Yohana 3 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 3:1-36

Nikodemo Amwendea Yesu Usiku

13:1 Yn 7:50; 19:39; Lk 23:13Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi3:1 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo Baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. lililotawala. 23:2 Yn 2:11; 9:16, 33; Mdo 2:22; 10:38Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”

33:3 Yn 1:13; 1Pet 1:23Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”

4Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”

53:5 Tit 3:5Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho. 63:6 Yn 1:13; Mwa 5:3; Za 51:5Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho. 7Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’ 83:8 Mk 4:41; Mhu 11:5Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”

93:9 Yn 6:52, 60Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”

103:10 Lk 2:46Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya? 113:11 Yn 1:18; 7:16-17Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu. 123:12 Lk 22:67Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni? 133:13 Mit 30:4; Efe 4:8-10; Ebr 4:14; 9:24Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu. 143:14 Hes 21:8-9; Yn 8:28; 12:32Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu. 153:15 Mwa 15:6; Rum 3:22Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele.

163:16 Rum 5:8; Efe 2:4; Yn 6:29, 40; 11:25-26“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. 173:17 Yn 17:8, 21; 20:21; Isa 53:11; Rum 11:14Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa. 183:18 Yn 5:24; 1:18; 1Yn 4:9Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu. 193:19 Yn 1:4; 8:12Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu. 203:20 Efe 5:11-13Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe. 21Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”

Ushuhuda Wa Yohana Mbatizaji Kuhusu Yesu

223:22 Yn 4:2Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza. 233:23 1Sam 9:4; Mt 3:6Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa. 243:24 Mt 4:12; 14:3(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani). 253:25 Yn 2:6Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso. 263:26 Mt 23:7; Yn 1:7Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”

273:27 Ebr 5:4; 1Kor 4:7; Yak 1:17Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni. 283:28 Yn 1:20-23; 3:9; Mt 9:15; Flp 2:2; 2Yn 12Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo,3:28 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. ila nimetumwa nimtangulie.’ 293:29 Mt 22:2; 2Kor 11:2; Efe 5:25, 27; Ufu 21:9; Wim 5:1Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika. 303:30 2Sam 3:1Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”

Yeye Aliyetoka Mbinguni

313:31 Yn 8:23; 1Yn 4:5“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote. 323:32 Yn 8:26; 15:15Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake. 333:33 Rum 3:4; 1Yn 5:10Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli. 343:34 Isa 42:1; Mt 12:18Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo. 353:35 Mt 28:18; Yn 17:2Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake. 363:36 Yn 5:24; 6:47Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.”

Slovo na cestu

Jan 3:1-36

Nikodém navštěvuje v noci Ježíše

1Jedním z předních Židů byl Nikodém, člen nejvyšší židovské rady. Patřil do skupiny farizejů, kteří přísně dodržovali všechny náboženské předpisy. 2Ten jedné noci vyhledal Ježíše a řekl mu: „Mistře, víme, že jsi učitel poslaný od Boha. Kdyby za tebou nestál sám Bůh, nemohl bys dělat takové zázraky, jaké jsi nám ukázal.“ 3Ježíš mu řekl: „Víš, na čem záleží? Na tom, aby se člověk znovu narodil, protože jinak se nestane občanem Božího království.“ 4„Znovu se narodit v mém věku?“ podivil se Nikodém. „Cožpak se někdo může vrátit do matčina těla a narodit se podruhé?“

5Ježíš vysvětloval: „Jestliže se s člověkem nestane zásadní proměna a není na něm patrný nový život z Ducha a jestliže není na znamení toho pokřtěn, nemůže vstoupit do Božího království. 6Život zrozený z člověka je tělesný. Teprve Boží Duch v člověku probouzí duchovní život. 7Nediv se mým slovům, že se musíte znovu narodit. 8Ovšem s Duchem svatým je to jako s větrem: Nemůžeš ho ovládat, ale pozoruješ jeho účinky. Tak se člověk znovu narodí z Ducha.“ 9Nikodém se zeptal: „Jak toho všeho dosáhnu?“

10„Jsi učitelem Božího národa a toto nevíš?“ podivil se Ježíš. 11„Věř mi, že mluvím o tom, co vím, a svědčím o tom, co jsem viděl. Vy ovšem moje slova neberete vážně. 12Když nechápete to, co se týká člověka, jak porozumíte tomu, co se týká Boha? 13Nikdo z lidí vám nemůže podat svědectví jako já, vždyť jsem přišel od Boha. 14Vzpomínáš si, co Izraelcům zachránilo život na poušti, kde je ohrožovali jedovatí hadi? Jak Mojžíš vyzvedl na sloup bronzového hada, a kdo na něj pohlédl s vírou, zachránil si život? Tak i já musím být vyzdvižen na kříž.

15Každý, kdo ve mne uvěří, ujde smrti a narodí se pro věčnost. 16Vždyť Bůh tak miloval svět, že dal svého jediného Syna, aby každý, kdo v něho uvěří, unikl záhubě a získal věčný život. 17Bůh svého Syna neposlal proto, aby svět odsoudil, ale zachránil. 18Kdo v něho věří, unikne odsouzení. Kdo však v něho nevěří, odsuzuje sám sebe, protože odmítá milost nabízenou samým Bohem. 19Pro takové lidi je osudné, že na svět přišlo světlo, ale oni se nechtějí vzdát tmy, protože doufají, že ta zakryje jejich viny. 20Zlé činy dělá člověk potmě, aby to nikdo nevěděl. Bojí se světla, aby nebyl odhalen. 21Kdo se však řídí Boží pravdou, tíhne ke světlu, aby věděl, zda jsou jeho činy v souladu s Boží vůlí.“

Jan Křtitel znovu představuje Ježíše

22Potom Ježíš odešel se svými učedníky na judský venkov, aby tam s nimi mohl v klidu pobývat a aby křtil.

23-24Také Jan Křtitel, který byl v té době ještě na svobodě, křtil v Ainonu nedaleko Salimu, kde bylo mnoho vody. Četní lidé se tam dali od Jana pokřtít. 25Někteří Židé se dohadovali s Janovými učedníky, kdo má právo křtít. 26Ti se obrátili na svého učitele: „Mistře, ten, kterého jsi označil za Mesiáše, také křtí a všichni teď chodí k němu.“

27Jan jim řekl: „Člověk sám si nemůže přisvojit žádnou duchovní moc, pokud mu není dána od Boha. 28Vy sami jste svědky, že jsem prohlásil: ‚On je Bohem poslaný Mesiáš a já mu jen připravuji cestu.‘ 29-30Nevěsta přece patří ženichovi. Jeho přítel je také na svatbě, ale raduje se z ženichova štěstí. To je právě moje radost. Jeho hvězda vychází a já chci, aby jasně zářila, a nechci jí zaclánět. 31Protože Ježíš přišel z nebe, převyšuje nás všechny. My lidé mluvíme jen o tom, co jsme prožili na zemi. 32On svědčí o tom, co viděl v nebi, a přece ho tak málo lidí přijímá. 33Kdo mu uvěří, dává za pravdu Bohu. Ježíš totiž mluví Boží slova z Božího pověření. 34Bůh jej k tomu také plně uschopnil svým Duchem. 35Vždyť Otec miluje Syna a svěřuje mu všechno. 36Proto, kdo věří Synu, má věčný život. Kdo mu nedůvěřuje, místo života ho stíhá Boží hněv.“