Yeremia 6 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 6:1-30

Yerusalemu Imezingirwa Na Jeshi

16:1 Yos 18:28; Neh 3:14; Yer 4:6; Hes 10:7; Yer 4:21; 2Nya 11:6“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini!

Kimbieni kutoka Yerusalemu!

Pigeni tarumbeta katika Tekoa!

Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu!

Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini,

na uharibifu wa kutisha.

26:2 Za 9:14; Mao 4:5Nitamwangamiza Binti Sayuni,

aliye mzuri sana na mwororo.

36:3 Yer 12:10; 2Fal 25:4; Lk 19:43Wachungaji pamoja na makundi yao

watakuja dhidi yake;

watapiga mahema yao kumzunguka,

kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”

46:4 Yer 15:8; 22:7“Jiandaeni kwa vita dhidi yake!

Inukeni tumshambulie mchana!

Lakini, ole wetu, mchana unaisha,

na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.

5Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku,

na kuharibu ngome zake!”

66:6 Kum 20:19-20; 2Sam 20:15; Eze 26:6-8; Kum 28:33; Yer 25:38; Sef 3:1Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Kateni miti mjenge boma

kuzunguka Yerusalemu.

Mji huu ni lazima uadhibiwe,

umejazwa na uonevu.

76:7 Isa 58:4; Yer 20:8; Mik 7:2-3; Za 55:9-11Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake,

ndivyo anavyomwaga uovu wake.

Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake,

ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.

86:8 Eze 23:18; Hos 9:12Pokea onyo, ee Yerusalemu,

la sivyo nitageukia mbali nawe

na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa,

asiweze mtu kuishi ndani yake.”

9Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli

kwa uangalifu kama kwenye mzabibu;

pitisha mkono wako kwenye matawi tena,

kama yeye avunaye zabibu.”

106:10 Kut 6:12; Yer 15:10-15; Mdo 7:51; Yer 20:8; 7:13; 35:15; Isa 42:20Niseme na nani na kumpa onyo?

Ni nani atakayenisikiliza mimi?

Masikio yao yameziba,6:10 Masikio yameziba kwa Kiebrania ina maana kwamba masikio yao hayajatahiriwa.

kwa hiyo hawawezi kusikia.

Neno la Bwana ni chukizo kwao,

hawalifurahii.

116:11 Yer 7:20; Ay 32:20; 2Nya 36:17; Isa 40:30; Yer 15:17; Mao 2:21Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana,

nami siwezi kuizuia.

“Wamwagie watoto walioko barabarani,

na juu ya vijana waume waliokusanyika;

mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake,

hata nao wazee waliolemewa na miaka.

126:12 Kum 28:30; Yer 8:10; Mik 2:4; Yer 43:6; Sef 1:4; Eze 6:14; Yer 43:6; 38:22Nyumba zao zitapewa watu wengine,

pamoja na mashamba yao na wake zao,

nitakapounyoosha mkono wangu

dhidi ya wale waishio katika nchi,”

asema Bwana.

136:13 Isa 56:11; Yer 8:10; Mao 4:13; Yer 2:29“Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa,

wote wana tamaa ya kupata faida zaidi;

manabii na makuhani wanafanana,

wote wanafanya udanganyifu.

146:14 Eze 13:10; Isa 30:10; Yer 4; 10Wanafunga majeraha ya watu wangu

bila uangalifu.

Wanasema, ‘Amani, amani,’

wakati hakuna amani.

156:15 Mik 3:7; Zek 13:7; Yer 3:3; 8:10-12; 2Nya 25:16; Yer 27:15Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao

inayochukiza mno?

Hapana, hawana aibu hata kidogo;

hawajui hata kuona haya.

Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka,

watashushwa chini nitakapowaadhibu,”

asema Bwana.

166:16 Yer 18:15; Lk 16:29; Yos 1:13; Mt 11:29; 1Fal 8:36; Isa 11:10Hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Simama kwenye njia panda utazame,

ulizia mapito ya zamani,

ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo,

nanyi mtapata raha nafsini mwenu.

Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’

176:17 Yer 25:4; Isa 52:8; Eze 3:17; 33:4; Kut 20:18; Yer 11:7-8Niliweka walinzi juu yenu na kusema,

‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’

Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’

186:18 Mit 1:31; Eze 20:13; Kum 4:26; Amo 2:4; Yer 22:29; Yos 23:15; Yer 11:11; 29:19Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa,

angalieni, enyi mashahidi,

lile litakalowatokea.

19Sikia, ee nchi:

Ninaleta maafa juu ya watu hawa,

matunda ya mipango yao,

kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu

na wameikataa sheria yangu.

206:20 Kut 30:23; Isa 60:6; Amo 5:22; Za 50:8-10; Hos 8:13; Mik 6:6-8; Mwa 10:7Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba,

au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali?

Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki,

dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”

216:21 Isa 8:14; Ay 5:12; Yer 13:16; Law 26:37Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa.

Baba na wana wao watajikwaa juu yake,

majirani na marafiki wataangamia.”

226:22 Yer 4:6; Kum 28:49Hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Tazama, jeshi linakuja

kutoka nchi ya kaskazini,

taifa kubwa linaamshwa

kutoka miisho ya dunia.

236:23 Isa 5:30; 13:18; Yer 4:29; Za 18:4; 93:3; Isa 10:32Wamejifunga pinde na mkuki,

ni wakatili na hawana huruma.

Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao.

Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita

ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”

246:24 Za 48:6; Yer 4:19, 31; 50:41-43; Isa 13:7Tumesikia taarifa zao,

nayo mikono yetu imelegea.

