Yeremia 9 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 9:1-26

19:1 Mao 3:48; Isa 22:4; Za 119:136; Yer 13:17; 14:17; Mao 2:11Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji

na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi!

Ningelia usiku na mchana

kwa kuuawa kwa watu wangu.

29:2 Hes 25:1; Hos 4:2; Za 55:7; Yer 23:10; Hos 7:4; 1Fal 19:10; Isa 24:16Laiti ningekuwa na nyumba

ya kukaa wasafiri jangwani,

ningewaacha watu wangu

na kwenda mbali nao,

kwa kuwa wote ni wazinzi,

kundi la watu wadanganyifu.

39:3 Kut 20:16; Mik 6:12; Amu 2:10; 1Sam 2:12; Za 64:3; Isa 44; 20; Yer 18:18“Huweka tayari ndimi zao kama upinde,

ili kurusha uongo;

wamekuwa na nguvu katika nchi

lakini si katika ukweli.

Wanatoka dhambi moja hadi nyingine,

hawanitambui mimi,”

asema Bwana.

49:4 Mik 7:5-6; Mwa 27:35; 2Sam 15:12; Kut 20:16; Law 19:16“Jihadhari na rafiki zako;

usiwaamini ndugu zako.

Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu,

na kila rafiki ni msingiziaji.

59:5 Za 15:2; Law 6:2; Isa 59:15Rafiki humdanganya rafiki,

hakuna yeyote asemaye kweli.

Wamefundisha ndimi zao kudanganya,

wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.

69:6 Yer 5:27; Mit 1:24Unakaa katikati ya udanganyifu;

katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,”

asema Bwana.

79:7 Ay 28:1; Isa 1:28; Hos 11:8; Yer 6:27Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu,

kwani ni nini kingine niwezacho kufanya

kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?

89:8 Za 35:20; Yer 5:26; Isa 3:5Ndimi zao ni mshale wenye sumu,

hunena kwa udanganyifu.

Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake,

lakini moyoni mwake humtegea mtego.

99:9 Kum 32:43; Isa 10:3Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?”

asema Bwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

kwa taifa kama hili?”

109:10 Hos 4:3; Yoe 1:18; Yer 31:35; 32:18; 23:10; 4:25; 12:4Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima

na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani.

Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo,

milio ya ngʼombe haisikiki.

Ndege wa angani wametoroka

na wanyama wamekimbia.

119:11 Ay 30:29; Isa 34:13; Law 26:31; Mao 1:4; Yer 26:18; Isa 25:2“Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu,

makao ya mbweha;

nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa

ili asiwepo atakayeishi humo.”

129:12 Za 107:43; Hos 14:9Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?

139:13 2Nya 7:19; Za 89:30-32Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu. 149:14 Amo 2:4; Yer 3:17; 7:24; 2:8Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.” 159:15 Mao 3:15; Yer 8:14; Za 80:5Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu. 169:16 Law 26:33; Kum 28:64; 4:32; Eze 5:12; Yer 44:27; 8:19Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”

179:17 2Nya 35:25; Amo 5:15-16; Mhu 12:5Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje,

waite wale walio na ustadi kuliko wote.

189:18 Za 119:136; Mao 3:48; Yer 14:17Nao waje upesi

na kutuombolezea,

mpaka macho yetu yafurike machozi

na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.

199:19 Law 18:29; Yer 4:13Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni:

‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa!

Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa!

Ni lazima tuihame nchi yetu

kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’ ”

209:20 Isa 32:9-13; Yer 23:16Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana;

fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake.

Wafundisheni binti zenu kuomboleza;

fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.

219:21 2Nya 36:17; Isa 40:30; Yoe 2:9; Yer 16:6Mauti imeingia ndani kupitia madirishani,

imeingia kwenye majumba yetu ya fahari;

imewakatilia mbali watoto katika barabara

na vijana waume kutoka viwanja vya miji.

229:22 2Fal 9:37; Yer 8:2Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Maiti za wanaume zitalala

kama mavi katika mashamba,

kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji,

wala hakuna anayekusanya.’ ”

239:23 Ay 4:12; Isa 5:21; Mhu 9:11; Za 62:10; 1Fal 20:11; Mit 11:28; Eze 28:4-5; Yer 48:7Hili ndilo asemalo Bwana:

“Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake,

au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake,

wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,

249:24 Gal 6:14; 2Kor 10:17; Za 34:2; Mik 6:8; Za 36:6; 1Kor 1:31lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili:

kwamba ananifahamu na kunijua mimi,

kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema,

hukumu na haki duniani,

kwa kuwa napendezwa na haya,”

asema Bwana.

