Yoeli 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoeli 3:1-21

Mataifa Yahukumiwa

13:1 Kum 30:3; Yer 16:15; 40:5; Eze 3:20; 38:8“Katika siku hizo na wakati huo,

nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,

23:2 Zek 14:2; Isa 13:9; 2Nya 20:26; Isa 66:16; Yer 2:35; Sef 3:8; Mwa 11:4; Law 26:33nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta

katika Bonde la Yehoshafati3:2 Yehoshafati maana yake Bwana huhukumu.

Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao

kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli,

kwa kuwa waliwatawanya watu wangu

miongoni mwa mataifa

na kuigawa nchi yangu.

33:3 Oba 1:11; Amo 2:6; Ay 6:27; Eze 24:6Wanawapigia kura watu wangu

na kuwauza wavulana ili kupata makahaba;

waliwauza wasichana

ili wapate kunywa mvinyo.

43:4 Mwa 10:15; Mt 11:21; Yak 2:13; Lk 18:7; Amo 1:6-9; Isa 14:29-31; 34:8; Za 87:4; Eze 25:15-17“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda. 53:5 1Fal 15:18; 2Nya 21:16-17Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu. 63:6 Eze 27:13; Zek 9:13Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.

73:7 Isa 43:5-6; 66:6; Yer 23:8“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya. 83:8 Eze 23:42; Isa 14:2; 60:14; Mwa 10:7; Yer 30:16; 2Nya 9:1Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.

93:9 Isa 8:9; Yer 46:4Tangazeni hili miongoni mwa mataifa:

Jiandaeni kwa vita!

Amsha askari!

Wanaume wote wapiganaji

wasogee karibu na kushambulia.

103:10 Zek 12:8; Isa 2:4; Mik 4:3; Hes 25:7Majembe yenu yafueni yawe panga

na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki.

Aliye dhaifu na aseme,

“Mimi nina nguvu!”

113:11 Eze 38:15-16; Sef 3:8; Isa 13:3Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote,

kusanyikeni huko.

Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!

123:12 Za 96:13; 82:1; 2Nya 20:26; Isa 2:4“Mataifa na yaamshwe;

na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati,

kwa kuwa nitaketi mahali pale

kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.

133:13 Isa 17:5; Ufu 14:15-20; Amu 6:11; Mt 13:39; Mk 4:29; Yer 51:33; Hos 6:11Tia mundu,

kwa kuwa mavuno yamekomaa.

Njooni, mkanyage zabibu,

kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa

na mapipa yanafurika:

kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”

143:14 Isa 2:4; 13:4; 34:2-8; Sef 1:7; Yoe 1:15; Eze 36:5Umati mkubwa, umati mkubwa

katika bonde la uamuzi!

Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu

katika bonde la uamuzi.

15Jua na mwezi vitatiwa giza,

na nyota hazitatoa mwanga wake tena.

163:16 Amu 5:4; Isa 14:16; 25:4; 42:13; 2Sam 22:3; Zek 9:12; Eze 38:19Bwana atanguruma kutoka Sayuni

na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu;

dunia na mbingu vitatikisika.

Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake,

ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.

Baraka Kwa Watu Wa Mungu

173:17 Yoe 2:27; Za 74:2; Isa 4:3; 35:8; Ufu 21:27; Nah 1:15; Kut 6:7; Yer 31:40; Eze 44:9“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu,

nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.

Yerusalemu utakuwa mtakatifu;

kamwe wageni hawatavamia tena.

183:18 Kut 3:8; Eze 47:1; Zek 13:1; Wim 5:1; Isa 25:6; 30:25; 35:6; 44:3; Ufu 22:1-2; Hes 25:1; Yoe 2:24“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya,

na vilima vitatiririka maziwa;

mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji.

Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana

na kunywesha Bonde la Shitimu.3:18 Au: Bonde la Migunga.

193:19 Yer 51:35; Oba 1:10; Isa 11:14; 34:11Lakini Misri itakuwa ukiwa,

Edomu itakuwa jangwa tupu,

kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda,

ambao katika nchi yao

walimwaga damu isiyo na hatia.

203:20 Ezr 9:12; Amo 9:15Yuda itakaliwa na watu milele

na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.

213:21 Eze 36:25; 48:35; Isa 1:15; 59:20; Za 74:2; Zek 8:3Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe,

nitasamehe.”

Bwana anakaa Sayuni!

New International Version – UK

Joel 3:1-21

The nations judged

In Hebrew texts 3:1-21 is numbered 4:1-21. 1‘In those days and at that time,

when I restore the fortunes of Judah and Jerusalem,

2I will gather all nations

and bring them down to the Valley of Jehoshaphat.3:2 Jehoshaphat means the Lord judges; also in verse 12.

There I will put them on trial

for what they did to my inheritance, my people Israel,

because they scattered my people among the nations

and divided up my land.

3They cast lots for my people

and traded boys for prostitutes;

they sold girls for wine to drink.

4‘Now what have you against me, Tyre and Sidon and all you regions of Philistia? Are you repaying me for something I have done? If you are paying me back, I will swiftly and speedily return on your own heads what you have done. 5For you took my silver and my gold and carried off my finest treasures to your temples.3:5 Or palaces 6You sold the people of Judah and Jerusalem to the Greeks, that you might send them far from their homeland.

7‘See, I am going to rouse them out of the places to which you sold them, and I will return on your own heads what you have done. 8I will sell your sons and daughters to the people of Judah, and they will sell them to the Sabeans, a nation far away.’ The Lord has spoken.

9Proclaim this among the nations:

Prepare for war!

Rouse the warriors!

Let all the fighting men draw near and attack.

10Beat your ploughshares into swords

and your pruning hooks into spears.

Let the weakling say,

‘I am strong!’

11Come quickly, all you nations from every side,

and assemble there.

Bring down your warriors, Lord!

12‘Let the nations be roused;

let them advance into the Valley of Jehoshaphat,

for there I will sit

to judge all the nations on every side.

13Swing the sickle,

for the harvest is ripe.

Come, trample the grapes,

for the winepress is full

and the vats overflow –

so great is their wickedness!’

14Multitudes, multitudes

in the valley of decision!

For the day of the Lord is near

in the valley of decision.

15The sun and moon will be darkened,

and the stars no longer shine.

16The Lord will roar from Zion

and thunder from Jerusalem;

the earth and the heavens will tremble.

But the Lord will be a refuge for his people,

a stronghold for the people of Israel.

Blessings for God’s people

17‘Then you will know that I, the Lord your God,

dwell in Zion, my holy hill.

Jerusalem will be holy;

never again will foreigners invade her.

18‘In that day the mountains will drip new wine,

and the hills will flow with milk;

all the ravines of Judah will run with water.

A fountain will flow out of the Lord’s house

and will water the valley of acacias.3:18 Or Valley of Shittim

19But Egypt will be desolate,

Edom a desert waste,

because of violence done to the people of Judah,

in whose land they shed innocent blood.

20Judah will be inhabited for ever

and Jerusalem through all generations.

21Shall I leave their innocent blood unavenged?

No, I will not.’

The Lord dwells in Zion!