Yohana 3 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 3:1-36

Nikodemo Amwendea Yesu Usiku

13:1 Yn 7:50; 19:39; Lk 23:13Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi3:1 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo Baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. lililotawala. 23:2 Yn 2:11; 9:16, 33; Mdo 2:22; 10:38Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”

33:3 Yn 1:13; 1Pet 1:23Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”

4Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”

53:5 Tit 3:5Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho. 63:6 Yn 1:13; Mwa 5:3; Za 51:5Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho. 7Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’ 83:8 Mk 4:41; Mhu 11:5Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”

93:9 Yn 6:52, 60Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”

103:10 Lk 2:46Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya? 113:11 Yn 1:18; 7:16-17Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu. 123:12 Lk 22:67Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni? 133:13 Mit 30:4; Efe 4:8-10; Ebr 4:14; 9:24Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu. 143:14 Hes 21:8-9; Yn 8:28; 12:32Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu. 153:15 Mwa 15:6; Rum 3:22Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele.

163:16 Rum 5:8; Efe 2:4; Yn 6:29, 40; 11:25-26“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. 173:17 Yn 17:8, 21; 20:21; Isa 53:11; Rum 11:14Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa. 183:18 Yn 5:24; 1:18; 1Yn 4:9Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu. 193:19 Yn 1:4; 8:12Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu. 203:20 Efe 5:11-13Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe. 21Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”

Ushuhuda Wa Yohana Mbatizaji Kuhusu Yesu

223:22 Yn 4:2Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza. 233:23 1Sam 9:4; Mt 3:6Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa. 243:24 Mt 4:12; 14:3(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani). 253:25 Yn 2:6Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso. 263:26 Mt 23:7; Yn 1:7Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”

273:27 Ebr 5:4; 1Kor 4:7; Yak 1:17Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni. 283:28 Yn 1:20-23; 3:9; Mt 9:15; Flp 2:2; 2Yn 12Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo,3:28 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. ila nimetumwa nimtangulie.’ 293:29 Mt 22:2; 2Kor 11:2; Efe 5:25, 27; Ufu 21:9; Wim 5:1Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika. 303:30 2Sam 3:1Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”

Yeye Aliyetoka Mbinguni

313:31 Yn 8:23; 1Yn 4:5“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote. 323:32 Yn 8:26; 15:15Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake. 333:33 Rum 3:4; 1Yn 5:10Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli. 343:34 Isa 42:1; Mt 12:18Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo. 353:35 Mt 28:18; Yn 17:2Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake. 363:36 Yn 5:24; 6:47Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.”

Słowo Życia

Jana 3:1-36

Jezus naucza Nikodema

1Wśród faryzeuszy był pewien człowiek imieniem Nikodem, który był żydowskim przywódcą. 2Pewnej nocy przyszedł do Jezusa i powiedział:

—Nauczycielu! Wiemy, że zostałeś posłany przez Boga, bo nikt nie mógłby czynić takich cudów, jakie Ty czynisz, gdyby On go nie posłał.

3—Zapewniam cię—rzekł Jezus—że jeśli się ktoś nie narodzi na nowo, nie ujrzy królestwa Bożego.

4—Urodzić się na nowo?—zdumiał się Nikodem. —Będąc starcem? Czy można powtórnie wejść do łona matki i urodzić się?

5—Jeszcze raz cię zapewniam—powtórzył Jezus—że jeśli człowiek nie narodzi się z wody i z Ducha, nie wejdzie do królestwa Bożego. 6Kto się narodził fizycznie, żyje tylko fizycznie. Kto się jednak narodził z Ducha, żyje także duchowo! 7Nie dziw się więc, że powiedziałem, iż trzeba się narodzić na nowo. 8Wiatr wieje, gdzie chce. Słyszysz go, ale nie wiesz, skąd i dokąd wieje. Podobnie jest z narodzeniem z Ducha—widzisz skutki, ale nie widzisz przyczyny.

9—Ale jak to się dzieje?—pytał dalej Nikodem.

