Yohana 12 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 12:1-50

Maria Ampaka Yesu Mafuta Huko Bethania

(Mathayo 26:6-13; Marko 14:3-9)

112:1 Yn 11:55; Mt 21:17Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi. 212:2 Lk 10:38-42Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu. 312:3 Yn 11:12Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja12:3 Painti moja ni kama nusu lita. yenye manukato ya nardo12:3 Nardo ni aina ya mafuta yaliyokuwa yanatengenezwa kutokana na mimea yenye mizizi inayotoa harufu nzuri. safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.

412:4 Mt 10:4Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema, 5“Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 30012:5 Dinari 300 ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku 300. na fedha hizo wakapewa maskini?” 612:6 Yn 13:29Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.

712:7 Yn 19:40Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu. 812:8 Kum 15:11Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”

Shauri La Kumuua Lazaro

912:9 Yn 11:43, 44Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua. 1012:10 Lk 16:31Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia, 1112:11 Yn 11:45; 12:18kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.

Kuingia Kwa Yesu Yerusalemu Kwa Ushindi

(Mathayo 21:1-11; Marko 1:1-11; Luka 19:28-40)

1212:12 Mt 21:8; Mk 11:8; Lk 19:35, 36Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu. 1312:13 Za 118:25-26; Yn 1:49Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema,

“Hosana!”12:13 Kiebrania kusema Okoa, basi likawa neno la shangwe.

“Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!”

“Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”

1412:14 Mt 21:7Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,

1512:15 Zek 9:9“Usiogope, Ewe binti Sayuni;

tazama, Mfalme wako anakuja,

amepanda mwana-punda!”

1612:16 Lk 18:34; Yn 7:39Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.

1712:17 Yn 11:42Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia. 1812:18 Yn 12:11; 19:37Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki. 1912:19 Yn 11:47, 48Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”

Yesu Anatabiri Kifo Chake

2012:20 Yn 7:35; Mdo 11:20Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu. 2112:21 Mt 11:21; Yn 1:44Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.” 22Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.

2312:23 Yn 13:32; 17:1Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa. 2412:24 1Kor 15:36Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi. 2512:25 Mk 8:35; Lk 14:26Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. 2612:26 Flp 1:23Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.

2712:27 Mt 26:38, 39; Lk 12:50; Yn 13:21; Lk 22:53; Yn 18:37“Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu. 2812:28 Mt 3:17Baba, litukuze jina lako.”

Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.” 2912:29 Lk 22:43Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”

3012:30 Kut 19:9Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu. 3112:31 Yn 16; 11; Efe 2:2; 1Yn 5:19Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje. 3212:32 Isa 11:10; Yn 3:14; 6:44Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.” 3312:33 Yn 18:32; 21:19Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.

3412:34 Za 110:4; Isa 9:7; Mt 8:20; Yn 3:14Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo12:34 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?”

3512:35 Yn 1:9; 8:12; 9:5; Yer 13:16; Efe 5:8; 1Yn 2:11Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda. 3612:36 Lk 16:8; Efe 5:8; 1The 5:5; 1Yn 2:9, 10, 11; Yn 8:59; 11:54Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.

Wayahudi Waendelea Kutokuamini

3712:37 Yn 2:11Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini. 3812:38 Isa 53:1; Rum 10:16Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema:

“Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu,

na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”

3912:39 Isa 6:9, 10; Mt 13:14, 15Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:

4012:40 Isa 6:10; Mt 13:13, 15“Amewafanya vipofu,

na kuifanya mioyo yao kuwa migumu,

ili wasiweze kuona kwa macho yao,

wala kuelewa kwa mioyo yao,

wasije wakageuka nami nikawaponya.”

4112:41 Isa 6:1-4; Lk 24:27Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.

4212:42 Yn 7:48; 9:22Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi. 4312:43 Yn 5:44; Rum 2:29Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.

Amwaminiye Yesu Hatabaki Gizani

4412:44 Mt 10:40; Yn 5:24Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma. 4512:45 Yn 14:9Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma. 4612:46 Yn 3:19; 8:12Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.

4712:47 Yn 3:17“Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa. 4812:48 Yn 5:45Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho. 4912:49 Yn 14:31Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema. 5012:50 Yn 8:26, 28Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.”

Nova Versão Internacional

João 12:1-50

Jesus é Ungido em Betânia

(Mt 26.6-13; Mc 14.3-9)

1Seis dias antes da Páscoa Jesus chegou a Betânia, onde vivia Lázaro, a quem ressuscitara dos mortos. 2Ali prepararam um jantar para Jesus. Marta servia, enquanto Lázaro estava à mesa com ele. 3Então Maria pegou um frasco12.3 Grego: 1 litra. A litra era uma medida de capacidade de cerca de um terço de litro. de nardo puro, que era um perfume caro, derramou-o sobre os pés de Jesus e os enxugou com os seus cabelos. E a casa encheu-se com a fragrância do perfume.

4Mas um dos seus discípulos, Judas Iscariotes, que mais tarde iria traí-lo, fez uma objeção: 5“Por que este perfume não foi vendido, e o dinheiro dado aos pobres? Seriam trezentos denários12.5 O denário era uma moeda de prata equivalente à diária de um trabalhador braçal.”. 6Ele não falou isso por se interessar pelos pobres, mas porque era ladrão; sendo responsável pela bolsa de dinheiro, costumava tirar o que nela era colocado.

7Respondeu Jesus: “Deixe-a em paz; que o guarde para o dia do meu sepultamento. 8Pois os pobres vocês sempre terão consigo, mas a mim vocês nem sempre terão”.

