Yeremia 8 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 8:1-22

18:1 Isa 14:19; Za 53:5“ ‘Wakati huo, asema Bwana, mifupa ya wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, na mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka makaburi yao. 28:2 Yer 44:19; Mdo 7:42; Za 83:10; 2Fal 23:5; Yer 19:13; Ay 31:27; Yer 14:16Itawekwa wazi kwa jua, na mwezi, na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia, na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyotapakaa juu ya ardhi. 38:3 Ay 3:22; Ufu 9:6; Kum 29:28Popote nitakapowafukuzia, mabaki wote wa kizazi hiki kiovu watatamani kufa kuliko kuishi, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’

Dhambi Na Adhabu

48:4 Mik 7:8; Mit 24:16; Yer 31:19; Za 119:67“Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“ ‘Je, watu wanapoanguka hawainuki?

Je, mtu anapopotea harudi?

58:5 Yer 5:27; Isa 1:20; Yer 7:24; Zek 7:11Kwa nini basi watu hawa walipotea?

Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara?

Wanangʼangʼania udanganyifu

na wanakataa kurudi.

68:6 2Pet 3:9; Ufu 9:20; Za 14:1-3; Mal 3:16Nimewasikiliza kwa makini,

lakini hawataki kusema lililo sawa.

Hakuna anayetubia makosa yake

akisema, “Nimefanya nini?”

Kila mmoja hufuata njia yake mwenyewe

kama farasi anayekwenda vitani.

78:7 Kum 32:28; Wim 2:12; Yer 4:22Hata korongo aliyeko angani

anayajua majira yake yaliyoamriwa,

nao njiwa, mbayuwayu na koikoi

hufuata majira yao ya kurudi.

Lakini watu wangu hawajui

Bwana anachotaka kwao.

88:8 Rum 2:17; Hos 8:12“ ‘Mwawezaje kusema, “Sisi tuna busara

kwa sababu tunayo sheria ya Bwana,”

wakati ambapo kwa hakika kalamu ya uongo ya waandishi

imeandika kwa udanganyifu?

98:9 Isa 29:14; Yer 5:16-19; 2Fal 19:26; Ay 5:13; Yer 6:19; 1Kor 1:20Wenye hekima wataaibika,

watafadhaika na kunaswa.

Kwa kuwa wamelikataa neno la Bwana,

hiyo hekima waliyo nayo ni ya namna gani?

108:10 Yer 6:12; Isa 56:11; Mao 4:13; Isa 28:7; Yer 14:14; Mao 2:14; Yer 23:11-15Kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao,

na mashamba yao kwa wamiliki wengine.

Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa,

wote wana tamaa ya kupata zaidi;

manabii na makuhani wanafanana,

wote wanafanya udanganyifu.

118:11 Yer 6:14; Eze 13:10; 7:25; Yer 4:10Wanafunga majeraha ya watu wangu

bila uangalifu.

Wanasema, “Amani, amani,”

wakati hakuna amani.

128:12 Za 52:5-7; Yer 3:3; Isa 3:9; Yer 6:15Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno?

Hapana, hawana aibu hata kidogo,

hawajui hata kuona haya.

Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka,

watashushwa chini watakapoadhibiwa,

asema Bwana.

138:13 Hos 2:12; Mt 21:19; Yer 5:17; Lk 13:6“ ‘Nitayaondoa mavuno yao,

asema Bwana.

Hapatakuwepo zabibu kwenye mzabibu.

Hapatakuwepo na tini kwenye mtini,

majani yake yatanyauka.

Kile nilichowapa

watanyangʼanywa.’ ”

148:14 Yos 10:20; Yer 23:15; Kum 29:18; Dan 9:5; Yer 35:11; 9:15; 14:7, 20“Kwa nini tunaketi hapa?

Kusanyikeni pamoja!

Tukimbilie kwenye miji yenye maboma,

tukaangamie huko!

Kwa kuwa Bwana, Mungu wetu

ametuhukumu kuangamia,

na kutupa maji yenye sumu tunywe,

kwa sababu tumemtenda dhambi.

158:15 Ay 19:8; Yer 14:19Tulitegemea amani,

lakini hakuna jema lililokuja,

tulitegemea wakati wa kupona,

lakini kulikuwa hofu tu.

168:16 Mwa 30:6; Yer 4:15, 29; 51:29; 5:17Mkoromo wa farasi za adui

umesikika kuanzia Dani,

kwa mlio wa madume yao ya farasi,

nchi yote inatetemeka.

Wamekuja kuangamiza nchi na vyote vilivyomo,

mji na wote waishio ndani yake.”

