Yeremia 9 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 9:1-26

19:1 Mao 3:48; Isa 22:4; Za 119:136; Yer 13:17; 14:17; Mao 2:11Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji

na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi!

Ningelia usiku na mchana

kwa kuuawa kwa watu wangu.

29:2 Hes 25:1; Hos 4:2; Za 55:7; Yer 23:10; Hos 7:4; 1Fal 19:10; Isa 24:16Laiti ningekuwa na nyumba

ya kukaa wasafiri jangwani,

ningewaacha watu wangu

na kwenda mbali nao,

kwa kuwa wote ni wazinzi,

kundi la watu wadanganyifu.

39:3 Kut 20:16; Mik 6:12; Amu 2:10; 1Sam 2:12; Za 64:3; Isa 44; 20; Yer 18:18“Huweka tayari ndimi zao kama upinde,

ili kurusha uongo;

wamekuwa na nguvu katika nchi

lakini si katika ukweli.

Wanatoka dhambi moja hadi nyingine,

hawanitambui mimi,”

asema Bwana.

49:4 Mik 7:5-6; Mwa 27:35; 2Sam 15:12; Kut 20:16; Law 19:16“Jihadhari na rafiki zako;

usiwaamini ndugu zako.

Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu,

na kila rafiki ni msingiziaji.

59:5 Za 15:2; Law 6:2; Isa 59:15Rafiki humdanganya rafiki,

hakuna yeyote asemaye kweli.

Wamefundisha ndimi zao kudanganya,

wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.

69:6 Yer 5:27; Mit 1:24Unakaa katikati ya udanganyifu;

katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,”

asema Bwana.

79:7 Ay 28:1; Isa 1:28; Hos 11:8; Yer 6:27Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu,

kwani ni nini kingine niwezacho kufanya

kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?

89:8 Za 35:20; Yer 5:26; Isa 3:5Ndimi zao ni mshale wenye sumu,

hunena kwa udanganyifu.

Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake,

lakini moyoni mwake humtegea mtego.

99:9 Kum 32:43; Isa 10:3Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?”

asema Bwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

kwa taifa kama hili?”

109:10 Hos 4:3; Yoe 1:18; Yer 31:35; 32:18; 23:10; 4:25; 12:4Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima

na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani.

Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo,

milio ya ngʼombe haisikiki.

Ndege wa angani wametoroka

na wanyama wamekimbia.

119:11 Ay 30:29; Isa 34:13; Law 26:31; Mao 1:4; Yer 26:18; Isa 25:2“Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu,

makao ya mbweha;

nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa

ili asiwepo atakayeishi humo.”

129:12 Za 107:43; Hos 14:9Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?

139:13 2Nya 7:19; Za 89:30-32Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu. 149:14 Amo 2:4; Yer 3:17; 7:24; 2:8Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.” 159:15 Mao 3:15; Yer 8:14; Za 80:5Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu. 169:16 Law 26:33; Kum 28:64; 4:32; Eze 5:12; Yer 44:27; 8:19Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”

179:17 2Nya 35:25; Amo 5:15-16; Mhu 12:5Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje,

waite wale walio na ustadi kuliko wote.

189:18 Za 119:136; Mao 3:48; Yer 14:17Nao waje upesi

na kutuombolezea,

mpaka macho yetu yafurike machozi

na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.

199:19 Law 18:29; Yer 4:13Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni:

‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa!

Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa!

Ni lazima tuihame nchi yetu

kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’ ”

209:20 Isa 32:9-13; Yer 23:16Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana;

fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake.

Wafundisheni binti zenu kuomboleza;

fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.

219:21 2Nya 36:17; Isa 40:30; Yoe 2:9; Yer 16:6Mauti imeingia ndani kupitia madirishani,

imeingia kwenye majumba yetu ya fahari;

imewakatilia mbali watoto katika barabara

na vijana waume kutoka viwanja vya miji.

229:22 2Fal 9:37; Yer 8:2Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Maiti za wanaume zitalala

kama mavi katika mashamba,

kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji,

wala hakuna anayekusanya.’ ”

239:23 Ay 4:12; Isa 5:21; Mhu 9:11; Za 62:10; 1Fal 20:11; Mit 11:28; Eze 28:4-5; Yer 48:7Hili ndilo asemalo Bwana:

“Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake,

au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake,

wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,

249:24 Gal 6:14; 2Kor 10:17; Za 34:2; Mik 6:8; Za 36:6; 1Kor 1:31lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili:

kwamba ananifahamu na kunijua mimi,

kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema,

hukumu na haki duniani,

kwa kuwa napendezwa na haya,”

asema Bwana.