259:25 Law 26:41; Rum 2:8-9; Amo 3:2“Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana, 269:26 Yer 25:23; 49:32; Mdo 7:51; Rum 2:28; Eze 31:18; 1Sam 14:6yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”

Nova Versão Internacional

Jeremias 9:1-26

1Ah, se a minha cabeça fosse uma fonte de água

e os meus olhos um manancial de lágrimas!

Eu choraria noite e dia

pelos mortos do meu povo.

2Ah, se houvesse um alojamento

para mim no deserto,

para que eu pudesse deixar o meu povo

e afastar-me dele.

São todos adúlteros,

um bando de traidores!

3“A língua deles é como um arco

pronto para atirar.

É a falsidade, não a verdade,

que prevalece nesta terra.9.3 Ou um arco que atira a mentira; não é pela verdade que prevalecem na terra.

Eles vão de um crime a outro;

eles não me reconhecem”,

declara o Senhor.

4“Cuidado com os seus amigos,

não confie em seus parentes.

Porque cada parente é um enganador9.4 Ou um Jacó enganador,

e cada amigo um caluniador.

5Amigo engana amigo, ninguém fala a verdade.

Eles treinaram a língua para mentir;

e, sendo perversos, eles se cansam demais

para se converterem.9.5 Ou eles se cansam de tanto pecar.

6De opressão em opressão, de engano em engano,

eles se recusam a reconhecer-me”,

declara o Senhor.

7Portanto, assim diz o Senhor dos Exércitos:

“Vejam, sou eu que vou refiná-los e prová-los.

Que mais posso eu fazer pelo meu povo?

8A língua deles é uma flecha mortal;

eles falam traiçoeiramente.

Cada um mostra-se cordial com o seu próximo,

mas no íntimo lhe prepara uma armadilha.

9Deixarei eu de castigá-los?”,

pergunta o Senhor.

“Não me vingarei

de uma nação como essa?”

10Chorarei, prantearei e me lamentarei pelos montes

por causa das pastagens da estepe;

pois estão abandonadas e ninguém mais as percorre.

Não se ouve o mugir do gado;

tanto as aves como os animais fugiram.

11“Farei de Jerusalém um amontoado de ruínas,

uma habitação de chacais.

Devastarei as cidades de Judá

até não restar nenhum morador.”

12Quem é bastante sábio para compreender isso? Quem foi instruído pelo Senhor, que possa explicá-lo? Por que a terra está arruinada e devastada como um deserto pelo qual ninguém passa?

13O Senhor disse: “Foi porque abandonaram a minha lei, que estabeleci diante deles; não me obedeceram nem seguiram a minha lei. 14Em vez disso, seguiram a dureza de seus próprios corações, indo atrás dos baalins, como os seus antepassados lhes ensinaram”. 15Por isso, assim diz o Senhor dos Exércitos, o Deus de Israel: “Vejam! Farei este povo comer comida amarga e beber água envenenada. 16Eu os espalharei entre as nações que nem eles nem os seus antepassados conheceram; e enviarei contra eles a espada até exterminá-los”.

17Assim diz o Senhor dos Exércitos:

“Considerem: Chamem as pranteadoras profissionais;

mandem chamar as mais hábeis entre elas.

18Venham elas depressa e lamentem por nós,

até que os nossos olhos transbordem de lágrimas

e águas corram de nossas pálpebras.

19O som de lamento se ouve desde Sião:

‘Como estamos arruinados!

Como é grande a nossa humilhação!

Deixamos a nossa terra

porque as nossas casas estão em ruínas’ ”.

20Ó mulheres, ouçam agora a palavra do Senhor;

abram os ouvidos às palavras de sua boca.

Ensinem suas filhas a lamentar-se;

ensinem umas as outras a prantear.

21A morte subiu e penetrou pelas nossas janelas

e invadiu as nossas fortalezas,

eliminando das ruas as crianças

e das praças os rapazes.

22“Diga: Assim declara o Senhor:

“Cadáveres ficarão estirados

como esterco em campo aberto,

como o trigo deixado para trás pelo ceifeiro,

sem que ninguém o ajunte.”

23Assim diz o Senhor:

“Não se glorie o sábio em sua sabedoria

nem o forte em sua força

nem o rico em sua riqueza,

24mas quem se gloriar, glorie-se nisto:

em compreender-me e conhecer-me,

pois eu sou o Senhor

e ajo com lealdade,

com justiça e com retidão sobre a terra,

pois é dessas coisas que me agrado”,

declara o Senhor.

25“Vêm chegando os dias”, declara o Senhor, “em que castigarei todos os que são circuncidados apenas no corpo, 26como também o Egito, Judá, Edom, Amom, Moabe e todos os que rapam a cabeça9.26 Ou e todos os que prendem o cabelo junto à testa e vivem no deserto; porque todas essas nações são incircuncisas, e a comunidade de Israel tem o coração obstinado9.26 Hebraico: é incircuncisa de coração..”