Yeremia 9 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 9:1-26

19:1 Mao 3:48; Isa 22:4; Za 119:136; Yer 13:17; 14:17; Mao 2:11Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji

na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi!

Ningelia usiku na mchana

kwa kuuawa kwa watu wangu.

29:2 Hes 25:1; Hos 4:2; Za 55:7; Yer 23:10; Hos 7:4; 1Fal 19:10; Isa 24:16Laiti ningekuwa na nyumba

ya kukaa wasafiri jangwani,

ningewaacha watu wangu

na kwenda mbali nao,

kwa kuwa wote ni wazinzi,

kundi la watu wadanganyifu.

39:3 Kut 20:16; Mik 6:12; Amu 2:10; 1Sam 2:12; Za 64:3; Isa 44; 20; Yer 18:18“Huweka tayari ndimi zao kama upinde,

ili kurusha uongo;

wamekuwa na nguvu katika nchi

lakini si katika ukweli.

Wanatoka dhambi moja hadi nyingine,

hawanitambui mimi,”

asema Bwana.

49:4 Mik 7:5-6; Mwa 27:35; 2Sam 15:12; Kut 20:16; Law 19:16“Jihadhari na rafiki zako;

usiwaamini ndugu zako.

Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu,

na kila rafiki ni msingiziaji.

59:5 Za 15:2; Law 6:2; Isa 59:15Rafiki humdanganya rafiki,

hakuna yeyote asemaye kweli.

Wamefundisha ndimi zao kudanganya,

wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.

69:6 Yer 5:27; Mit 1:24Unakaa katikati ya udanganyifu;

katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,”

asema Bwana.

79:7 Ay 28:1; Isa 1:28; Hos 11:8; Yer 6:27Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu,

kwani ni nini kingine niwezacho kufanya

kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?

89:8 Za 35:20; Yer 5:26; Isa 3:5Ndimi zao ni mshale wenye sumu,

hunena kwa udanganyifu.

Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake,

lakini moyoni mwake humtegea mtego.

99:9 Kum 32:43; Isa 10:3Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?”

asema Bwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

kwa taifa kama hili?”

109:10 Hos 4:3; Yoe 1:18; Yer 31:35; 32:18; 23:10; 4:25; 12:4Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima

na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani.

Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo,

milio ya ngʼombe haisikiki.

Ndege wa angani wametoroka

na wanyama wamekimbia.

119:11 Ay 30:29; Isa 34:13; Law 26:31; Mao 1:4; Yer 26:18; Isa 25:2“Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu,

makao ya mbweha;

nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa

ili asiwepo atakayeishi humo.”

129:12 Za 107:43; Hos 14:9Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?

139:13 2Nya 7:19; Za 89:30-32Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu. 149:14 Amo 2:4; Yer 3:17; 7:24; 2:8Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.” 159:15 Mao 3:15; Yer 8:14; Za 80:5Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu. 169:16 Law 26:33; Kum 28:64; 4:32; Eze 5:12; Yer 44:27; 8:19Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”

179:17 2Nya 35:25; Amo 5:15-16; Mhu 12:5Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje,

waite wale walio na ustadi kuliko wote.

189:18 Za 119:136; Mao 3:48; Yer 14:17Nao waje upesi

na kutuombolezea,

mpaka macho yetu yafurike machozi

na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.

199:19 Law 18:29; Yer 4:13Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni:

‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa!

Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa!

Ni lazima tuihame nchi yetu

kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’ ”

209:20 Isa 32:9-13; Yer 23:16Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana;

fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake.

Wafundisheni binti zenu kuomboleza;

fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.

219:21 2Nya 36:17; Isa 40:30; Yoe 2:9; Yer 16:6Mauti imeingia ndani kupitia madirishani,

imeingia kwenye majumba yetu ya fahari;

imewakatilia mbali watoto katika barabara

na vijana waume kutoka viwanja vya miji.

229:22 2Fal 9:37; Yer 8:2Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Maiti za wanaume zitalala

kama mavi katika mashamba,

kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji,

wala hakuna anayekusanya.’ ”

239:23 Ay 4:12; Isa 5:21; Mhu 9:11; Za 62:10; 1Fal 20:11; Mit 11:28; Eze 28:4-5; Yer 48:7Hili ndilo asemalo Bwana:

“Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake,

au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake,

wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,

249:24 Gal 6:14; 2Kor 10:17; Za 34:2; Mik 6:8; Za 36:6; 1Kor 1:31lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili:

kwamba ananifahamu na kunijua mimi,

kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema,

hukumu na haki duniani,

kwa kuwa napendezwa na haya,”

asema Bwana.

