejom, stigao je u grad Kanu, gdje bijaše pretvorio vodu u vino. U gradu Kafarnaumu bio je neki kraljevski činovnik čiji je sin bio bolestan. 47Kad je čuo da je Isus došao iz Judeje i da putuje kroz Galileju, ode u Kanu te zamoli Isusa da dođe u Kafarnaum i iscijeli mu sina na samrti.

48Isus reče: “Vi zaista nećete vjerovati ne vidite li znakove i čudesa.”

49Kraljevski ga je činovnik preklinjao: “Gospodine, molim te, dođi dok mi dijete nije umrlo!”

50“Idi kući,” reče mu Isus, “sin ti je živ.” Čovjek povjeruje Isusovim riječima i uputi se doma.

51Dok je još bio na putu, susretne svoje sluge koji su nosili vijest da mu je dijete živo. 52Upita ih kada se dječak počeo osjećati bolje, a oni mu rekoše: “Jučer poslijepodne oko jedan sat groznica mu je naglo minula.” 53Otac shvati da je to bilo upravo onda kad mu je Isus rekao: “Sin ti je živ.” Činovnik i svi njegovi ukućani povjeruju u Isusa. 54Bilo je to drugo čudo koje je Isus učinio u Galileji vraćajući se iz Judeje.