Yeremia 6 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 6:1-30

Yerusalemu Imezingirwa Na Jeshi

16:1 Yos 18:28; Neh 3:14; Yer 4:6; Hes 10:7; Yer 4:21; 2Nya 11:6“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini!

Kimbieni kutoka Yerusalemu!

Pigeni tarumbeta katika Tekoa!

Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu!

Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini,

na uharibifu wa kutisha.

26:2 Za 9:14; Mao 4:5Nitamwangamiza Binti Sayuni,

aliye mzuri sana na mwororo.

36:3 Yer 12:10; 2Fal 25:4; Lk 19:43Wachungaji pamoja na makundi yao

watakuja dhidi yake;

watapiga mahema yao kumzunguka,

kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”

46:4 Yer 15:8; 22:7“Jiandaeni kwa vita dhidi yake!

Inukeni tumshambulie mchana!

Lakini, ole wetu, mchana unaisha,

na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.

5Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku,

na kuharibu ngome zake!”

66:6 Kum 20:19-20; 2Sam 20:15; Eze 26:6-8; Kum 28:33; Yer 25:38; Sef 3:1Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Kateni miti mjenge boma

kuzunguka Yerusalemu.

Mji huu ni lazima uadhibiwe,

umejazwa na uonevu.

76:7 Isa 58:4; Yer 20:8; Mik 7:2-3; Za 55:9-11Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake,

ndivyo anavyomwaga uovu wake.

Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake,

ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.

86:8 Eze 23:18; Hos 9:12Pokea onyo, ee Yerusalemu,

la sivyo nitageukia mbali nawe

na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa,

asiweze mtu kuishi ndani yake.”

9Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli

kwa uangalifu kama kwenye mzabibu;

pitisha mkono wako kwenye matawi tena,

kama yeye avunaye zabibu.”

106:10 Kut 6:12; Yer 15:10-15; Mdo 7:51; Yer 20:8; 7:13; 35:15; Isa 42:20Niseme na nani na kumpa onyo?

Ni nani atakayenisikiliza mimi?

Masikio yao yameziba,6:10 Masikio yameziba kwa Kiebrania ina maana kwamba masikio yao hayajatahiriwa.

kwa hiyo hawawezi kusikia.

Neno la Bwana ni chukizo kwao,

hawalifurahii.

116:11 Yer 7:20; Ay 32:20; 2Nya 36:17; Isa 40:30; Yer 15:17; Mao 2:21Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana,

nami siwezi kuizuia.

“Wamwagie watoto walioko barabarani,

na juu ya vijana waume waliokusanyika;

mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake,

hata nao wazee waliolemewa na miaka.

126:12 Kum 28:30; Yer 8:10; Mik 2:4; Yer 43:6; Sef 1:4; Eze 6:14; Yer 43:6; 38:22Nyumba zao zitapewa watu wengine,

pamoja na mashamba yao na wake zao,

nitakapounyoosha mkono wangu

dhidi ya wale waishio katika nchi,”

asema Bwana.

136:13 Isa 56:11; Yer 8:10; Mao 4:13; Yer 2:29“Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa,

wote wana tamaa ya kupata faida zaidi;

manabii na makuhani wanafanana,

wote wanafanya udanganyifu.

146:14 Eze 13:10; Isa 30:10; Yer 4; 10Wanafunga majeraha ya watu wangu

bila uangalifu.

Wanasema, ‘Amani, amani,’

wakati hakuna amani.

156:15 Mik 3:7; Zek 13:7; Yer 3:3; 8:10-12; 2Nya 25:16; Yer 27:15Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao

inayochukiza mno?

Hapana, hawana aibu hata kidogo;

hawajui hata kuona haya.

Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka,

watashushwa chini nitakapowaadhibu,”

asema Bwana.

166:16 Yer 18:15; Lk 16:29; Yos 1:13; Mt 11:29; 1Fal 8:36; Isa 11:10Hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Simama kwenye njia panda utazame,

ulizia mapito ya zamani,

ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo,

nanyi mtapata raha nafsini mwenu.

Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’

176:17 Yer 25:4; Isa 52:8; Eze 3:17; 33:4; Kut 20:18; Yer 11:7-8Niliweka walinzi juu yenu na kusema,

‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’

Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’

186:18 Mit 1:31; Eze 20:13; Kum 4:26; Amo 2:4; Yer 22:29; Yos 23:15; Yer 11:11; 29:19Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa,

angalieni, enyi mashahidi,

lile litakalowatokea.

19Sikia, ee nchi:

Ninaleta maafa juu ya watu hawa,

matunda ya mipango yao,

kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu

na wameikataa sheria yangu.

206:20 Kut 30:23; Isa 60:6; Amo 5:22; Za 50:8-10; Hos 8:13; Mik 6:6-8; Mwa 10:7Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba,

au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali?

Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki,

dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”

216:21 Isa 8:14; Ay 5:12; Yer 13:16; Law 26:37Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa.

Baba na wana wao watajikwaa juu yake,

majirani na marafiki wataangamia.”

226:22 Yer 4:6; Kum 28:49Hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Tazama, jeshi linakuja

kutoka nchi ya kaskazini,

taifa kubwa linaamshwa

kutoka miisho ya dunia.

236:23 Isa 5:30; 13:18; Yer 4:29; Za 18:4; 93:3; Isa 10:32Wamejifunga pinde na mkuki,

ni wakatili na hawana huruma.

Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao.

Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita

ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”

246:24 Za 48:6; Yer 4:19, 31; 50:41-43; Isa 13:7Tumesikia taarifa zao,

nayo mikono yetu imelegea.

Uchungu umetushika,

maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.

256:25 Ay 15:21; Za 31:13; Amo 5:6; Yer 49:29Usitoke kwenda mashambani

au kutembea barabarani,

kwa kuwa adui ana upanga,

na kuna vitisho kila upande.

266:26 Yer 4:8; Ay 2:8; Yon 3:6; Zek 12:10; Mwa 12:16; Yer 25:34; Eze 27:30; Kut 12:23Enyi watu wangu, vaeni magunia

mjivingirishe kwenye majivu,

ombolezeni kwa kilio cha uchungu

kama amliliaye mwana pekee,

kwa maana ghafula

mharabu atatujia.

276:27 Yer 9:7; Zek 13:9“Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma,

nao watu wangu kama mawe yenye madini,

ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.

286:28 Yer 5:23; Eze 22:18; Yer 9:4; Law 19:16Wote ni waasi sugu,

wakienda huku na huko kusengenya.

Wao ni shaba na chuma,

wote wanatenda upotovu.

29Mivuo inavuma kwa nguvu,

kinachoungua kwa huo moto ni risasi,

lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure;

waovu hawaondolewi.

306:30 Za 53:5; Mao 5:22; Hos 9:17; Mit 17:3; Eze 22; 18; Yer 7:29Wanaitwa fedha iliyokataliwa,

kwa sababu Bwana amewakataa.”

New International Version

Jeremiah 6:1-30

Jerusalem Under Siege

1“Flee for safety, people of Benjamin!

Flee from Jerusalem!

Sound the trumpet in Tekoa!

Raise the signal over Beth Hakkerem!

For disaster looms out of the north,

even terrible destruction.

2I will destroy Daughter Zion,

so beautiful and delicate.

3Shepherds with their flocks will come against her;

they will pitch their tents around her,

each tending his own portion.”

4“Prepare for battle against her!

Arise, let us attack at noon!

But, alas, the daylight is fading,

and the shadows of evening grow long.

5So arise, let us attack at night

and destroy her fortresses!”

6This is what the Lord Almighty says:

“Cut down the trees

and build siege ramps against Jerusalem.

This city must be punished;

it is filled with oppression.

7As a well pours out its water,

so she pours out her wickedness.

Violence and destruction resound in her;

her sickness and wounds are ever before me.

8Take warning, Jerusalem,

or I will turn away from you

and make your land desolate

so no one can live in it.”

9This is what the Lord Almighty says:

“Let them glean the remnant of Israel

as thoroughly as a vine;

pass your hand over the branches again,

like one gathering grapes.”

10To whom can I speak and give warning?

Who will listen to me?

Their ears are closed6:10 Hebrew uncircumcised

so they cannot hear.

The word of the Lord is offensive to them;

they find no pleasure in it.

11But I am full of the wrath of the Lord,

and I cannot hold it in.

“Pour it out on the children in the street

and on the young men gathered together;

both husband and wife will be caught in it,

and the old, those weighed down with years.

12Their houses will be turned over to others,

together with their fields and their wives,

when I stretch out my hand

against those who live in the land,”

declares the Lord.

13“From the least to the greatest,

all are greedy for gain;

prophets and priests alike,

all practice deceit.

14They dress the wound of my people

as though it were not serious.

‘Peace, peace,’ they say,

when there is no peace.

15Are they ashamed of their detestable conduct?

No, they have no shame at all;

they do not even know how to blush.

So they will fall among the fallen;

they will be brought down when I punish them,”

says the Lord.

16This is what the Lord says:

“Stand at the crossroads and look;

ask for the ancient paths,

ask where the good way is, and walk in it,

and you will find rest for your souls.

But you said, ‘We will not walk in it.’

17I appointed watchmen over you and said,

‘Listen to the sound of the trumpet!’

But you said, ‘We will not listen.’

18Therefore hear, you nations;

you who are witnesses,

observe what will happen to them.

19Hear, you earth:

I am bringing disaster on this people,

the fruit of their schemes,

because they have not listened to my words

and have rejected my law.

20What do I care about incense from Sheba

or sweet calamus from a distant land?

Your burnt offerings are not acceptable;

your sacrifices do not please me.”

21Therefore this is what the Lord says:

“I will put obstacles before this people.

Parents and children alike will stumble over them;

neighbors and friends will perish.”

22This is what the Lord says:

“Look, an army is coming

from the land of the north;

a great nation is being stirred up

from the ends of the earth.

23They are armed with bow and spear;

they are cruel and show no mercy.

They sound like the roaring sea

as they ride on their horses;

they come like men in battle formation

to attack you, Daughter Zion.”

24We have heard reports about them,

and our hands hang limp.

Anguish has gripped us,

pain like that of a woman in labor.

25Do not go out to the fields

or walk on the roads,

for the enemy has a sword,

and there is terror on every side.

26Put on sackcloth, my people,

and roll in ashes;

mourn with bitter wailing

as for an only son,

for suddenly the destroyer

will come upon us.

27“I have made you a tester of metals

and my people the ore,

that you may observe

and test their ways.

28They are all hardened rebels,

going about to slander.

They are bronze and iron;

they all act corruptly.

29The bellows blow fiercely

to burn away the lead with fire,

but the refining goes on in vain;

the wicked are not purged out.

30They are called rejected silver,

because the Lord has rejected them.”