Yoeli 2 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoeli 2:1-32

Jeshi La Nzige

12:1 Hos 10:2, 7; Kut 15:17; Oba 1:15; Sef 1:14-16; Eze 12:23Pigeni tarumbeta katika Sayuni;

pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu.

Wote waishio katika nchi na watetemeke,

kwa kuwa siku ya Bwana inakuja. Iko karibu,

22:2 Ay 9:7; Isa 8:22; 13:10; Amo 5:18; Kut 10:14; Dan 9:12; Mt 24:21; Eze 34:12siku ya giza na huzuni,

siku ya mawingu na utusitusi.

Kama mapambazuko yasambaavyo

toka upande huu wa milima

hata upande mwingine

jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja.

Jambo kama hili halijakuwepo tangu zamani

wala halitakuwepo tena kamwe

kwa vizazi vijavyo.

32:3 Za 97:3; 105:34-35; Kut 10:12-15; Isa 14:17; Zek 7:14; Isa 1:31Mbele yao moto unateketeza,

nyuma yao miali ya moto

inawaka kwa nguvu.

Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni,

nyuma yao ni jangwa lisilofaa:

hakuna kitu kinachowaepuka.

4Wanaonekana kama farasi;

wanakwenda mbio

kama askari wapanda farasi.

52:5 Ufu 9:9; Isa 5:24; 30:30Wanatoa sauti kama magari ya vita,

wanaporukaruka juu ya vilele vya milima,

kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua,

kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.

62:6 Yer 8:21; Isa 13Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu;

kila uso unabadilika rangi.

72:7 Isa 5:27; Mit 30:27; Ay 16:14Wanashambulia kama wapiganaji wa vita;

wanapanda kuta kama askari.

Wote wanatembea katika safu,

hawapotoshi safu zao.

8Hakuna anayemsukuma mwenzake;

kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja.

Wanapita katika vizuizi

bila kuharibu safu zao.

92:9 Yer 9:21; Kut 10:6Wanaenda kasi kuingia mjini;

wanakimbia ukutani.

Wanaingia ndani ya nyumba;

kwa kuingilia madirishani kama wevi.

102:10 Isa 5:30; 13:10; Za 18:7; 102:26; Ufu 9:2; Ay 9:7; Eze 38:19Mbele yao dunia inatikisika,

anga linatetemeka,

jua na mwezi vinatiwa giza,

na nyota hazitoi mwanga wake tena.

112:11 Isa 2:12; Hes 24:23; Ufu 6:17; 18:8; Sef 2:11; Eze 30:3; Yoe 1:15; Yer 50:34; Mal 3:2; Za 29:3Bwana anatoa mshindo wa ngurumo

mbele ya jeshi lake;

majeshi yake hayana idadi,

ni wenye nguvu nyingi

wale ambao hutii agizo lake.

Siku ya Bwana ni kuu,

ni ya kutisha.

Ni nani anayeweza kuistahimili?

Rarueni Mioyo Yenu

122:12 Kum 4:30; Hos 12:6; Eze 33:11; 1Sam 7:3“Hata sasa,” asema Bwana,

“nirudieni kwa mioyo yenu yote,

kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”

132:13 Za 34:18; 51:17; 86:5; Mwa 37:29; Hes 14:6; Kut 34:6; Yon 4:2; Isa 57:15; 2Fal 22:19; Mt 5:3-4; Ay 1:20Rarueni mioyo yenu

na siyo mavazi yenu.

Mrudieni Bwana, Mungu wenu,

kwa maana yeye ndiye mwenye neema

na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo,

huona huruma, hujizuia kuleta maafa.

142:14 Yer 26:3; 31:14; Yn 3:9; Sef 2:3; Isa 65:8; Zek 8:13; Yos 14:12; Amo 5:15; Hag 2:19; Mal 3:10Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma

na kuacha baraka nyuma yake:

sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji

kwa ajili ya Bwana Mungu wenu.

