Yohana 2 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 2:1-25

Arusi Huko Kana

12:1 Yn 4:46; 21:2; Mt 12:46Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale. 2Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia. 3Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”

42:4 Yn 19:26; Mt 8:26; 26:18; Yn 7:6Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”

52:5 Mwa 41:55Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”

62:6 Mk 7:3-4; Yn 3:25Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.2:6 Kipipa kimoja chenye ujazo wa lita 40; hivyo kila mtungi ulikuwa na ujazo wa lita 80 au 120.

7Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.

8Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.”

Hivyo wakachota, wakampelekea. 92:9 Yn 4:46Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando 10akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”

112:11 Mt 12:38; Yn 1:14; Kut 14:31Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.

Yesu Atakasa Hekalu

(Mathayo 21:12-13; Marko 11:15-17; Luka 19:45-46)

12Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.

132:13 Yn 11:55; Kum 16:1-6; Lk 2:41Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu. 142:14 Mt 21:12; Mk 11:15; Lk 19:452:14 Mt 21:12, 13; Mk 11:15-17; Lk 19:45, 46Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha. 15Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao. 162:16 Lk 2:49Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”

172:17 Za 69; 9Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”

182:18 Mt 12:38Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”

192:19 Mt 26:61; Mdo 6:14Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”

20Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?” 212:21 1Kor 6:19Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake. 222:22 Lk 24:5-8; Yn 14:26Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.

232:23 Yn 3:15Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake. 24Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote. 252:25 Kum 31:21; Mt 9:4Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.

New International Reader’s Version

John 2:1-25

Jesus Changes Water Into Wine

1On the third day there was a wedding. It took place at Cana in Galilee. Jesus’ mother was there. 2Jesus and his disciples had also been invited to the wedding. 3When the wine was gone, Jesus’ mother said to him, “They have no more wine.”

4“Dear woman, why are you telling me about this?” Jesus replied. “The time for me to show who I really am isn’t here yet.”

5His mother said to the servants, “Do what he tells you.”

6Six stone water jars stood nearby. The Jews used water from that kind of jar for special washings. They did that to make themselves pure and “clean.” Each jar could hold 20 to 30 gallons.

7Jesus said to the servants, “Fill the jars with water.” So they filled them to the top.

8Then he told them, “Now dip some out. Take it to the person in charge of the dinner.”

They did what he said. 9The person in charge tasted the water that had been turned into wine. He didn’t realize where it had come from. But the servants who had brought the water knew. Then the person in charge called the groom to one side. 10He said to him, “Everyone brings out the best wine first. They bring out the cheaper wine after the guests have had too much to drink. But you have saved the best until now.”

11What Jesus did here in Cana in Galilee was the first of his signs. Jesus showed his glory by doing this sign. And his disciples believed in him.

12After this, Jesus went down to Capernaum. His mother and brothers and disciples went with him. They all stayed there for a few days.

Jesus Clears Out the Temple Courtyard

13It was almost time for the Jewish Passover Feast. So Jesus went up to Jerusalem. 14In the temple courtyard he found people selling cattle, sheep and doves. Others were sitting at tables exchanging money. 15So Jesus made a whip out of ropes. He chased all the sheep and cattle from the temple courtyard. He scattered the coins of the people exchanging money. And he turned over their tables. 16He told those who were selling doves, “Get these out of here! Stop turning my Father’s house into a market!” 17His disciples remembered what had been written. It says, “My great love for your house will destroy me.” (Psalm 69:9)

18Then the Jewish leaders asked him, “What sign can you show us to prove your authority to do this?”

19Jesus answered them, “When you destroy this temple, I will raise it up again in three days.”

20They replied, “It has taken 46 years to build this temple. Are you going to raise it up in three days?” 21But the temple Jesus had spoken about was his body. 22His disciples later remembered what he had said. That was after he had been raised from the dead. Then they believed the Scripture. They also believed the words that Jesus had spoken.

23Meanwhile, he was in Jerusalem at the Passover Feast. Many people saw the signs he was doing. And they believed in his name. 24But Jesus did not fully trust them. He knew what people are like. 25He didn’t need anyone to tell him what people are like. He already knew why people do what they do.