10—Jesteś nauczycielem narodu i nie wiesz tego?—odparł Jezus. 11—Zapewniam cię, że mówię o tym, co dobrze znam i co sam widziałem, ale wy nie uznajecie tego. 12Jeśli nie wierzycie w to, co mówię o sprawach ziemskich, to jak uwierzycie w to, co powiem o sprawach niebiańskich? 13Nikt jednak nie wstąpił do nieba oprócz Mnie, Syna Człowieczego. Stamtąd bowiem przyszedłem. 14Podobnie jak wąż, który na pustyni został podniesiony w górę przez Mojżesza, tak i Ja, Syn Człowieczy, również muszę zostać podniesiony w górę, 15aby każdy, kto Mi uwierzy, otrzymał życie wieczne. 16Tak bowiem Bóg ukochał świat, że oddał swojego jedynego Syna, aby każdy, kto Mu uwierzy, nie zginął, ale miał życie wieczne. 17Bóg nie posłał Syna, aby potępił świat, lecz aby go zbawił. 18Ten, kto Mu wierzy, nie podlega potępieniu. Ale ten, kto Mu nie wierzy, już został osądzony, bo nie uwierzył jedynemu Synowi Bożemu. 19Wyrok taki zapadł dlatego, że chociaż na świat przyszło światło, ludzie bardziej pokochali ciemność, bo ich czyny były złe. 20Ten, kto czyni zło, nienawidzi światła i nie zbliża się do niego, aby nie wyszły na jaw jego czyny. 21Kto zaś postępuje zgodnie z prawdą, zbliża się do światła, aby ujawniły się jego czyny, które podobają się Bogu.

Wyznanie Jana Chrzciciela o Jezusie

22Jakiś czas później Jezus wraz z uczniami udał się na tereny Judei. Zatrzymał się tam i udzielał ludziom chrztu. 23Niedaleko Salim, w Ainon, przebywał również Jan Chrzciciel. On także chrzcił, bo w tych okolicach było dużo wody i wielu ludzi przychodziło do niego, aby ich w niej zanurzył. 24W tym czasie Jan był bowiem jeszcze na wolności.

25Pewnego dnia ktoś posprzeczał się z uczniami Jana o sprawy dotyczące rytualnych oczyszczeń. 26Przyszli więc do Jana i zapytali:

—Nauczycielu! Ten, którego spotkałeś na drugim brzegu Jordanu i o którym powiedziałeś, że jest Mesjaszem, także chrzci i teraz wszyscy idą do Niego.

27—Nikt nie może wziąć czegoś, czego nie otrzymał z nieba—odpowiedział Jan. 28—Sami możecie potwierdzić, że powiedziałem: „Nie jestem Mesjaszem. Zostałem tylko wysłany przed Nim”. 29Panna młoda należy przecież do pana młodego. A przyjaciel pana młodego cieszy się z tego, że może przy nim stać i słuchać go. Obecnie w całej pełni doświadczam takiej właśnie radości. 30Teraz On będzie się stawał coraz ważniejszy, ja zaś muszę schodzić ze sceny. 31Ten, kto przychodzi z góry, przewyższa wszystkich. Ten zaś, kto pochodzi z ziemi, jest ograniczony do rzeczy ziemskich. 32Ten, kto przybywa z nieba, mówi o tym, co widział i słyszał w niebie. Ludzie nie chcą Go słuchać, 33ci jednak, którzy Mu uwierzyli, uznali, że Bóg mówi prawdę. 34Ten bowiem, kto został wysłany przez Boga, przemawia w Jego imieniu. A Bóg w pełni obdarza Go swoim Duchem. 35Ojciec kocha Syna i wszystko Mu powierzył. 36Ten, kto wierzy Synowi Bożemu, ma życie wieczne. Ten zaś, kto Mu nie wierzy, nawet nie ujrzy tego życia—przeciwnie: zobaczy gniew Boga.