152:15 2Nya 20:3; Hes 10:2-3; Yer 36:9Pigeni tarumbeta katika Sayuni,

tangazeni saumu takatifu,

liiteni kusanyiko takatifu.

162:16 Kut 19:10; 2Nya 20:13; 1Kor 7:5; Za 19Wakusanyeni watu,

wekeni wakfu kusanyiko;

waleteni pamoja wazee,

wakusanyeni watoto,

wale wanyonyao maziwa.

Bwana arusi na atoke chumbani mwake

na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.

172:17 Eze 8:16; Mt 23:35; Kum 9:26-29; Ay 17:6; Za 42:3; Kut 32:11; Isa 37:20; Yoe 1:13; Isa 22:12Makuhani, ambao wanahudumu mbele za Bwana,

na walie katikati ya ukumbi

wa Hekalu na madhabahu.

Waseme, “Wahurumie watu wako, Ee Bwana.

Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa,

neno la dhihaka kati ya mataifa.

Kwa nini wasemezane miongoni mwao,

‘Yuko wapi Mungu wao?’ ”

Jibu La Bwana

182:18 Isa 26:11; 42:13; Zek 8:2; 1:14; Kum 32:36; Za 103:13; 72:13Kisha Bwana atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake

na kuwa na huruma juu ya watu wake.

192:19 Yer 31:12; Eze 34:29; Za 4:7; Law 26:5Bwana atawajibu:

“Ninawapelekea nafaka,

mvinyo mpya na mafuta,

vya kuwatosha ninyi

hadi mridhike kabisa;

kamwe sitawafanya tena

kitu cha kudharauliwa na mataifa.

202:20 Yer 1:14-15; Zek 14:8; Kum 11:24; Kut 10:19; Isa 34:3“Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi,

nikilisukuma ndani ya jangwa,

askari wa safu za mbele wakienda

ndani ya bahari ya mashariki

na wale wa safu za nyuma

katika bahari ya magharibi.

Uvundo wake utapaa juu;

harufu yake itapanda juu.”

Hakika ametenda mambo makubwa.

212:21 Sef 3:16-17; Isa 25:1; 29:22; 54:4; 1Yn 4:18Usiogope, ee nchi;

furahi na kushangilia.

Hakika Bwana ametenda mambo makubwa.

222:22 Yoe 1:18-20; Zek 8:12; Za 65:12; Hes 16:14; 1Fal 4:25Msiogope, enyi wanyama pori,

kwa kuwa mbuga za malisho yenu

zinarudia ubichi.

Miti nayo inazaa matunda,

mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.

232:23 Hab 3:18; Yak 5:7; Za 28:7; 33:21; Law 26:4Furahini, enyi watu wa Sayuni,

shangilieni katika Bwana Mungu wenu,

kwa kuwa amewapa mvua za vuli

kwa kipimo cha haki.

Anawapelekea mvua nyingi,

mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.

242:24 Law 26:10; Mal 3:10; Mit 3:10; Amo 9:13; Yoe 3:18Sakafu za kupuria zitajaa nafaka,

mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.

252:25 Kut 14:10; Amo 4:9“Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige:

parare, madumadu na tunutu,

jeshi langu kubwa ambalo

nililituma katikati yenu.

262:26 Law 23:40; 26:5; Isa 25:1; 29:22; 62:9; Za 126:3; Mik 6:14Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe,

na mtalisifu jina la Bwana Mungu wenu,

ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu;

kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.

272:27 Kut 6:2; Isa 44:8; 45:5; 54:4; Yoe 3:17; Law 26:11; Sef 3:11Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli

kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu,

na kwamba hakuna mwingine;

kamwe watu wangu hawataaibika tena.

Siku Ya Bwana

282:28 Yn 7:38; 11:2; Eze 39:29; Mdo 21:9; Hes 11:17; Gal 3:14; 1Sam 19:20“Hata itakuwa, baada ya hayo,

nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili.