9Enquanto isso, uma grande multidão de judeus, ao descobrir que Jesus estava ali, veio, não apenas por causa de Jesus, mas também para ver Lázaro, a quem ele ressuscitara dos mortos. 10Assim, os chefes dos sacerdotes fizeram planos para matar também Lázaro, 11pois por causa dele muitos estavam se afastando dos judeus e crendo em Jesus.

A Entrada Triunfal

(Mt 21.1-11; Mc 11.1-11; Lc 19.28-40)

12No dia seguinte, a grande multidão que tinha vindo para a festa ouviu falar que Jesus estava chegando a Jerusalém. 13Pegaram ramos de palmeiras e saíram ao seu encontro, gritando:

“Hosana!12.13 Expressão hebraica que significa “Salve!”, e que se tornou exclamação de louvor.

“Bendito é o que vem em nome do Senhor!”12.13 Sl 118.25,26

“Bendito é o Rei de Israel!”

14Jesus conseguiu um jumentinho e montou nele, como está escrito:

15“Não tenha medo, ó cidade12.15 Grego: filha. de Sião;

eis que o seu rei vem,

montado num jumentinho”12.15 Zc 9.9.

16A princípio seus discípulos não entenderam isso. Só depois que Jesus foi glorificado, eles se lembraram de que essas coisas estavam escritas a respeito dele e lhe foram feitas.

17A multidão que estava com ele, quando mandara Lázaro sair do sepulcro e o ressuscitara dos mortos, continuou a espalhar o fato. 18Muitas pessoas, por terem ouvido falar que ele realizara tal sinal milagroso, foram ao seu encontro. 19E assim os fariseus disseram uns aos outros: “Não conseguimos nada. Olhem como o mundo todo vai atrás dele!”

Jesus Prediz sua Morte

20Entre os que tinham ido adorar a Deus na festa da Páscoa, estavam alguns gregos. 21Eles se aproximaram de Filipe, que era de Betsaida da Galileia, com um pedido: “Senhor, queremos ver Jesus”. 22Filipe foi dizê-lo a André, e os dois juntos o disseram a Jesus.

23Jesus respondeu: “Chegou a hora de ser glorificado o Filho do homem. 24Digo verdadeiramente que, se o grão de trigo não cair na terra e não morrer, continuará ele só. Mas, se morrer, dará muito fruto. 25Aquele que ama a sua vida a perderá; ao passo que aquele que odeia a sua vida neste mundo a conservará para a vida eterna. 26Quem me serve precisa seguir-me; e, onde estou, o meu servo também estará. Aquele que me serve, meu Pai o honrará.

27“Agora meu coração está perturbado, e o que direi? Pai, salva-me desta hora? Não; eu vim exatamente para isto, para esta hora. 28Pai, glorifica o teu nome!”

Então veio uma voz dos céus: “Eu já o glorifiquei e o glorificarei novamente”. 29A multidão que ali estava e a ouviu disse que tinha trovejado; outros disseram que um anjo lhe tinha falado.

30Jesus disse: “Esta voz veio por causa de vocês e não por minha causa. 31Chegou a hora de ser julgado este mundo; agora será expulso o príncipe deste mundo. 32Mas eu, quando for levantado da terra, atrairei todos a mim”. 33Ele disse isso para indicar o tipo de morte que haveria de sofrer.

34A multidão falou: “A Lei nos ensina que o Cristo permanecerá para sempre; como podes dizer: ‘O Filho do homem precisa ser levantado’? Quem é esse ‘Filho do homem’?”

35Disse-lhes então Jesus: “Por mais um pouco de tempo a luz estará entre vocês. Andem enquanto vocês têm a luz, para que as trevas não os surpreendam, pois aquele que anda nas trevas não sabe para onde está indo. 36Creiam na luz enquanto vocês a têm, para que se tornem filhos da luz”. Terminando de falar, Jesus saiu e ocultou-se deles.

A Incredulidade dos Judeus

37Mesmo depois que Jesus fez todos aqueles sinais milagrosos, não creram nele. 38Isso aconteceu para se cumprir a palavra do profeta Isaías, que disse:

“Senhor, quem creu em nossa mensagem,

e a quem foi revelado o braço do Senhor?”12.38 Is 53.1

39Por esta razão eles não podiam crer, porque, como disse Isaías noutro lugar:

40“Cegou os seus olhos

e endureceu-lhes o coração,

para que não vejam com os olhos

nem entendam com o coração,

nem se convertam, e eu os cure”12.40 Is 6.10.

41Isaías disse isso porque viu a glória de Jesus e falou sobre ele.

42Ainda assim, muitos líderes dos judeus creram nele. Mas, por causa dos fariseus, não confessavam a sua fé, com medo de serem expulsos da sinagoga; 43pois preferiam a aprovação12.43 Grego: glória. dos homens do que a aprovação de Deus.

44Então Jesus disse em alta voz: “Quem crê em mim, não crê apenas em mim, mas naquele que me enviou. 45Quem me vê, vê aquele que me enviou. 46Eu vim ao mundo como luz, para que todo aquele que crê em mim não permaneça nas trevas.

47“Se alguém ouve as minhas palavras e não lhes obedece, eu não o julgo. Pois não vim para julgar o mundo, mas para salvá-lo. 48Há um juiz para quem me rejeita e não aceita as minhas palavras; a própria palavra que proferi o condenará no último dia. 49Pois não falei por mim mesmo, mas o Pai que me enviou me ordenou o que dizer e o que falar. 50Sei que o seu mandamento é a vida eterna. Portanto, o que eu digo é exatamente o que o Pai me mandou dizer”.