Yohana 3 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 3:1-36

Nikodemo Amwendea Yesu Usiku

13:1 Yn 7:50; 19:39; Lk 23:13Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi3:1 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo Baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. lililotawala. 23:2 Yn 2:11; 9:16, 33; Mdo 2:22; 10:38Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”

33:3 Yn 1:13; 1Pet 1:23Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”

4Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”

53:5 Tit 3:5Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho. 63:6 Yn 1:13; Mwa 5:3; Za 51:5Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho. 7Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’ 83:8 Mk 4:41; Mhu 11:5Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”

93:9 Yn 6:52, 60Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”

103:10 Lk 2:46Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya? 113:11 Yn 1:18; 7:16-17Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu. 123:12 Lk 22:67Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni? 133:13 Mit 30:4; Efe 4:8-10; Ebr 4:14; 9:24Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu. 143:14 Hes 21:8-9; Yn 8:28; 12:32Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu. 153:15 Mwa 15:6; Rum 3:22Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele.

163:16 Rum 5:8; Efe 2:4; Yn 6:29, 40; 11:25-26“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. 173:17 Yn 17:8, 21; 20:21; Isa 53:11; Rum 11:14Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa. 183:18 Yn 5:24; 1:18; 1Yn 4:9Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu. 193:19 Yn 1:4; 8:12Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu. 203:20 Efe 5:11-13Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe. 21Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”

Ushuhuda Wa Yohana Mbatizaji Kuhusu Yesu

223:22 Yn 4:2Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza. 233:23 1Sam 9:4; Mt 3:6Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa. 243:24 Mt 4:12; 14:3(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani). 253:25 Yn 2:6Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso. 263:26 Mt 23:7; Yn 1:7Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”

273:27 Ebr 5:4; 1Kor 4:7; Yak 1:17Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni. 283:28 Yn 1:20-23; 3:9; Mt 9:15; Flp 2:2; 2Yn 12Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo,3:28 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. ila nimetumwa nimtangulie.’ 293:29 Mt 22:2; 2Kor 11:2; Efe 5:25, 27; Ufu 21:9; Wim 5:1Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika. 303:30 2Sam 3:1Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”

Yeye Aliyetoka Mbinguni

313:31 Yn 8:23; 1Yn 4:5“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote. 323:32 Yn 8:26; 15:15Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake. 333:33 Rum 3:4; 1Yn 5:10Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli. 343:34 Isa 42:1; Mt 12:18Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo. 353:35 Mt 28:18; Yn 17:2Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake. 363:36 Yn 5:24; 6:47Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.”

New International Version

John 3:1-36

Jesus Teaches Nicodemus

1Now there was a Pharisee, a man named Nicodemus who was a member of the Jewish ruling council. 2He came to Jesus at night and said, “Rabbi, we know that you are a teacher who has come from God. For no one could perform the signs you are doing if God were not with him.”

3Jesus replied, “Very truly I tell you, no one can see the kingdom of God unless they are born again.3:3 The Greek for again also means from above; also in verse 7.

4“How can someone be born when they are old?” Nicodemus asked. “Surely they cannot enter a second time into their mother’s womb to be born!”

5Jesus answered, “Very truly I tell you, no one can enter the kingdom of God unless they are born of water and the Spirit. 6Flesh gives birth to flesh, but the Spirit3:6 Or but spirit gives birth to spirit. 7You should not be surprised at my saying, ‘You3:7 The Greek is plural. must be born again.’ 8The wind blows wherever it pleases. You hear its sound, but you cannot tell where it comes from or where it is going. So it is with everyone born of the Spirit.”3:8 The Greek for Spirit is the same as that for wind.

9“How can this be?” Nicodemus asked.

10“You are Israel’s teacher,” said Jesus, “and do you not understand these things? 11Very truly I tell you, we speak of what we know, and we testify to what we have seen, but still you people do not accept our testimony. 12I have spoken to you of earthly things and you do not believe; how then will you believe if I speak of heavenly things? 13No one has ever gone into heaven except the one who came from heaven—the Son of Man.3:13 Some manuscripts Man, who is in heaven 14Just as Moses lifted up the snake in the wilderness, so the Son of Man must be lifted up,3:14 The Greek for lifted up also means exalted. 15that everyone who believes may have eternal life in him.”3:15 Some interpreters end the quotation with verse 21.

16For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life. 17For God did not send his Son into the world to condemn the world, but to save the world through him. 18Whoever believes in him is not condemned, but whoever does not believe stands condemned already because they have not believed in the name of God’s one and only Son. 19This is the verdict: Light has come into the world, but people loved darkness instead of light because their deeds were evil. 20Everyone who does evil hates the light, and will not come into the light for fear that their deeds will be exposed. 21But whoever lives by the truth comes into the light, so that it may be seen plainly that what they have done has been done in the sight of God.

John Testifies Again About Jesus

22After this, Jesus and his disciples went out into the Judean countryside, where he spent some time with them, and baptized. 23Now John also was baptizing at Aenon near Salim, because there was plenty of water, and people were coming and being baptized. 24(This was before John was put in prison.) 25An argument developed between some of John’s disciples and a certain Jew over the matter of ceremonial washing. 26They came to John and said to him, “Rabbi, that man who was with you on the other side of the Jordan—the one you testified about—look, he is baptizing, and everyone is going to him.”

27To this John replied, “A person can receive only what is given them from heaven. 28You yourselves can testify that I said, ‘I am not the Messiah but am sent ahead of him.’ 29The bride belongs to the bridegroom. The friend who attends the bridegroom waits and listens for him, and is full of joy when he hears the bridegroom’s voice. That joy is mine, and it is now complete. 30He must become greater; I must become less.”3:30 Some interpreters end the quotation with verse 36.

31The one who comes from above is above all; the one who is from the earth belongs to the earth, and speaks as one from the earth. The one who comes from heaven is above all. 32He testifies to what he has seen and heard, but no one accepts his testimony. 33Whoever has accepted it has certified that God is truthful. 34For the one whom God has sent speaks the words of God, for God3:34 Greek he gives the Spirit without limit. 35The Father loves the Son and has placed everything in his hands. 36Whoever believes in the Son has eternal life, but whoever rejects the Son will not see life, for God’s wrath remains on them.