259:25 Law 26:41; Rum 2:8-9; Amo 3:2“Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana, 269:26 Yer 25:23; 49:32; Mdo 7:51; Rum 2:28; Eze 31:18; 1Sam 14:6yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”

New International Version

Jeremiah 9:1-26

In Hebrew texts 9:1 is numbered 8:23, and 9:2-26 is numbered 9:1-25. 1Oh, that my head were a spring of water

and my eyes a fountain of tears!

I would weep day and night

for the slain of my people.

2Oh, that I had in the desert

a lodging place for travelers,

so that I might leave my people

and go away from them;

for they are all adulterers,

a crowd of unfaithful people.

3“They make ready their tongue

like a bow, to shoot lies;

it is not by truth

that they triumph9:3 Or lies; / they are not valiant for truth in the land.

They go from one sin to another;

they do not acknowledge me,”

declares the Lord.

4“Beware of your friends;

do not trust anyone in your clan.

For every one of them is a deceiver,9:4 Or a deceiving Jacob

and every friend a slanderer.

5Friend deceives friend,

and no one speaks the truth.

They have taught their tongues to lie;

they weary themselves with sinning.

6You9:6 That is, Jeremiah (the Hebrew is singular) live in the midst of deception;

in their deceit they refuse to acknowledge me,”

declares the Lord.

7Therefore this is what the Lord Almighty says:

“See, I will refine and test them,

for what else can I do

because of the sin of my people?

8Their tongue is a deadly arrow;

it speaks deceitfully.

With their mouths they all speak cordially to their neighbors,

but in their hearts they set traps for them.

9Should I not punish them for this?”

declares the Lord.

“Should I not avenge myself

on such a nation as this?”

10I will weep and wail for the mountains

and take up a lament concerning the wilderness grasslands.

They are desolate and untraveled,

and the lowing of cattle is not heard.

The birds have all fled

and the animals are gone.

11“I will make Jerusalem a heap of ruins,

a haunt of jackals;

and I will lay waste the towns of Judah

so no one can live there.”

12Who is wise enough to understand this? Who has been instructed by the Lord and can explain it? Why has the land been ruined and laid waste like a desert that no one can cross?

13The Lord said, “It is because they have forsaken my law, which I set before them; they have not obeyed me or followed my law. 14Instead, they have followed the stubbornness of their hearts; they have followed the Baals, as their ancestors taught them.” 15Therefore this is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: “See, I will make this people eat bitter food and drink poisoned water. 16I will scatter them among nations that neither they nor their ancestors have known, and I will pursue them with the sword until I have made an end of them.”

17This is what the Lord Almighty says:

“Consider now! Call for the wailing women to come;

send for the most skillful of them.

18Let them come quickly

and wail over us

till our eyes overflow with tears

and water streams from our eyelids.

19The sound of wailing is heard from Zion:

‘How ruined we are!

How great is our shame!

We must leave our land

because our houses are in ruins.’ ”

20Now, you women, hear the word of the Lord;

open your ears to the words of his mouth.

Teach your daughters how to wail;

teach one another a lament.

21Death has climbed in through our windows

and has entered our fortresses;

it has removed the children from the streets

and the young men from the public squares.

22Say, “This is what the Lord declares:

“ ‘Dead bodies will lie

like dung on the open field,

like cut grain behind the reaper,

with no one to gather them.’ ”

23This is what the Lord says:

“Let not the wise boast of their wisdom

or the strong boast of their strength

or the rich boast of their riches,

24but let the one who boasts boast about this:

that they have the understanding to know me,

that I am the Lord, who exercises kindness,

justice and righteousness on earth,

for in these I delight,”

declares the Lord.

25“The days are coming,” declares the Lord, “when I will punish all who are circumcised only in the flesh— 26Egypt, Judah, Edom, Ammon, Moab and all who live in the wilderness in distant places.9:26 Or wilderness and who clip the hair by their foreheads For all these nations are really uncircumcised, and even the whole house of Israel is uncircumcised in heart.”