Yeremia 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 7:1-34

Dini Za Uongo Hazina Maana

1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 27:2 Yer 17:19; 19:2-3“Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu:

“ ‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana. 37:3 Yer 26:13; 35:13; 18:11Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa. 47:4 Yer 28:15; Mik 3:11; Ay 15:31Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!” 57:5 Kut 22:22; Law 25:17; Isa 1:17; Yer 26:13Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake, 67:6 2Fal 21:16; Kum 8:19; Yer 22:3; Kut 20:3; Yer 5:28; Eze 22:7; Yer 2:34kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe, 77:7 Kum 4:40; Yos 1:16ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele. 8Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.

97:9 Yer 11:13-17; Kut 20:3; Hos 2:13; Kut 20:13-15; Law 19:12; Zek 8:17; Yer 32:29“ ‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua, 107:10 2Fal 21:4-5; Eze 23:38-39; Yer 23:11; 32:34; Eze 33:25kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza? 117:11 Isa 56:7; Mt 21:13; Mk 11:17; Mwa 31:50; Amu 11:10; Hes 11:29; Lk 19:40; Yer 42:5Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.

127:12 1Sam 4:10; Yos 18:1; Za 78:60-64; 1Sam 2:32; Kut 40:2; Yos 18:10; Dan 9:18“ ‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli. 137:13 2Nya 36:15; Isa 65:12; Yer 35:17; Za 71:17; Isa 48:17; Yer 32:33; Mit 1:24Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu. 14Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu. 157:15 Mwa 4:14; Kut 33; 15; 2Fal 17:20; Za 78:67; Yer 23:39Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’

167:16 Kut 32:10; Kum 9:14; Hes 23:19“Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza. 17Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 187:18 Yer 44:17; 19:13; Kum 31:17; 1Fal 14:9; Isa 57:6Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha. 197:19 Ay 7:20; 1Kor 10:22; Yer 22:22; Kum 32:21; Yer 44:3; 9:19Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?

207:20 Ay 40:11; Mao 2:3-5; Isa 30:15; Yer 42:18; 6:11-12; Mao 4:11; Eze 20:47-48“ ‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.

217:21 Isa 1:11; Amo 5:21-22; 1Sam 2:12-17; Hos 8:13; Yer 6:20; 7:22; Isa 43:23; 1Sam 15:22“ ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe! 22Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu, 237:23 Kut 15:26; 19:5; Law 26:12; Kum 5:33; 1Yn 3:23; Isa 51:16; 1Fal 8:36; 7:24; Za 81:11-12; Kum 29:19; Yer 34:14; 6:10; 11:8; 17:23; 3:17; 2:19lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa. 24Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele. 257:25 Neh 9:30; Yer 25:4; 2Nya 36:15; Isa 20:3; Hes 11:29; Yer 35:15Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii. 267:26 Za 81:11; Kut 32:9; Mdo 7:51; Yer 16:12; Lk 11:27Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’

277:27 Eze 2:7; Zek 7:13; Eze 3:7; Isa 65:12“Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu. 28Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao. 297:29 Isa 15:2; Hos 11:8; Mik 5:3; Law 21:5; Ay 1:20; Yer 4:8; 6:30; 12:7Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.

Bonde La Machinjo

307:30 Yer 2:7; 32:34; Eze 7:20-22; Law 20:3“ ‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi. 317:31 2Fal 23:10; Law 18:21; Za 106:38; Eze 20:31; Mik 6:7; Yos 15:8; 2Nya 33:6Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu. 327:32 Yer 19:6; 19:11Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi. 337:33 Kum 28:26; Eze 29:5; Mwa 15:11; Yer 6:11; 14:16Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza. 347:34 Hos 2:11; Isa 24:8; Eze 26:13; Ufu 18:23; Zek 7:14; Mt 23:38; Isa 24:7-12Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 7:1-34

