Yohana 15 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 15:1-27

Yesu Mzabibu Wa Kweli

115:1 Za 80:8-11“Mimi ndimi mzabibu wa kweli na Baba yangu ndiye mkulima. 215:2 Mt 3:10; Za 92:14; Mt 3:8; 7:20; Gal 5:22; Efe 5:9; Flp 1:11; Yn 16:6Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, Baba yangu hulikata, nalo kila tawi lizaalo, hulisafisha ili lipate kuzaa matunda zaidi. 315:3 Yn 17:17; Efe 5:26Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililonena nanyi. 415:4 Yn 6:56; 2:6Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda lisipokaa ndani ya mzabibu, vivyo hivyo ninyi msipokaa ndani yangu hamwezi kuzaa matunda.

515:5 1Kor 12:12, 27; 2Kor 3:5“Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa sana, maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya jambo lolote. 615:6 Mt 3:10; 13:40; Eze 15:4; Yn 15:2Mtu yeyote asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka. Matawi kama hayo hukusanywa na kutupwa motoni, yakateketea. 715:7 Mk 11:24; Yn 6:56; Mt 7:7Ninyi mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni lolote mtakalo, nanyi mtatendewa. 815:8 Mt 5:16; Yn 8:31Kwa hiyo Baba yangu hutukuzwa, kwa vile mzaavyo matunda mengi, nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.

915:9 Yn 17:23, 24, 26“Kama vile Baba alivyonipenda mimi, hivyo ndivyo mimi nilivyowapenda ninyi. Basi kaeni katika pendo langu. 1015:10 Yn 14:15Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. 1115:11 Yn 3:29Nimewaambia mambo haya ili furaha yangu iwe ndani yenu na furaha yenu iwe kamili. 1215:12 Yn 13:34; 1Yn 3:11; Mk 12:30Amri yangu ndiyo hii: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi. 1315:13 Mwa 44:33; Rum 5:7, 8Hakuna mtu mwenye upendo mkuu kuliko huu, mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. 1415:14 Mit 18:24; Mt 12:50Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru. 1515:15 Yn 8:26Siwaiti ninyi watumishi tena, kwa sababu watumishi hawajui bwana wao analofanya, bali nimewaita ninyi rafiki, kwa maana nimewajulisha mambo yote niliyoyasikia kutoka kwa Baba yangu. 1615:16 Yn 6:70; 13:18Si ninyi mlionichagua, bali mimi ndiye niliyewachagua ninyi na kuwaweka mwende mkazae matunda, na matunda yenu yapate kudumu. Ili nalo lolote mtakalomwomba Baba katika Jina langu, awape ninyi. 1715:17 Yn 15:12Amri yangu ndiyo hii: Mpendane.

Ulimwengu Wawachukia Wanafunzi

1815:18 Isa 66:5“Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba ulinichukia mimi kabla yenu. 1915:19 Yn 15:16; 17:14Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungeliwapenda kama vile unavyowapenda walio wake. Kwa sababu ninyi si wa ulimwengu, lakini mimi nimewachagua kutoka ulimwengu, hii ndiyo sababu ulimwengu unawachukia. 2015:20 Yn 13:16; 2Tim 3:12Kumbukeni lile neno nililowaambia, ‘Hakuna mtumishi aliye mkuu kuliko bwana wake.’ Kama wamenitesa mimi, nanyi pia watawatesa. Kama wamelishika neno langu, watalishika na neno lenu pia. 2115:21 Isa 66:5; Yn 16:3Watawatendea ninyi haya yote kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu hawamjui yeye aliyenituma. 2215:22 Rum 1:20; 2:1Kama sikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa hawana udhuru kwa ajili ya dhambi zao. 2315:23 1Yn 2:23Yeyote anayenichukia mimi, anamchukia pia na Baba yangu. 2415:24 Yn 5:36Kama sikuwa nimefanya miujiza ambayo haijapata kufanywa na mtu mwingine yeyote, wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa wameiona miujiza hii na bado wakatuchukia mimi na Baba yangu. 2515:25 Za 69:4; 109:3Lakini hii ni kutimiza lile neno lililoandikwa kwenye Sheria kwamba, ‘Walinichukia pasipo sababu.’