Uchungu umetushika,

maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.

256:25 Ay 15:21; Za 31:13; Amo 5:6; Yer 49:29Usitoke kwenda mashambani

au kutembea barabarani,

kwa kuwa adui ana upanga,

na kuna vitisho kila upande.

266:26 Yer 4:8; Ay 2:8; Yon 3:6; Zek 12:10; Mwa 12:16; Yer 25:34; Eze 27:30; Kut 12:23Enyi watu wangu, vaeni magunia

mjivingirishe kwenye majivu,

ombolezeni kwa kilio cha uchungu

kama amliliaye mwana pekee,

kwa maana ghafula

mharabu atatujia.

276:27 Yer 9:7; Zek 13:9“Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma,

nao watu wangu kama mawe yenye madini,

ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.

286:28 Yer 5:23; Eze 22:18; Yer 9:4; Law 19:16Wote ni waasi sugu,

wakienda huku na huko kusengenya.

Wao ni shaba na chuma,

wote wanatenda upotovu.

29Mivuo inavuma kwa nguvu,

kinachoungua kwa huo moto ni risasi,

lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure;

waovu hawaondolewi.

306:30 Za 53:5; Mao 5:22; Hos 9:17; Mit 17:3; Eze 22; 18; Yer 7:29Wanaitwa fedha iliyokataliwa,

kwa sababu Bwana amewakataa.”

King James Version

Jeremiah 6:1-30

1O ye children of Benjamin, gather yourselves to flee out of the midst of Jerusalem, and blow the trumpet in Tekoa, and set up a sign of fire in Beth-haccerem: for evil appeareth out of the north, and great destruction. 2I have likened the daughter of Zion to a comely and delicate woman.6.2 comely: or, dwelling at home 3The shepherds with their flocks shall come unto her; they shall pitch their tents against her round about; they shall feed every one in his place. 4Prepare ye war against her; arise, and let us go up at noon. Woe unto us! for the day goeth away, for the shadows of the evening are stretched out. 5Arise, and let us go by night, and let us destroy her palaces.

6¶ For thus hath the LORD of hosts said, Hew ye down trees, and cast a mount against Jerusalem: this is the city to be visited; she is wholly oppression in the midst of her.6.6 cast…: or, pour out the engine of shot 7As a fountain casteth out her waters, so she casteth out her wickedness: violence and spoil is heard in her; before me continually is grief and wounds. 8Be thou instructed, O Jerusalem, lest my soul depart from thee; lest I make thee desolate, a land not inhabited.6.8 depart: Heb. be loosed, or, disjointed

9¶ Thus saith the LORD of hosts, They shall throughly glean the remnant of Israel as a vine: turn back thine hand as a grapegatherer into the baskets. 10To whom shall I speak, and give warning, that they may hear? behold, their ear is uncircumcised, and they cannot hearken: behold, the word of the LORD is unto them a reproach; they have no delight in it. 11Therefore I am full of the fury of the LORD; I am weary with holding in: I will pour it out upon the children abroad, and upon the assembly of young men together: for even the husband with the wife shall be taken, the aged with him that is full of days. 12And their houses shall be turned unto others, with their fields and wives together: for I will stretch out my hand upon the inhabitants of the land, saith the LORD. 13For from the least of them even unto the greatest of them every one is given to covetousness; and from the prophet even unto the priest every one dealeth falsely. 14They have healed also the hurt of the daughter of my people slightly, saying, Peace, peace; when there is no peace.6.14 hurt: Heb. bruise, or, breach 15Were they ashamed when they had committed abomination? nay, they were not at all ashamed, neither could they blush: therefore they shall fall among them that fall: at the time that I visit them they shall be cast down, saith the LORD. 16Thus saith the LORD, Stand ye in the ways, and see, and ask for the old paths, where is the good way, and walk therein, and ye shall find rest for your souls. But they said, We will not walk therein. 17Also I set watchmen over you, saying, Hearken to the sound of the trumpet. But they said, We will not hearken.

18¶ Therefore hear, ye nations, and know, O congregation, what is among them. 19Hear, O earth: behold, I will bring evil upon this people, even the fruit of their thoughts, because they have not hearkened unto my words, nor to my law, but rejected it. 20To what purpose cometh there to me incense from Sheba, and the sweet cane from a far country? your burnt offerings are not acceptable, nor your sacrifices sweet unto me. 21Therefore thus saith the LORD, Behold, I will lay stumblingblocks before this people, and the fathers and the sons together shall fall upon them; the neighbour and his friend shall perish. 22Thus saith the LORD, Behold, a people cometh from the north country, and a great nation shall be raised from the sides of the earth. 23They shall lay hold on bow and spear; they are cruel, and have no mercy; their voice roareth like the sea; and they ride upon horses, set in array as men for war against thee, O daughter of Zion. 24We have heard the fame thereof: our hands wax feeble: anguish hath taken hold of us, and pain, as of a woman in travail. 25Go not forth into the field, nor walk by the way; for the sword of the enemy and fear is on every side.

26¶ O daughter of my people, gird thee with sackcloth, and wallow thyself in ashes: make thee mourning, as for an only son, most bitter lamentation: for the spoiler shall suddenly come upon us. 27I have set thee for a tower and a fortress among my people, that thou mayest know and try their way. 28They are all grievous revolters, walking with slanders: they are brass and iron; they are all corrupters. 29The bellows are burned, the lead is consumed of the fire; the founder melteth in vain: for the wicked are not plucked away. 30Reprobate silver shall men call them, because the LORD hath rejected them.6.30 Reprobate…: or, Refuse silver