Wana wenu na binti zenu watatabiri,

wazee wenu wataota ndoto,

na vijana wenu wataona maono.

292:29 1Kor 12:13; Gal 3:28; Eze 36:27Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake,

katika siku zile nitamimina Roho wangu.

302:30 Lk 21:11; Mk 13:24-25Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu

na duniani:

damu, moto na mawimbi ya moshi.

312:31 Isa 22:5; Mt 24:29; Isa 13:9-10; Mal 3:2; Yer 4:23; Yoe 1:15Jua litageuzwa kuwa giza

na mwezi kuwa mwekundu kama damu,

kabla ya kuja siku ya Bwana

ile kuu na ya kutisha.

322:32 Rum 9:27; 10:13; Oba 1:17; Mik 4:7; 7:18; Isa 11:11; 46:13; Za 106:8; 50:12; Yer 33:3; Mwa 4:26; Mdo 2:21, 39Na kila mtu atakayeliitia

jina la Bwana ataokolewa.

Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu

kutakuwepo wokovu,

kama Bwana alivyosema,

miongoni mwa walionusurika

ambao Bwana awaita.

Korean Living Bible

요엘 2:1-32

여호와의 날

1시온에서 나팔을 불고 2:1 또는 ‘나의 성산에서’하나님의 거룩한 산에서 경종을 울려 이 땅에 사는 모 든 사람들을 떨게 하라. 여호와의 심판 날이 다가오고 있다.

2그 날은 어둡고 침울한 날이며 캄캄하고 구름 낀 날이다. 새벽의 여명이 온 산을 뒤덮듯이 크고 강한 군대가 이르렀으니 이와 같은 일은 전에도 없었고 앞으로도 없을 것이다.

3불이 그들의 앞을 삼키고 불꽃이 그들의 뒤를 태우고 있다. 그들의 앞에 있는 땅은 에덴 동산 같고 그들의 뒤에 있는 땅은 황폐한 사막 같으니 그들을 피할 자가 없을 것이다.

4그들은 모양이 말 같아서 기병처럼 달린다.

5그들이 산꼭대기에서 뛰는 소리는 전차 소리 같고 마른 풀이 불에 타는 소리 같으며 그들이 전열을 갖춘 큰 군대처럼 늘어섰으니

6그들을 본 사람들이 질겁하여 새파랗게 질려 버렸다.

7그들은 용사처럼 공격하며 무사처럼 성벽을 기어오르고 곧장 앞을 향하여 자기 대열을 벗어나지 않는다.

8그들이 서로 부딪치지 않고 각자 자기 위치를 지키며 방어진을 뚫고 나아가나 대열이 끊어지지 않는구나.

9그들이 성으로 뛰어들고 성벽 위로 달리며 집 안으로 기어오르고 도둑같이 창으로 들어가니

10그들 앞에서 땅이 진동하며 하늘이 떨고 해와 달이 어두워지며 별들이 빛을 잃는다.

11여호와께서 그 군대에게 명령을 내리시고 그의 명령을 수행하는 군대는 그 수가 엄청나고 막강하다. 여호와의 날이 무섭고 두려우니 누가 살아 남을 수 있겠는가?

너희 마음을 찢어라

12여호와께서 “너희는 지금이라도 금식하고 울고 애통하며 진심으로 뉘우치고 나에게 돌아오라” 고 말씀하신다.

13그러므로 너희는 옷을 찢을 것이 아니라 너희 마음을 찢고 너희 하나님 여호와에게 돌아오라. 그는 은혜롭고 자비로우시며 좀처럼 화를 내지 않으시고 사랑이 많으셔서 벌하는 것을 마음 아프게 여기는 분이시다.

14혹시 너희 하나님 여호와께서 뜻을 돌이키시고 너희를 축복하셔서 너희 하나님께 소제를 드릴 곡식과 전제를 드릴 포도주를 주실는지 누가 알겠는가?