2615:26 Yn 14:15; 16:7; 14:17; 1Yn 4:4“Lakini atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, yaani, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi. 2715:27 Lk 24:48; 1:21; 1Yn 4:14Ninyi nanyi itawapasa kushuhudia kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

הבשורה על-פי יוחנן 15:1-27

1”אני הגפן האמתית ואבי הוא הכורם. 2הוא גוזם את כל הענפים שאינם נושאים פרי, ומטהר את הענפים שנושאים פרי, כדי שישאו יותר פרי. 3אתם כבר מטוהרים על־ידי הדברים שאמרתי לכם. 4עליכם לקשור את חייכם בחיי. אם לא תהיו חלק ממני, לא תוכלו לשאת פרי, כשם שענף גזום אינו מסוגל לשאת פרי מעצמו.

5”כן, אני הגפן ואתם הענפים. מי שמחובר אלי ואני אליו ישא פרי רב, כי בלעדי אינכם מסוגלים לעשות דבר. 6מי שיאנו מחובר אלי ייזרק החוצה כענף יבש וחסר־תועלת שנועד לשריפה. 7אולם אם תקשרו את חייכם בחיי ותשמרו את מצוותי, אתן לכם כל מה שתבקשו ממני, 8ואבי יכובד בעשותכם פרי ובהיותכם תלמידי.

9”אני אוהב אתכם כפי שאבי אוהב אותי; דבקו באהבתי! 10אם תשמרו את מצוותי תעמדו באהבתי, כשם שאני שומר את מצוות אבי ועומד באהבתו. 11אני מספר לכם דברים אלה כדי שתימלאו בשמחתי, וכדי ששמחתכם תהיה מושלמת. 12אני דורש מכם שתאהבו איש את רעהו כשם שאני אוהב אתכם. 13האהבה הגדולה ביותר היא זו של אדם שמקריב את נפשו בעד ידידיו; 14ואם תשמעו בקולי תהיו ידידי. 15לא אקרא לכם יותר ’עבדים‘, כי האדון אינו משתף את עבדיו בסודותיו; עתה הנכם ידידי ואנשי־סודי, כי סיפרתי לכם כל מה שאמר לי אבי.

16”לא אתם בחרתם בי, כי אם אני בחרתי בכם ושלחתי אתכם ללכת ולעשות פרי מבורך ואמתי, כדי שאבי יתן לכם כל מה שתבקשו ממנו בשמי. 17אני מצווה עליכם לאהוב איש את רעהו. 18העולם אמנם שונא אתכם, אולם דעו לכם שהוא שנא אותי לפני ששנא אתכם. 19אילו הייתם שייכים לעולם, היה העולם אוהב אתכם; אולם אינכם שייכים לעולם, כי אני בחרתי להוציא אתכם ממנו, ומשום כך הוא שונא אתכם. 20האם אתם זוכרים מה שאמרתי לכם? ’העבד אינו גדול מאדוניו‘, וכך הם רודפים אתכם משום שרדפו אותי; אילו הקשיבו לי, היו מקשיבים גם לכם. 21האנשים בעולם ירדפו אתכם משום שאתם שייכים לי, ומשום שהם לא מכירים את האלוהים אשר שלח אותי.

22”לולא דיברתי אליהם הם לא היו אשמים, אולם עתה אין להם כל תירוץ להמשיך בחטאיהם. 23כל השונא אותי שונא גם את אבי. 24לולא עשיתי לפניהם את כל הניסים והנפלאות הם גם לא היו אשמים; אולם הם ראו את הניסים והנפלאות, ובכל זאת הם שונאים אותי ואת אבי. 25כך מתקיימים הדברים בתורה שלהם שמתייחסים למשיח: ’שנאת חינם שנאוני‘.

26”אולם אני אשלח לכם את המנחם – את רוח הקודש שהוא מקור האמת. הוא יבוא אליכם מאת האב ללמד אתכם ולזהכיר לכם את כל מה שאמרתי לכם. 27גם עליכם מוטל לספר לכולם על אודותי, משום שהייתם איתי מלכתחילה.“