聖殿講道

1耶和華對耶利米說: 2「你站在耶和華殿的門口這樣宣告,『從這些門進殿敬拜耶和華的猶大人啊,你們要聽耶和華的話。 3以色列的上帝——萬軍之耶和華說,你們改過自新,我便讓你們在這裡安居。 4你們不要相信那些謊言,說這是耶和華的殿,這是耶和華的殿,這是耶和華的殿。

5「『如果你們真正改過自新,彼此公平相待, 6不欺壓異鄉人和孤兒寡婦,不在這地方濫殺無辜,不拜其他神明自取毀滅, 7我便讓你們在這塊我永遠賜給你們祖先的土地上安居。

8「『然而,你們竟相信那些空洞的謊言。 9你們偷盜、謀殺、通姦、起假誓、向巴力獻祭、拜素不認識的神明, 10然後來到這用來敬拜我的殿,站在我面前說自己安全了,以為可以繼續做可憎之事。 11難道這用來敬拜我的殿在你們眼中竟成了賊窩?這些事,我都看在眼裡。這是耶和華說的。

12「『你們去我曾選為我名所在之地的示羅,看看我是怎樣因我以色列子民的罪而懲罰那地方的。 13我對你們的所作所為一再提出警告,你們卻充耳不聞;我呼喚你們,你們卻不回應。這是耶和華說的。 14因此,我要像對付示羅一樣對付你們所倚靠的這用來敬拜我的殿,對付我賜給你們和你們祖先的土地。 15我要把你們從我面前趕走,好像從前趕走你們的弟兄以法蓮7·15 以法蓮」此處指「北國以色列」。人一樣。』」

16耶和華說:「耶利米啊,不要為這些百姓禱告,不要替他們哀求,不要為他們向我祈求,因為我必不聽。 17你沒有看見他們在猶大各城和耶路撒冷街道上所做的事嗎? 18孩子拾柴,父親點火,婦人揉麵做餅向天后獻祭,向別的神明奠酒,惹我發怒。 19耶和華說,『難道他們是在惹我發怒嗎?難道他們不是自害己身,自取羞辱嗎?』 20主耶和華說,『我要向這地方的人、牲畜、田野的樹木和地裡的出產發怒,發烈怒,如無法熄滅的火。』」

21以色列的上帝——萬軍之耶和華說:「你們把平安祭連同燔祭都拿去吃吧! 22因為我把你們祖先帶出埃及的時候,並沒有吩咐他們獻燔祭或其他祭物, 23只吩咐他們,『你們要聽從我的話,我就做你們的上帝,你們做我的子民;你們遵行我的吩咐,就必蒙福。』 24他們卻掩耳不聽,一意孤行,任意行惡,越來越壞。 25從你們的祖先離開埃及那天起,一直到今天,我日復一日地差遣我的僕人——眾先知到你們那裡, 26但你們掩耳不聽,頑固不化,比你們的祖先更邪惡。 27耶利米啊,你將這番話告訴他們,他們也不會聽;你向他們呼籲,他們也不會回應。 28你要對他們說,『你們這些國民不聽你們上帝耶和華的話,不肯受管教,口中毫無真理。

29『你們要剪掉頭髮,

在光禿的山上哀哭,

因為耶和華已棄絕這惹祂發怒的百姓。』」

30耶和華說:「猶大人做了我視為邪惡的事,把可憎的偶像放在用來敬拜我的聖殿中,玷污了聖殿。 31他們在欣嫩子谷的陀斐特建造邱壇,焚燒自己的兒女。我從未吩咐他們這樣做,連想都沒想過。這不是我的吩咐,我也從未這樣想過。 32因此,看啊,時候將到,那地方必不再叫陀斐特欣嫩子谷,而要叫殺戮谷。那裡要埋葬死人,直到無處可埋。這是耶和華說的。 33飛鳥和走獸必吃這百姓的屍體,無人驅趕牠們。 34我要使猶大各城和耶路撒冷街上的歡樂聲、新郎和新娘的歡笑聲全部消失,因為大地必荒涼。」