15너희는 시온에서 나팔을 불어 특별히 금식일을 정하고 거룩한 모임을 선포하여

16백성을 모으고 그 모임을 거룩하게 하라. 장로들을 데려오고 아이들과 젖먹이들을 모으며 신혼 부부도 그들의 방에서 나오게 하라.

17여호와를 섬기는 제사장들은 성전 현관과 제단 사이에서 울며 이렇게 기도하라. “여호와여, 우리를 불쌍히 여기셔서 주의 백성인 우리가 이방 나라의 멸시와 조롱거리가 되지 않게 하소서. 어째서 이방 나라들에게 ‘너희 하나님이 어디 있느냐?’ 하고 말하게 하십니까?”

여호와의 응답

18그때 여호와께서 2:18 또는 ‘자기땅을위하여중심이뜨거우시며’자기 땅에 대하여 관심을 보이시고 자기 백성을 불쌍히 여기시며

19그들에게 이렇게 대답하실 것이다. “내가 너희에게 곡식과 새 포도주와 기름을 주어 너희를 흡족하게 하고 다시는 너희가 이방 나라의 멸시를 당하지 않게 하겠다.

20내가 북쪽 군대를 너희에게서 멀리 추방하여 메마르고 황폐한 땅으로 몰아내겠다. 그 전군은 2:20 원문에는 ‘동해’사해로 들어가고 그 후군은 2:20 원문에는 ‘서해’지중해로 들어갈 것이다. 그래서 악취가 나고 상한 냄새가 올라올 것이다. 이것은 내가 너희를 위해 큰 기적을 행하였기 때문이다.”

21땅이여, 두려워하지 말고 기뻐하며 즐거워하라. 여호와께서 큰 일을 행하셨다.

22들짐승들아, 두려워하지 말아라. 메마른 들판이 다시 푸르게 되고 나무가 열매를 맺으며 무화과나무와 포도나무가 다시 무성해질 것이다.

23시온의 백성들아, 너희는 너희 하나님 여호와께서 너희를 위해 행하신 일을 보고 기뻐하며 즐거워하라. 그가 너희를 용서한 표로 비를 주실 것이니 이전처럼 2:23 또는 ‘늦은비’봄비와 2:23 또는 ‘이른비’가을비를 너희에게 내려 주실 것이다.

24그래서 타작 마당에는 곡식이 가득하고 독에는 새 포도주와 기름이 넘칠 것이다.

25여호와께서 말씀하신다. “내가 전에 너희에게 보낸 큰 군대, 곧 메뚜기와 느치와 황충과 팥중이가 먹은 것만큼 너희에게 갚아 주겠다.

26너희는 배부를 때까지 실컷 먹고 너희를 위해 놀라운 일을 행한 너희 하나님 나 여호와의 이름을 찬양할 것이며 다시는 수치를 당하지 않을 것이다.

27그때 너희는 내가 이스라엘 백성 가운데 있으며 나만이 너희 하나님 여호와임을 알게 될 것이다. 그리고 너희가 다시는 수치를 당하지 않을 것이다.”

성령에 대한 약속

28“그 후에 내가 성령을 모든 사람에게 부어 주겠다. 너희 자녀들은 예언할 것이며 너희 노인들은 꿈을 꾸고 너희 청년들은 환상을 볼 것이다.

29그 때에 내가 또 나의 남녀 종들에게 성령을 부어 줄 것이며

30내가 하늘과 땅에 이상한 징조를 보여 줄 것이니 곧 피와 불과 연기 기둥이다.

31나 여호와의 크고 두려운 날이 오기 전에 해가 어두워지고 달이 핏빛으로 변할 것이다.

32누구든지 나 여호와의 이름을 부르는 사람은 구원을 받을 것이다. 내가 말한 대로 시온산과 예루살렘에서 피할 자가 있을 것이며 살아 남은 사람 중에 나의 부름을 받을 자가 있을 것이다.”