259:25 Law 26:41; Rum 2:8-9; Amo 3:2“Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana, 269:26 Yer 25:23; 49:32; Mdo 7:51; Rum 2:28; Eze 31:18; 1Sam 14:6yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Jeremías 9:1-26

1¡Ojalá mi cabeza fuera un manantial,

y mis ojos una fuente de lágrimas,

para llorar de día y de noche

por los muertos de mi pueblo!

2¡Ojalá tuviera yo en el desierto

una posada junto al camino!

Abandonaría a mi pueblo,

y me alejaría de ellos.

Porque todos ellos son adúlteros,

son una banda de traidores.

3«Tensan su lengua como un arco;

en el país prevalece la mentira, no la verdad,

porque van de mal en peor,

y a mí no me conocen

—afirma el Señor—.

4Cuídese cada uno de su amigo,

no confíe ni siquiera en el hermano,

porque todo hermano engaña,

y todo amigo difama.

5Se engañan unos a otros;

no se hablan con la verdad.

Han enseñado a sus lenguas a mentir,

y pecan hasta el cansancio.

6»Tú, Jeremías, vives en medio de engañadores,

que por su engaño no quieren reconocerme»,

afirma el Señor.

7Por eso, así dice el Señor Todopoderoso:

«Voy a refinarlos, a ponerlos a prueba.

¿Qué más puedo hacer con mi pueblo?

8Su lengua es una flecha mortífera,

su boca solo sabe engañar;

hablan cordialmente con su amigo,

mientras en su interior le tienden una trampa.

9¿Y no los he de castigar por esto?

—afirma el Señor—.

¿Acaso no he de vengarme de semejante nación?»

10Lloraré y gemiré por las montañas,

haré lamentos por las praderas del desierto,

porque están desoladas:

ya nadie las transita

ni se escuchan los mugidos del ganado.

Desde las aves del cielo hasta los animales del campo,

todos han huido.

11«Convertiré a Jerusalén en un montón de ruinas,

en una guarida de chacales.

Convertiré en desolación las ciudades de Judá;

¡las dejaré sin habitantes!»

12¿Quién es tan sabio como para entender esto? ¿A quién habló el Señor para que lo anuncie? ¿Por qué está arruinado el país, desolado como un desierto por el que nadie pasa?

13El Señor dice: «Ellos abandonaron la ley que yo les entregué; no me obedecieron ni vivieron conforme a ella. 14Siguieron la terquedad de su corazón; se fueron tras los baales, como les habían enseñado sus antepasados». 15Por eso, así dice el Señor Todopoderoso, el Dios de Israel: «A este pueblo le daré a comer ajenjo y a beber agua envenenada. 16Los dispersaré entre naciones que ni ellos ni sus antepasados conocieron; los perseguiré con espada hasta aniquilarlos».

17Así dice el Señor Todopoderoso:

«¡Atención! Llamad a las plañideras.

Que vengan las más expertas.

18Que se den prisa,

que hagan lamentación por nosotros.

Nuestros ojos se inundarán de lágrimas,

y brotará de nuestros párpados el llanto.

19Desde Sión se escuchan gemidos y lamentos:

“Hemos sido devastados;

nos han avergonzado por completo.

Tenemos que abandonar el país,

porque han derribado nuestros hogares”».

20Escuchad, mujeres, la palabra del Señor;

reciban vuestros oídos la palabra de su boca.

Enseñad a vuestras hijas a entonar endechas;

que unas a otras se enseñen este lamento:

21«La muerte se ha metido por nuestras ventanas,

ha entrado en nuestros palacios;

ha eliminado en las calles a los niños,

y en las plazas a los jóvenes.

22Yacen tendidos los cadáveres

como estiércol sobre los campos,

como gavillas que caen tras el segador,

sin que nadie las recoja»,

afirma el Señor.

23Así dice el Señor:

«Que no se gloríe el sabio de su sabiduría,

ni el poderoso de su poder,

ni el rico de su riqueza.

24Si alguien ha de gloriarse,

que se gloríe de conocerme

y de comprender que yo soy el Señor,

que actúo en la tierra con amor,

con derecho y justicia,

pues es lo que a mí me agrada

—afirma el Señor—.

25»Vienen días —afirma el Señor— en que castigaré al que haya sido circuncidado solo del prepucio: 26castigaré a Egipto, Judá, Edom, Amón, Moab, y a todos los que viven en el desierto y se rapan las sienes. Todas las naciones son incircuncisas, pero el pueblo de Israel es incircunciso de corazón».