178:17 Hes 21:6; Kum 32:24; Isa 3:3; Za 58:5“Tazama, nitatuma nyoka wenye sumu kali katikati yenu,

fira ambao hawawezi kulogwa,

nao watawauma,”

asema Bwana.

188:18 Mao 5:17Ee Mfariji wangu katika huzuni,

moyo wangu umezimia ndani yangu.

198:19 Kum 28:64; Yer 9:16; Mik 4:9; Yer 44:3; Isa 41:24; Kum 32:21Sikia kilio cha watu wangu

kutoka nchi ya mbali:

“Je, Bwana hayuko Sayuni?

Je, Mfalme wake hayuko tena huko?”

“Kwa nini wamenikasirisha kwa vinyago vyao,

kwa sanamu zao za kigeni zisizofaa?”

20“Mavuno yamepita,

kiangazi kimekwisha,

nasi hatujaokolewa.”

218:21 Nah 2:10; Mao 2:13; Eze 6:9; Za 94:5; Isa 43:24; Yer 4:19Kwa kuwa watu wangu wamepondwa, nami nimepondeka pia;

ninaomboleza, nayo hofu kuu imenishika.

228:22 Mwa 37:25; Yer 30:12; Ay 13:4; Isa 1:6Je, hakuna zeri ya kuponya katika Gileadi?

Je, hakuna tabibu huko?

Kwa nini basi hakuna uponyaji

wa majeraha ya watu wangu?

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 8:1-22

1耶和華說:「那時,猶大王、首領、祭司、先知及耶路撒冷居民的骸骨都要從墳墓中被挖出來, 2拋散在他們昔日戀慕、供奉、追隨、求問、祭拜的日月星辰之下,無人收殮和埋葬,他們好像地上的糞便。 3我要把這邪惡民族的餘民流放異地,他們在那裡必痛不欲生。這是萬軍之耶和華說的。」

4耶和華吩咐我對猶大人說:

「人跌倒後難道不站起來嗎?

人走錯了路難道不回頭嗎?

5為什麼耶路撒冷的居民一味地背叛我?

他們詭詐成性,不肯回頭。

6我仔細聽,沒有人說實話,

沒有人為自己的惡行後悔,說,

『我做了可怕的事!』

人人一意孤行,

像戰馬直奔戰場。

7天空的鸛鳥尚且知道來去的季節,

斑鳩、燕子和白鶴也遵守遷徙的時間,

但我的子民卻不認識耶和華的法則。

8「你們怎能說,『我們有智慧,

因為我們有耶和華的律法』?

事實上,律法教師撒謊的筆把律法篡改了。

9智者必蒙羞辱,受驚嚇,

被捉拿。

看啊,他們既棄掉耶和華的話,

哪裡還有智慧可言呢?

10因此,我要把他們的妻子和田地交給別人,

因為他們無論貴賤,

個個貪圖不義之財;

無論是先知還是祭司,

都行為詭詐。

11他們敷衍了事地醫治我子民的傷痛,說,

『沒事了,沒事了!』

其實情況很糟。

12他們做可憎的事會羞愧嗎?

不!他們不知廉恥,

毫不臉紅。

因此,他們要與其他人一樣滅亡,

死在我的懲罰下。

這是耶和華說的。

13我要徹底滅絕他們。

葡萄樹必沒有葡萄,

無花果樹必沒有果子,

樹葉也要枯乾,

我所賜給他們的都要被奪走。

這是耶和華說的。」

14他們說:「我們為什麼還坐在這裡?

大家一起進入堅城,死在那裡吧!

我們的上帝耶和華要毀滅我們,

給我們毒藥喝,

因為我們得罪了祂。

15我們期待平安,

卻沒有平安;

渴望得到醫治,

卻飽受驚嚇。

16「從傳來敵人戰馬的嘶鳴,

聲音震動大地。

他們要來吞滅我們的土地和作物、城邑和居民。

17「看啊,我要派毒蛇去咬你們,

法術無法制伏牠們。」

這是耶和華說的。

18我有無限憂愁,傷心欲絕。

19聽啊!遠處傳來我同胞的哀鳴:

「難道耶和華不在錫安了嗎?

難道她的王不在她那裡了嗎?」

耶和華說:「他們為什麼供奉雕刻的神像和外族無用的偶像,惹我發怒?」

20他們說:「麥收已完,

夏季已過,

但我們還未得救。」

21同胞的創傷令我傷心欲絕,

痛苦萬分,

驚慌失措。

22難道基列沒有藥物、

沒有醫生嗎?

為什麼我同胞的創傷至今未癒?